1. Mara ya kwanza Kesi iliyosumbua sana, ya yule mmiliki wa mabasi maarufu ya J Four(J4) ya kuwaua wadeni wake kwa kuwapiga risasi, mpaka kuhukumiwa kufungwa maisha(kama sijasahau ilikuwa kunyongwa hadi kufa) ambayo kiuhalisia ni kweli jamaa aliwaua watu wale(alikiri kuhusika), Wakili huyu kwa kuwa anafahamu namna alivyo na mtandao mkubwa wa mahakimu akaingilia kesi ile na kesi kuanza upya, na kwa dalili zilizokuwepo ni kwamba yule jamaa(J4) alikuwa anaelekea kushinda kesi(sijui kama hukumu ilishatoka maana niliondoka Tz, nikaacha kufuatilia) hivyo roho za wale waliouawa zikawa zimedhulumiwa kwa kujuana na nguvu ya pesa.
2. Kesi ya mke wa marehemu Bilionea Msuya,
Baada ya mauaji ya dada wa marehemu bilionea Msuya, mama wa mtoto mmoja na aliyekuwa akifanya kazi Wizara ya Fedha, kuuawa kwa kuchinjwa kama kuku, Mke wa marehemu bilionea Msuya alikiri kuhusika na mauaji yale kwa kigezo kuwa marehemu(dada wa bilionea Msuya) alikuwa akimsumbua sana kwenye mirathi, hivyo akahukumiwa kifungo cha maisha kama sijasahau
Ni yule yule wakili kuingilia kesi hiyo ambayo awali mtuhumiwa alikiri kuhusika na mauaji hayo, baada ya muda na wakili huyo kuchezesha kama kawaida yake, February mwaka huu muuaji kaachiwa huru bila shaka yoyote kua hakuhusika
Ni kesi hii ndiyo inayoibua maswali na kejeli nyingi kwa mahakama zetu na vyombo vya ulinzi na usalama hasa jeshi la polisi upande wa upelelezi, na wengi kuona kua kesi ile haikumtendea haki marehemu dada wa bilionea Msuya ambayo kimsingi ni kweli
Sasa mimi nimekaa na kutafakari sana, kimwili na hasa kiroho, nikajiuliza huyu wakili mwenye koneksheni na majaji mbona ameifanya pesa, koneksheni na elimu yake kama fimbo ya kuwachapia wale wasiofika bei,
Roho za marehemu hao zinalia, familia za marehemu hao zinataabika, watoto wa marehemu hao wanateseka sababu ya kuuawa kwa wapendwa wao, ni nani atazifuta machozi familia hizi, Ee Mwenyezi Mungu ni nani atawafuta machozi watoto wa marehemu hao ambao wengine walikua wakisoma shule nzuri leo hii wanaenda kidumu na mfagio sababu ya kuuawa kwa wapendwa wao na mbaya zaidi ukweli kupindishwa na mhusika wa kupindisha ukweli ni huyu wakili, ninajua nayeye ana watoto ana ndugu na ipo siku hao waovu anaowatetea, roho za marehemu zitamrudia yeye na kizazi chake kwa kua anafanya hivyo si kwa sababu watu hao walionewa bali watu hao wamemlipa pesa ya kutosha ambayo anaweza kugawana na wenzake na kesi ikapindishwa , na kuwashuhudia uongo marehemu hao
Ukweli utabaki pale pale, dunia tunapita, vile unavyowatendea wenzako nawe siku moja utatendewa vivyo hivyo kama si wewe basi kizazi chako. Pesa haijawahi kutosha na haitotosha kamwe, unashuhudia vipi uongo ambao unajua kweli yake, kweli pesa mwanaharamu, Ee Mwenyezi Mungu nijaalie nipunguze tamaa hasa dhidi ya pesa, sijui huyo mtoto wa dada wa Bilionea Msuya atakua na umri gani lakini katika kufikiria kwangu hata akiwa mkubwa ataoneshwa watu wawili waliohusika na kifo cha mama yake, Muuaji(ambaye awali alikiri) na wakili aliyemsimamia na kumtetea kua hakuhusika ilihali anajua kuwa alihusika.
Najua hata watu hao wangefungwa isingewaongezea kitu familia zao lakini kitendo cha wao kufungwa kingeleta ahueni kwa wapendwa wao.
Sijui kwanini kesi ya huyu dada wa bilionea Msuya imeniumiza sana, nimeumia sana, japo nikiri kuwa mimi sikuwahi kuwafahamu watu hao ila nilikuwa interested tu kuona haki ikitendeka kwa kua wauaji walikiri,
Ndugu na rafiki yangu wakili najua unazipenda kesi hizi kwakua zinakupa pesa ndefu kwa wakati mmoja lakini kweli ya mauaji ya watu hao unazijua, ni kesi zenye nguvu za kiroho, naomba nikukumbushe "Karma is a bitch" kama si kwako hata kwa vizazi vyako.
Mungu azitie nguvu familia za marehemu. "Sisi ni wake na kwake tutarejea"
Amina
2. Kesi ya mke wa marehemu Bilionea Msuya,
Baada ya mauaji ya dada wa marehemu bilionea Msuya, mama wa mtoto mmoja na aliyekuwa akifanya kazi Wizara ya Fedha, kuuawa kwa kuchinjwa kama kuku, Mke wa marehemu bilionea Msuya alikiri kuhusika na mauaji yale kwa kigezo kuwa marehemu(dada wa bilionea Msuya) alikuwa akimsumbua sana kwenye mirathi, hivyo akahukumiwa kifungo cha maisha kama sijasahau
Ni yule yule wakili kuingilia kesi hiyo ambayo awali mtuhumiwa alikiri kuhusika na mauaji hayo, baada ya muda na wakili huyo kuchezesha kama kawaida yake, February mwaka huu muuaji kaachiwa huru bila shaka yoyote kua hakuhusika
Ni kesi hii ndiyo inayoibua maswali na kejeli nyingi kwa mahakama zetu na vyombo vya ulinzi na usalama hasa jeshi la polisi upande wa upelelezi, na wengi kuona kua kesi ile haikumtendea haki marehemu dada wa bilionea Msuya ambayo kimsingi ni kweli
Sasa mimi nimekaa na kutafakari sana, kimwili na hasa kiroho, nikajiuliza huyu wakili mwenye koneksheni na majaji mbona ameifanya pesa, koneksheni na elimu yake kama fimbo ya kuwachapia wale wasiofika bei,
Roho za marehemu hao zinalia, familia za marehemu hao zinataabika, watoto wa marehemu hao wanateseka sababu ya kuuawa kwa wapendwa wao, ni nani atazifuta machozi familia hizi, Ee Mwenyezi Mungu ni nani atawafuta machozi watoto wa marehemu hao ambao wengine walikua wakisoma shule nzuri leo hii wanaenda kidumu na mfagio sababu ya kuuawa kwa wapendwa wao na mbaya zaidi ukweli kupindishwa na mhusika wa kupindisha ukweli ni huyu wakili, ninajua nayeye ana watoto ana ndugu na ipo siku hao waovu anaowatetea, roho za marehemu zitamrudia yeye na kizazi chake kwa kua anafanya hivyo si kwa sababu watu hao walionewa bali watu hao wamemlipa pesa ya kutosha ambayo anaweza kugawana na wenzake na kesi ikapindishwa , na kuwashuhudia uongo marehemu hao
Ukweli utabaki pale pale, dunia tunapita, vile unavyowatendea wenzako nawe siku moja utatendewa vivyo hivyo kama si wewe basi kizazi chako. Pesa haijawahi kutosha na haitotosha kamwe, unashuhudia vipi uongo ambao unajua kweli yake, kweli pesa mwanaharamu, Ee Mwenyezi Mungu nijaalie nipunguze tamaa hasa dhidi ya pesa, sijui huyo mtoto wa dada wa Bilionea Msuya atakua na umri gani lakini katika kufikiria kwangu hata akiwa mkubwa ataoneshwa watu wawili waliohusika na kifo cha mama yake, Muuaji(ambaye awali alikiri) na wakili aliyemsimamia na kumtetea kua hakuhusika ilihali anajua kuwa alihusika.
Najua hata watu hao wangefungwa isingewaongezea kitu familia zao lakini kitendo cha wao kufungwa kingeleta ahueni kwa wapendwa wao.
Sijui kwanini kesi ya huyu dada wa bilionea Msuya imeniumiza sana, nimeumia sana, japo nikiri kuwa mimi sikuwahi kuwafahamu watu hao ila nilikuwa interested tu kuona haki ikitendeka kwa kua wauaji walikiri,
Ndugu na rafiki yangu wakili najua unazipenda kesi hizi kwakua zinakupa pesa ndefu kwa wakati mmoja lakini kweli ya mauaji ya watu hao unazijua, ni kesi zenye nguvu za kiroho, naomba nikukumbushe "Karma is a bitch" kama si kwako hata kwa vizazi vyako.
Mungu azitie nguvu familia za marehemu. "Sisi ni wake na kwake tutarejea"
Amina