GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,694
- 109,132
Sawa ni kweli kwamba Mwanao alifariki akiwa na huyo Binti katika Starehe zao na hata hivyo Marehemu Mwanao nae kama kungekuwa kuna uwezekano na Sheria za Kuhukumu Maiti basi yawezekana hata Yeye pia huko huko aliko mavumbini basi angehukumiwa Kifungo cha miaka 30 kwa kufanya Mapenzi na Binti aliye chini ya Umri wa miaka 18.
Mpaka sasa nawaza na akili yangu imegoma kabisa kuelewa baadhi ya matukio yanayohitaji mno tafakuri tunduizi ( critical thinking ) ya kilichotokea jana katika Nyumba moja ya Sheria na Utoaji wa hukumu nchini Tanzania maeneo ya Posta.
Hivi Mama wa Marehemu amepata faida gani labda kwa kufurahia Binti mdogo kwenda Lupango kwa miezi 24? Hivi Mama wa Marehemu kitendo cha kutoka pale Nyumba ya Sheria na Hukumu Posta huku akifurahi na moja kwa moja kwenda alipolala Mwanae Kinondoni kumsalimia kilikuwa kina maanisha nini?
Kama ni mashindano je Mama wa Marehemu alikuwa anashindana nini na Binti aliyehukumiwa miezi 24 Gerezani? Zile furaha pale Posta zilizokuwa zikisindikizwa na machozi zilitokana na nini hasa? Je baada ya ule ushindi wa Kisheria na Kihukumu wa jana Marehemu ameshafufuka na sasa amerudi Kwake Sinza?
Hivi hapakuwa na room ya mazungumzo yoyote ya Kidiplomasia baina ya pande mbili Kinzani / Hasimu zaidi ya Kukomoana na kuonyeshana nani ni Bingwa / Mshindi? Kwahiyo kumbe siku hizi Wakristo nchini Tanzania tunarudishiana ubaya kwa ubaya ( wenyewe mnasema kama noma na iwe noma ) kwa wale Maadui zetu.
Naomba kuuliza hivi laiti kama zile Mali za aliyelala sasa pale Mtaa wa Mkulima Kinondoni zingekuwepo hadi hivi leo na zinazalisha Mama Marehemu angepoteza muda na Kesi hiyo? Je hapa tukiamini kama labda ukazaji wa Vyuma ndiyo umejenga hasira kwa Mama hadi akaamua Kumkomo Binti wa Watu tutakuwa tumekosea?
Nimalizie tu kwa kusema kwamba huko nyuma nilikuwa nasikia tu kwamba Watanzania japo masikioni mwa wengi wanasifika kwa kuwa Wakarimu ila nilichokigundua na leo mtanisamehe sana ni kwamba hakuna Watu wenye roho mbaya, makatili and pure sadists kama Watanzania kubali kataeni.
Kama Mkristo wa kweli binafsi sikuona haja yoyote ya Mama Marehemu kulishikilia hili jambo bango hivi na badala yake ningesamehe tu na kumuachia kila kitu Mwenyezi Mungu na kuendelea na maisha yangu bila Marehemu nikijua / kuamini kwamba kila jambo hupangwa na Mwenyezi Mungu.
Huyu Mama anaweza kudhani kuwa amefanikiwa 100% ila kwa jicho kali la Kisaikolojia nasema wazi kabisa kwamba Mama Marehemu huenda sasa akawa katika data base yake ndiyo ameharakisha kuongeza idadi kubwa ya Maadui kuliko Marafiki na hali ambayo huenda pia ikampelekea akawa na maisha magumu na ya shida pengine hata kuliko ambapo huyo Binti aliyefungwa angekuwepo uraiani.
Wadau huu ni mtazamo wangu tu na kama na Wewe una wako nakukaribisha sana nawe pia uweze Kutiririka na Kuserereka hapa na jisikie huru kunipinga kwa Hoja kwani hapa Great Thinkers tunaunganisha bongo zetu na kulifikiria hili nje ya box kabisa ili tuwekane sawa. Naomba leo katika uzi huu kusiwepo na matusi ya aina yoyote yale ila madongo ya hapa na pale Kwangu nayaruhusu ila siyo matusi. Nimetahadharisha mapema tu ili huko mbele ya safari tusije kulaumiana.
Nawapendeni nyote na karibuni pia.
Nawasilisha.
Mpaka sasa nawaza na akili yangu imegoma kabisa kuelewa baadhi ya matukio yanayohitaji mno tafakuri tunduizi ( critical thinking ) ya kilichotokea jana katika Nyumba moja ya Sheria na Utoaji wa hukumu nchini Tanzania maeneo ya Posta.
Hivi Mama wa Marehemu amepata faida gani labda kwa kufurahia Binti mdogo kwenda Lupango kwa miezi 24? Hivi Mama wa Marehemu kitendo cha kutoka pale Nyumba ya Sheria na Hukumu Posta huku akifurahi na moja kwa moja kwenda alipolala Mwanae Kinondoni kumsalimia kilikuwa kina maanisha nini?
Kama ni mashindano je Mama wa Marehemu alikuwa anashindana nini na Binti aliyehukumiwa miezi 24 Gerezani? Zile furaha pale Posta zilizokuwa zikisindikizwa na machozi zilitokana na nini hasa? Je baada ya ule ushindi wa Kisheria na Kihukumu wa jana Marehemu ameshafufuka na sasa amerudi Kwake Sinza?
Hivi hapakuwa na room ya mazungumzo yoyote ya Kidiplomasia baina ya pande mbili Kinzani / Hasimu zaidi ya Kukomoana na kuonyeshana nani ni Bingwa / Mshindi? Kwahiyo kumbe siku hizi Wakristo nchini Tanzania tunarudishiana ubaya kwa ubaya ( wenyewe mnasema kama noma na iwe noma ) kwa wale Maadui zetu.
Naomba kuuliza hivi laiti kama zile Mali za aliyelala sasa pale Mtaa wa Mkulima Kinondoni zingekuwepo hadi hivi leo na zinazalisha Mama Marehemu angepoteza muda na Kesi hiyo? Je hapa tukiamini kama labda ukazaji wa Vyuma ndiyo umejenga hasira kwa Mama hadi akaamua Kumkomo Binti wa Watu tutakuwa tumekosea?
Nimalizie tu kwa kusema kwamba huko nyuma nilikuwa nasikia tu kwamba Watanzania japo masikioni mwa wengi wanasifika kwa kuwa Wakarimu ila nilichokigundua na leo mtanisamehe sana ni kwamba hakuna Watu wenye roho mbaya, makatili and pure sadists kama Watanzania kubali kataeni.
Kama Mkristo wa kweli binafsi sikuona haja yoyote ya Mama Marehemu kulishikilia hili jambo bango hivi na badala yake ningesamehe tu na kumuachia kila kitu Mwenyezi Mungu na kuendelea na maisha yangu bila Marehemu nikijua / kuamini kwamba kila jambo hupangwa na Mwenyezi Mungu.
Huyu Mama anaweza kudhani kuwa amefanikiwa 100% ila kwa jicho kali la Kisaikolojia nasema wazi kabisa kwamba Mama Marehemu huenda sasa akawa katika data base yake ndiyo ameharakisha kuongeza idadi kubwa ya Maadui kuliko Marafiki na hali ambayo huenda pia ikampelekea akawa na maisha magumu na ya shida pengine hata kuliko ambapo huyo Binti aliyefungwa angekuwepo uraiani.
Wadau huu ni mtazamo wangu tu na kama na Wewe una wako nakukaribisha sana nawe pia uweze Kutiririka na Kuserereka hapa na jisikie huru kunipinga kwa Hoja kwani hapa Great Thinkers tunaunganisha bongo zetu na kulifikiria hili nje ya box kabisa ili tuwekane sawa. Naomba leo katika uzi huu kusiwepo na matusi ya aina yoyote yale ila madongo ya hapa na pale Kwangu nayaruhusu ila siyo matusi. Nimetahadharisha mapema tu ili huko mbele ya safari tusije kulaumiana.
Nawapendeni nyote na karibuni pia.
Nawasilisha.