Nahitaji kurudi nyumbani

Nahitaji kurudi nyumbani

Mankaa

Senior Member
Joined
Jan 21, 2012
Posts
156
Reaction score
49
Habari zenu wapendwa, imani yangu ni kuwa mu wazima,

Kuna tatizo hapa, asubuhi ya leo nimekaa najiandaa kutoka kaja binamu wa mume wangu na mabegi kuuliza eti amekuja kukaa nyumbani kwangu asome chuo.

Kumuhoji kawa mkali eti mimi sina ubinadmu na mambo mengi mabaya nikasema tatizo siyo huyo binti kuja tatizo kwa nini hakunijulisha kama walishapanga amlete hapo nyumbani.

Nilichofikiria mimi naondoka niende nyumbani kwetu kidogo nirudi baada ya wiki moja coz haya mambo hata katika familia nilivyokulia baba hawezi fanya kitu kama hicho bila kumjulisha mama.

Hapa nipo sahihi wapendwa?
 
mmmmhh!!!!KWANINI?HEBU KUWA NA MSIMAMO WAKO KUWA UNAUWEZO WA KUMSAIDIA KAKA YAKE ILA KAMA HUYO BINT ANAKUJA KWA MDA NA KWENDA CHUO SIO MBAYA MUACHE KAMA KWELI HAUTAKUWA MZIGO KWAKO MAANA WASIJE WAKAZANI GHARAMA ZOTE NI WW UNAZITOA AAAH KUWA NA MSIMAMO LOO
 
haupo sahihi mpendwa a.k.a twin wangu kwanin uondoke nyumban kwako??? ama hutaki wageni hizi familia za nuclear ziliisha zaman saiv kuna ujamaa ati. hapo umeletewa binamu unataka urud kwenu ingekuwa ndio mtoto wa mume kaja si ungejiua kabisa? wageni ni baraka ndugu
 
mmmmhh!!!!KWANINI?HEBU KUWA NA MSIMAMO WAKO KUWA UNAUWEZO WA KUMSAIDIA KAKA YAKE ILA KAMA HUYO BINT ANAKUJA KWA MDA NA KWENDA CHUO SIO MBAYA MUACHE KAMA KWELI HAUTAKUWA MZIGO KWAKO MAANA WASIJE WAKAZANI GHARAMA ZOTE NI WW UNAZITOA AAAH KUWA NA MSIMAMO LOO

Gharama za ada wanadai watalipa wao ila mwngne kama nauli hadi chuo ni 3000per day hujaweka chakula na mengne na sijajipanga nimeshtukizwa nashindwa nifanyaje
 
Mwenzako kafanya kosa kwa kutokushirikisha katka suala kama hilo. Hata hivyo uamuz wa kuondoka uache familia si mzuri nadhani bado mna muda wa kukaa mkazungumza juu ya hilo hata kama kosa la awali lishafanyika. Hiyo ni familia yako na we kama mama una mchango mkubwa kuhakikisha inakaa stable. Kitendo cha kuondoka hata kama ni wiki kinaweza kuwa na madhara makubwa kuliko unavyoweza kufikiria
 
Yaani hata ujampa muda mgeni aweke mizigo ushalianzisha duh asubui ya leo, leo leo umepanga kuondoka hata kama hakukushirikisha ilo ni jambo la kuongea...kuna watu wana roho mbaya hata mwanaume kumnunulia mama mzazi kipande cha khanga anakatazwa nshapata mashaka na wewe na nahisi ndio maana ameku suprize
 
Wanawake wengine bana ni Viazi, inamaana wewe mtu akitaka kuja kwa mmeo lazima akwambie wewe ndio umpe Visa ama? Nathubutu kusema ni utoto unakusumbua na pili ni kwakuwa hauna watoto bila shaka ndio maana!
 
Gharama za ada wanadai watalipa wao ila mwngne kama nauli hadi chuo ni 3000per day hujaweka chakula na mengne na sijajipanga nimeshtukizwa nashindwa nifanyaje

pole sana kwa hilo kaa na mwenzio myarekebishe yaishe unajua kufumba macho sio njia ya kuikwepa ngumi ya uso
 
Tatizo threads zako huwa haziaminiki bi mkubwa...
 
Kufanya jambo bila kukuuliza haikuwa vizuri lakini inategemea ulivyomzoeza yawezekana mambo mengi hufanya bila kukushirikisha hivyo hata hili amechukulia ni la kawaida tu.

tatizo lako liko kwenye kauli yako hii
Nilichofikiria mimi naondoka niende nyumbani kwetu kidogo nirud baada ya wiki moja coZ haya mambo hata katika familia nilivyokulia baba hawezi fanya kitu kama hicho bila kumjulisha mama
Hapa nipo sahihi wapendwa?

Mnapoamua kuoana na kuwaacha wazazi wenu hamwezi kuiendesha familia kwa kucopy na ku paste kutoka kwa wazazi wenu ndoa itakuwa ngumu sana,ila ni kuanza maisha kwa mfumo mnaokubaliana,siyo eti mume wangu hanitoi out kama baba alivyokuwa anamtoa mama.

Kukimbia tatizo siyo suluhisho maana hiyo wiki ikiisha utawakuta wapo then unafanyaje.cha msingi kwa sababu ameshawaleta wewe kubaliane na hali hiyo atamaliza chuo na atarudi kwao.maana unaweza kuondoka na akatumia hiyo kama njia ya kutafuta nyumba ndogo na kukuanzishia visa ili uondoke kwake.

"Nguvu zenu zitakuwa katika kutulia na kutumaini."



 
Usiondoke,si kaja kusoma tu akimaliza shule anaondoka zake,mimi kwangu nina wifi yangu ninakaa nae tokea niolewe,yaani nimeolewa tu akaja,nina shemeji zangu 3,na nina mtoto wa shemeji yangu 1,mtoto wa mme wangu 1,na wanangu watatu.Wewe kuletewa huyo tu mmoja tena kuna sababu kabisa ambayo kaja kusoma tu,Binti tulia kwako huyo anapita tu.Kama mme hajakujulisha samehe tu,itakuwa yeye alichukulia easy tu
 
Nimegundua mumeo hajakushirikisha c anajua una roho ya korosho.
 
baba ndo kichwa cha nyumba sema amekosea hakukutaarifu ila kuondoka sio solution
 
Habari zenu wapendwa, imani yangu ni kuwa mu wazima,

.......haya mambo hata katika familia nilivyokulia baba hawezi fanya kitu kama hicho bila kumjulisha mama.....


Ondoka uende ukute mchepuko, kisha urudi hapa utuambie maana naona hata huamini km hapo ni kwako na kama hapo ni alpha na omega kwako. Kwa baba yako lazima pawe tofauti na kwako. Unatakiwa ukae na mmeo hata km ni mkali kiasi gani. Msubirie akiwa ktk furaha afu muingizie topic kiulaini. Hapo ni kwako na haitafanana kamwe na kwenu. Inaonekana ndio stahili ya maisha mme wako kuku suprise. Na hii mlikosea tangu mwanzo wa mapenzi yenu. Hivyo kaa naye muanze upya kupanga mipango ya nyumbani. Saidieni wasiojiweza kila mlipo na uwezo. Je, hapendezi iwapo una jambo la maana kwa mumeo, ukalirudia rudia kila anapokuwa ametulia hadi lipate kibali? Je, ni sahihi kukimbilia kwenu wkt kuna shida ktk maisha yenu ya ndoa? Fikiria!
 
Habari zenu wapendwa, imani yangu ni kuwa mu wazima,

Kuna tatizo hapa, asubuhi ya leo nimekaa najiandaa kutoka kaja binamu wa mume wangu na mabegi kuuliza eti amekuja kukaa nyumbani kwangu asome chuo.

Kumuhoji kawa mkali eti mimi sina ubinadmu na mambo mengi mabaya nikasema tatizo siyo huyo binti kuja tatizo kwa nini hakunijulisha kama walishapanga amlete hapo nyumbani.

Nilichofikiria mimi naondoka niende nyumbani kwetu kidogo nirudi baada ya wiki moja coz haya mambo hata katika familia nilivyokulia baba hawezi fanya kitu kama hicho bila kumjulisha mama.

Hapa nipo sahihi wapendwa?

Wachagga kwa roho mbaya mmezidi,..mgeni kafika asubuhi umejiandaa kwenda kazini umeona ugombe kwanza kwanini mgen kaja bila kujali utachelewa kazini....huyu mume wako ni lazima atakua ni kabila tofauti na wewe na anajua una roho mbaya ndio maana kaona asikuambie,....nampa big_up huyo jamaa....you just go back to your parent..and never come back.
 
wewe ndio utakuwa boya zaidi coz mwenzio kafanya kosa na ww umetambua kuwa kafanya kosa.
ingawa anaweza akawa yupo sahihi kufanya hivyo sababu hatujui life style yenu mwaishije yawezekana ndio kawaida yenu.
sasa kama huyo mgeni kaja bila ww kupewa taarifa badala ya kukaa chini na mzungumze ww unaikimbia nyumba na kama atakaa hapo miaka mpaka amalize CHUO inamaana ndio utakuwa ushajipiga taraka??

inavyoonekana ww nimkolini sana tena nimgoroko sana koro hutaki wageni vitu vingine vidogo tuu unacomplicate sana.
kwani hata kama hizi garama utagaramikia ww kunatatizo gani??anayekupa riziki ndio mpanga wa yote anayajua hayo so atakuongezea tuu na kukufungulia milango mingi ya riziki harafu kumvuka kunaleo na kesho..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom