Nahitaji Critical Thinking hapa tafadhali

Nahitaji Critical Thinking hapa tafadhali

Kuuwa ni kuuwa tu haijalishi umeuwaje!!! tabia mbaya ni tabia mbaya tu haijalishi unaifanya kwa mtindo upi!!! udogo wa miaka sio gigezo hata siku moja 18 is just a number!!! mtoto mdogo usiku wa manane unakwenda kwa watu kutafuta nini!!! Asiye funzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengo!!! usitetee ujinga hata kama aliyeufanya ni mtu wako wa karibu kiasi gani!!! ujinga ni ujinga tu..
 
Wewe unapwaya sana kwenye hili jukwaa siyo size yako.

Zipo kesi nyingi tu zinaondolewa mahakamani na zinaenda kumalizwa nje ya mahakama.

Na hata zile kesi ambazo Jamhuri ndio mshtaki DPP ana mamlaka ya kuzifuta kama Manji alivyofutiwa kesi ya uhujumu uchumi na DPP.

Wacha kuropoka kwa vitu usivyovijuwa, siyo lazima ugande jukwaa hili unaweza kwenda hata jukwaa la mapishi ukajifunze kupika.

Mkuu niachie huyo ' Bwege Nazi ' kwani tayari nimeshampa ' dozi ' yake muda si punde. Hata hivyo akhsante nawe kwa kuanza nae. Kuna mijitu humu mipuuzi sana halafu ukiikuta huko mitaani Kwao inatamba kabisa kama ni Intellectuals wakati kumbe ni Kinyume chake.
 
Wewe ndio ulileta uzi wa 'sniper' wa Lissu?
 
' Kamarada ' Matola hii ' Kitu ' nasikia kwa sasa haipo tena na imeshafutwa hivyo ukipigwa ' mvua ' ya miaka miwili ni miaka mwili hiyo hiyo. Tafuta Watu wa Magereza watusaidie katika hili ila nami nilidokezwa na Mdau mmoja hivi wa masuala haya haya ya Kisheria sasa sijui aliniambia kweli au alinilisha tu tango pori lililotukuka.
Class mate wangu mmoja ni mkuu wa gereza mojawapo hapa nchini nina taarifa sahihi na hata humu kuna uzi pia maofisa wa jeshi la Magereza wamelifafanuwa hilo mwaka huu.

Lulu atatumikia mwaka 1 na miezi 4 tu na hata pungufu ya hapo accordingly.
 
Nimejibu kwa akili uliyotumia wewe kuita greater thinker sasa hapo wewe ndio utaweka kama ni popoma au Ngumbaru........... maana hata wewe maelezo yako sio ya great ni ya kundi hilo hilo la ngumbaru na popoma ova

😀😀😀😀😀😀😀 naomba unitake radhi upesi kwa kuniita Ngumbaru ( Mjinga ) na Popoma ( Mpumbavu ) Duniani kote aliyevumbua maneno / misamiati mipya huwa hatakiwi kurudishiwa Yeye hayo hayo maneno / misamiati yake hivyo umenikosea sana. Omba radhi upesi Mkuu 😀😀😀😀😀😀😀
 
Mkuu awali ya yote nakusalimu na kwa kuwa umehitaji kuliangalia tukio kwa Jicho Pana ebu tusaidiane Jambo kwa Pamoja..
Kwenye Paragraph yako ya kwanza umeeleza kuwa kama sheria zinagekuwa zinaruhusu kumshitaki na kumtia hatia maiti basi marehemu angepigwa mvua ya miaka 30 kwa kufanya ngono na mtogo ambaye alikuwa chini ya miaka 18.. Ok Kulingana na Sheria ya kubaka Je ili mtu awe na akutwe na hatia ya kumuingilia Mwenzie bila ridhaa yake mlalamikaji anatakiwa awe nani? Jamhuri , mtendewa au? Kama nilisikia vizuri toka tukio zima linaanza na utetezi wa kadada ketu kazuri nikuwa kwa kipindi kile tukio linatokea kalikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa takribni miezi minne?? Je kabla ya kuwa na mahusiano na Marehemu haka kadada kalikuwa na Mahusiano na Wanaume wangapi? Je ni Mtanzania gani aliyewahi kumkemea na kumzuia huyu mtoto na mahusiano katika umri mdogo kisi kile? Wote ni mashahidi ni mara ngapi huyu bidada alikuwa akihudhuria kumbi za starehe na kuvaa nusu uchi mbele za watu wasomi na wabobezi wa Sheria za ustawi wa jamii lakini hakuna aliyekemea Jambo hilo hadi leo..?

Pia labda ufafanuzi hii kesi nani aliyeifukunyua au ilikuwa kesi kati ya Mtuhumiwa / Mfungwa na Mama wa marehemu au ilikuwa Kati ya Mtuhumiwa na Jamhuri? Nani alikuwa mtetezi kwa upande wa Jamhuri? ni Mama wa marehemu au wakili wa serikali? kuna mahala ambapo Mama wa marehemu kwa namna moja ama nyingine ameonekana akitoa maelezo ya kilichomtokea Marehemu..

I think we should stop kuongeza chumvi na kukuza lawama ambazo hata hazina miguu zaidi ya kujenga chuki baina ya watu hao....
Umeandika mengi sana, ila Chinese proverbs says a photo can speak thousands language. Jibu lako liko hapo.

Kanumba+na+Lulu.jpeg
kanumba_akiri_mu_buzima_hamwe_na_lulu.jpg
 
Class mate wangu mmoja ni mkuu wa gereza mojawapo hapa nchini nina taarifa sahihi na hata humu kuna uzi pia maofisa wa jeshi la Magereza wamelifafanuwa hilo mwaka huu.

Lulu atatumikia mwaka 1 na miezi 4 tu na hata pungufu ya hapo accordingly.

Afadhali Mkuu na akhsante kwa taarifa yako ambayo sasa naiamini kutokana na ninavyokuamini pia Wewe humu Jamvini. Kwahiyo Mbunye itarudi soon Mkuu ili Wadau waendelee kutiririka na kuserereka nayo kama kawaida? Ila kuna Washkaji zangu fulani hivi wa Kolokoloni moja ni ' Wabanduaji ' hatari sijui kama ' Mfungwa ' hatoichezea ' Mikuyenge ' yao huko aliko Kolokoloni Mkuu. Mwenyezi Mungu amsaidie na amlinde tu!
 
Niko upande wa Lulu.
Mahakama ya kichwa changu. Haijapata uthibitisho. Lulu anahusika vipi na kifo cha kanumba.
Angetumia zana yoyote. Mfano kisu, panga, nyundo n. K. Hapo ningesema sawa.
MAHAKAMA HAINA MAKOSA. hakuna wa kulaumiwa.
Ni sehemu ya maisha yetu.
OMBA YASIKUKUTE.

Ungeisoma hukumu yote Kwanza ungeelewa vizuri my sister
 
Class mate wangu mmoja ni mkuu wa gereza mojawapo hapa nchini nina taarifa sahihi na hata humu kuna uzi pia maofisa wa jeshi la Magereza wamelifafanuwa hilo mwaka huu.

Lulu atatumikia mwaka 1 na miezi 4 tu na hata pungufu ya hapo accordingly.
kumbe waliotoa ufafanuzi ni wakuu wa Magereza hahahahahaha aisee mi nilijua ni wajuzi wa Sheria inayosimamia Magereza
 
Soma mada inasemaje na wahusika wa kuchangia thread wanatakiwa watu wa aina gani?

Mkuu leo unawapa Watu ' dozi ' kali kali tu hadi nabaki kucheka na kupasuka mbavu zangu huku. Ama hakika leo wanaowashwawashwa watakukoma katika uzi huu. Leo umeifanya Kazi yangu kuwa rahisi na nimekuwa mapumzikoni sasa. Yaani unawapa tit for tat kitendo bila kuchelewa 😀😀😀😀😀😀😀
 
kumbe waliotoa ufafanuzi ni wakuu wa Magereza hahahahahaha aisee mi nilijua ni wajuzi wa Sheria inayosimamia Magereza
Wewe akili huna siwezi kupoteza muda wangu na wewe.

Kwa taarifa yako classmate wangu ana degree ya sheria ndio inayompandisha vyeo na siyo kupiga kwata.

Ukisikia askari unadhani hawana fani zao mpuuzi sana wewe.

Isitoshe hiyo system ya kutumikia kifungo 1/3 imewekwa na magereza wenyewe.
 
Niliposema Critical Thinking itumike hapa sikutaka huu ' upumbavu ' kama wako unaokusumbua badala yake nilitaka sasa Watu twende mbali zaidi na tufikirie kwa Kina kabisa na hasa nje ya box ili kuleta tafakuri pana yenye nadharia kubwa iliyojaa mantiki ambayo itaweza kusaidia hata kwa siku za baadae Watu kuwa makini na kutorudia Kosa. Kila siku huwa nawaambia ukiona GENTAMYCINE nimeanzisha uzi usiukurupukie Kwanza au ukadhani nimeandika tu ili mradi bali maandiko yangu mengi huwa yanamtaka Mtu aushirikishe vizuri Ubongo wake lakini kama Ubongo umejaa ' Kamasi ' na ' Kohozi ' kama ulionao huwezi kung'amua / kuelewa lolote.
Ndio maana nilikwambia unataka tutumie ajili gani kwa jambo ambalo liko wazi kama hili, kwa mtu anayejiita great thinkers kama wewe hii ni kamasi jumlisha na shahawa yaani ni ujinga uliopitiza
 
Ungewatafuta uwashauri wamalizane kindugu ungeonekana wa maana zaidi.

Saivi haisaidii ...sana waonekana mtafuta kiki tu kama wengine.
 
No critical thinking is needed here..

Sheria ni Msumeno.
 
Alichoniacha hoi huyo mama ati anaishukuru serikali ya awamu ya tano, haya ni mauzauza matupu hajui hata muhimili wa mahakama ni nini.

Huyu mama kwa mara ya kwanza nilimsikia amekuja kwenye msiba wa Kanumba Dar na mpaka leo amezamia Dar na hana hata mpango na mzazi mwenzanke Baba Kanumba na amejipa haki zote za urithi wa marehemu, huyu mama ni sehemu ya mashetani tunaoishi nao humu duniani wakiwa na maumbo ya binadamu.

Since day one, tulipopata taarifa za kifo cha Kanumba hapa JF mpaka leo msimamo wangu juu ya Kanumba haujawahi kuyumba wala kubadilika, kwangu Kanumba alikuwa ni mbakaji tu na wala si vinginevyo.

Mungu amuweke anapostahili.
Mama Kanumba yupo Dar zamani sana hata kabla ya Kanumba kuwa maarufu alienda kwenye msiba Bukoba wakati mwanae anafariki usipotoshe
 
Ndio maana nilikwambia unataka tutumie ajili gani kwa jambo ambalo liko wazi kama hili, kwa mtu anayejiita great thinkers kama wewe hii ni kamasi jumlisha na shahawa yaani ni ujinga uliopitiza

Shikamoo Mkuu hili ' dongo ' limeniingia hadi nabaki kucheka tu hapa sasa. Mkuu leo umenipatia haya bhana!
 
Ni kweli mama kanumba asingeweza kusema asamehewe ambacho angeweza kufanya ni kutotokea mahakamani yeye na mashahidi mwisho wa siku keai ingefutwa kwa kukosa mashahidi
Kwani mama Kanumba ni shahidi?una mtoto?kama unaye umeshafikiria utamfanya nini aliyemuua hata kama hakukusudia?
 
Ungewatafuta uwashauri wamalizane kindugu ungeonekana wa maana zaidi.

Saivi haisaidii ...sana waonekana mtafuta kiki tu kama wengine.

Watch out not that extent please!
 
Back
Top Bottom