Mkuu umetumia kigezo gani kuniita mimi kuwa Sina Akili na wewe Kujipambanua kuwa una akili kupitia kwa huyo Classmate wako anayepandishwa Vyeo kupitia sheria za Magereza ambazo hazina ushindani???Wewe akili huna siwezi kupoteza muda wangu na wewe.
Kwa taarifa yako classmate wangu ana degree ya sheria ndio inayompandisha vyeo na siyo kupiga kwata.
Ukisikia askari unadhani hawana fani zao mpuuzi sana wewe.
Isitoshe hiyo system ya kutumikia kifungo 1/3 imewekwa na magereza wenyewe.
Kwanza nahitaji kujua kuna ushahidi upi wa waziwazi ambao ulimtia hatiani akafungwa, hata hao mashahidi hakuna aliyeona kama kamuua bila kukusudia. Walikuwepo wawili tu ndani, sijaelewa kwa mantiki ipi akahitimishiwa na kufungwa. Niseme tu hapa kuna namna, pia mawakili wa kumtetea ndiyo wamemtia binti shimoni utetezi wao haukuwa msaada.Sawa ni kweli kwamba Mwanao alifariki akiwa na huyo Binti katika Starehe zao na hata hivyo Marehemu Mwanao nae kama kungekuwa kuna uwezekano na Sheria za Kuhukumu Maiti basi yawezekana hata Yeye pia huko huko aliko mavumbini basi angehukumiwa Kifungo cha miaka 30 kwa kufanya Mapenzi na Binti aliye chini ya Umri wa miaka 18.
Mpaka sasa nawaza na akili yangu imegoma kabisa kuelewa baadhi ya matukio yanayohitaji mno tafakuri tunduizi ( critical thinking ) ya kilichotokea jana katika Nyumba moja ya Sheria na Utoaji wa hukumu nchini Tanzania maeneo ya Posta.
Hivi Mama wa Marehemu amepata faida gani labda kwa kufurahia Binti mdogo kwenda Lupango kwa miezi 24? Hivi Mama wa Marehemu kitendo cha kutoka pale Nyumba ya Sheria na Hukumu Posta huku akifurahi na moja kwa moja kwenda alipolala Mwanae Kinondoni kumsalimia kilikuwa kina maanisha nini?
Kama ni mashindano je Mama wa Marehemu alikuwa anashindana nini na Binti aliyehukumiwa miezi 24 Gerezani? Zile furaha pale Posta zilizokuwa zikisindikizwa na machozi zilitokana na nini hasa? Je baada ya ule ushindi wa Kisheria na Kihukumu wa jana Marehemu ameshafufuka na sasa amerudi Kwake Sinza?
Hivi hapakuwa na room ya mazungumzo yoyote ya Kidiplomasia baina ya pande mbili Kinzani / Hasimu zaidi ya Kukomoana na kuonyeshana nani ni Bingwa / Mshindi? Kwahiyo kumbe siku hizi Wakristo nchini Tanzania tunarudishiana ubaya kwa ubaya ( wenyewe mnasema kama noma na iwe noma ) kwa wale Maadui zetu.
Naomba kuuliza hivi laiti kama zile Mali za aliyelala sasa pale Mtaa wa Mkulima Kinondoni zingekuwepo hadi hivi leo na zinazalisha Mama Marehemu angepoteza muda na Kesi hiyo? Je hapa tukiamini kama labda ukazaji wa Vyuma ndiyo umejenga hasira kwa Mama hadi akaamua Kumkomo Binti wa Watu tutakuwa tumekosea?
Nimalizie tu kwa kusema kwamba huko nyuma nilikuwa nasikia tu kwamba Watanzania japo masikioni mwa wengi wanasifika kwa kuwa Wakarimu ila nilichokigundua na leo mtanisamehe sana ni kwamba hakuna Watu wenye roho mbaya, makatili and pure sadists kama Watanzania kubali kataeni.
Kama Mkristo wa kweli binafsi sikuona haja yoyote ya Mama Marehemu kulishikilia hili jambo bango hivi na badala yake ningesamehe tu na kumuachia kila kitu Mwenyezi Mungu na kuendelea na maisha yangu bila Marehemu nikijua / kuamini kwamba kila jambo hupangwa na Mwenyezi Mungu.
Huyu Mama anaweza kudhani kuwa amefanikiwa 100% ila kwa jicho kali la Kisaikolojia nasema wazi kabisa kwamba Mama Marehemu huenda sasa akawa katika data base yake ndiyo ameharakisha kuongeza idadi kubwa ya Maadui kuliko Marafiki na hali ambayo huenda pia ikampelekea akawa na maisha magumu na ya shida pengine hata kuliko ambapo huyo Binti aliyefungwa angekuwepo uraiani.
Wadau huu ni mtazamo wangu tu na kama na Wewe una wako nakukaribisha sana nawe pia uweze Kutiririka na Kuserereka hapa na jisikie huru kunipinga kwa Hoja kwani hapa Great Thinkers hapa tuunganishe bongo zetu na tulifikirie hili nje ya box kabisa ili tuwekane sawa. Naomba leo katika uzi huu kusiwepo na matusi ya aina yoyote yale ila madongo ya hapa na pale Kwangu nayaruhusu ila siyo matusi. Nimetahadharisha mapema tu ili huko mbele ya safari tusije kulaumiana.
Nawapendeni nyote na karibuni pia.
Nawasilisha.
Mama Kanumba yupo Dar zamani sana hata kabla ya Kanumba kuwa maarufu alienda kwenye msiba Bukoba wakati mwanae anafariki usipotoshe
Nashukuru kwa kunielewa mkuu na sasa ndio naamini kuwa wewe ni great thinkerShikamoo Mkuu hili ' dongo ' limeniingia hadi nabaki kucheka tu hapa sasa. Mkuu leo umenipatia haya bhana!
Kweli hesabu ni janga la kitaifa!kwa hiyo theluthi ya miaka miwili ni mwaka na miezi nane?1/3 ya two years ni mwaka mmoja na miezi minne ndio muda anaopaswa kutumikia Lulu gerezani kwa sheria za Magereza.
Kosa moja alilolifanya Lulu ni kuweka ukaribu wa kupitiliza na mama Kanumba baada ya kutoka jela. Baada ya kukwaruzana mama alikuwa na jazba na Jana alifurahia kale katoto kanakomkosea adabu na kaliko sababisha kifo cha mwanae kanaenda jela.
Kosa moja alilolifanya Lulu ni kuweka ukaribu wa kupitiliza na mama Kanumba baada ya kutoka jela. Baada ya kukwaruzana mama alikuwa na jazba na Jana alifurahia kale katoto kanakomkosea adabu na kaliko sababisha kifo cha mwanae kanaenda jela.
Mkuu umetumia kigezo gani kuniita mimi kuwa Sina Akili na wewe Kujipambanua kuwa una akili kupitia kwa huyo Classmate wako anayepandishwa Vyeo kupitia sheria za Magereza ambazo hazina ushindani???
Kwa Kifupi walikuwa wanachukuwa option yoa kwenda aidha CCP Moshi au Magereza walio wengi hawakuwa wamepata kuchaguliwa kuendelea aidha na Kidato cha tano kwa hiyo from that angle, Kujiiendeleza siyo kigezo kuwa mbobezi kwenye taalum fulani au Kupandishwa Vyeo hasa hivi vya serikalini havina uhusiano na utendaji bali huwa mara nyingi kwa baadhi ya Sekta na Taasisi huangaliwa na Muda uliokaa Nafasi Fulani.
Kwa ushauri siku Nyingine uwe na heshima na unapoongea jinasibu wewe siyo kupitia uliyombiwa na classmate wako.
hahahahahahahaha Umenifurahisha hahahahahaOya acha ' mikwara ' Mbuzi basi sawa? Tuheshimiane kwani humu tunajuana kwa Minyago / Misura yetu? Mara ngapi Mimi kwa mfano tena humu humu huwa napigwa ' Madongo ' ya hatari na sometimes yananiuma lakini Mwanamume nakula tu Kobis / nauchuna na wala silii kama unavyofanya Wewe sasa? Jifunze kuhimili changamoto mbalimbali hasa za Kimtazamo au za maneno ya Kuudhi unayokutana nayo humu. Nadhani humu JF hakuna Member ninayepigwa ' madongo ' kama Mimi GENTAMYCINE lakini hutosikia nalalamika kwa Mtu bali na Mimi sasa hujipanga vizuri na nikirudi nami narudi na ' Kitu ' cha maana kisha tunaheshimiana na maisha yanaenda. Hivi kila Member wa JF akiwa analia lia / ana deka deka kama Wewe hivi hili ' jamvi ' litanoga / litapendeza Kweli? Kuwa kama Mwanaume bhana na tuliomzoea Matola humu wala hatumshangai kwa hayo maneno yako na labda kwa kukushauri tu na Wewe mvizie na mpe ' dongo ' kwa Kujenga hoja nae litamuingia vile vile ila siyo kudekadeka. Acha hizo Mkuu!
Nashukuru kwa kunielewa mkuu na sasa ndio naamini kuwa wewe ni great thinker
Nadhani uelewa ndio janga la Taifa, ni wapi nilipoandika mwaka na miezi nane?Kweli hesabu ni janga la kitaifa!kwa hiyo theluthi ya miaka miwili ni mwaka na miezi nane?
Kesi za mauaji ni Kesi za Jamhuri dhidi ya mtuhumiwa kwa hiyo mama Kanumba hangeweza kusema amesamehe Kesi iondolewe mahakamani mimi naona kosa la mama huyu ni kushangilia adhabu iliyotolewa kwa Lulu
Maelfu na mamilioni ya watanzania wanafiki na hamnazo ndiyo walioomboleza kifo cha huyo mbakaji. Mungu kamchapa yeye na bongo movie yoteAlichoniacha hoi huyo mama ati anaishukuru serikali ya awamu ya tano, haya ni mauzauza matupu hajui hata muhimili wa mahakama ni nini.
Huyu mama kwa mara ya kwanza nilimsikia amekuja kwenye msiba wa Kanumba Dar na mpaka leo amezamia Dar na hana hata mpango na mzazi mwenzanke Baba Kanumba na amejipa haki zote za urithi wa marehemu, huyu mama ni sehemu ya mashetani tunaoishi nao humu duniani wakiwa na maumbo ya binadamu.
Since day one, tulipopata taarifa za kifo cha Kanumba hapa JF mpaka leo msimamo wangu juu ya Kanumba haujawahi kuyumba wala kubadilika, kwangu Kanumba alikuwa ni mbakaji tu na wala si vinginevyo.
Mungu amuweke anapostahili.