Nahisi simpendi mke wangu

Asante dada kwa her
 

we mtu bwana.....nani kakwambia huyo jamaa amefunga ndoa kanisani? hivi umeisoma vizuri posti yake au unaendeshwa na matukio tu hapa.....?
Ndoa hakuna pale....wanaishi bila kufunga ndoa kwa miaka kumi sasa....kwa hiyo mungu haitambui ndoa yao....wamezini kwa miaka kumi mfululizo hadi kupata w atoto watatu sasa....nadhani tuanzie hapo....
kwahiyo ushauri wangu kwake nimeuelekeza vilevile kama wanavyoishi(kishetanishetani)....hopeful umenielewa sasa
 
Mh pole sana kaka kwa yanayokukuta, mwanamke amepata mwanaume mzuri ila yeye ni majanga mh i wish it was me kweli kila mtu na bahati yake
 
Mwache sasa, vituko vyote hivyo bado haujasanuka
 
Lati hujajaaliwa kalio? Naona unaongea kwa uchungu sana!! Usijali wapo wengi tu wasioangalia kalio.
 
Kijana kwanza pole sana,... Wengi wameshauri vizuri kila mmoja kwa jinsi alivyoweza kuyapima maelezo yako. Ni wewe tu na akili yako ufuate lipi uache lipi. Kumbuka mali hutafutwa ila si roho ya binadamu. Jiulize ivi maana ya ndoa ni ipi? Je ni kubembelezana au ni maelewano? pia tafuta jibu la kwa nini wewe pekee ndio unaonekana kuitafuta amani wkt mwenzako anaongeza chuki? na je kwa nini hataki kujulikana kanisani na wewe hukutilia maanani hadi hali imeendelea kuwa mbaya kiasi hiki? anyway wazungu wanasema keep yourself together or you will loose everything. Muulize anataka nini mpe nafasi aongee hadi amalize then utaamua mwenyewe kupata jibu litakalokufanya uwe na maamuzi yatakayokupa amani ya moyo wako. However ikitokea amekataa kubadilika kabisa yaani abaki kama alivyo..... huyu dada atapata malipo yake hapahapa duniani.
 
Kazi ipo. Atakuua. kama si kwa sumu au ushirikina, basi kwa shinikizo. Fanya maamuzi ndugu. Sio wewe humpendi. yeye ndio hakupendi
 
Pole sana.Kweli kwenye miti hapana wajenzi.Anaona unampenda ndo maana anakunyanyasa.
 
mmhh sijui ni tatizo la elimu, ignorance au ushirikina!? Aisee kaka pole kwa unayopitia, ongezea na maombi.
 

Spade4spade . Nimesoma huu uzi mara nyingi na kupitia maoni ya watu wengi but speaking from experience nachelea kuamini hii stori kwa asilimia mia. There is a lot that was going on hatujaaelezwa. In short I don't buy it. Nina mkasa wa mwanaume mkorofi, mwenye roho ngumu na asiyejali hisia za mkewe na yeye ndiye haswa chanzo cha shida kwenye nyumba. Lakini huzunguka na stori kama hii sasa nashindwa kuelewa huruma za wananchi juu yake sijui huwa zinamsaidiaje wakati deep down his heart anajua ye ndiye chanzo cha mkewe kutomwamini and all other stuffs.
 
Uko sahihi kabisa. Hapa kuna vitu vingi hatuvijui ila tunakimbilia kusema huyu mwanamke ni this n that. Ogopa sana mwanaume anaekupa stori kujionyesha kuwa ye ni victim wa matukio mabaya ya mkewe au girlfriend. Mtu wa namna hii mara nyingi ni mbaya na guilty consciousness yake kwa anayoyafanya humfanya kujivictimize ili aonekane ye ni mwema. Hivi unaweza ukawa na matatizo ya uhusiano tangu mnaanza kuishi pamoja then hamfungi ndoa, then mnapata two more kids bila ndoa. Na mnaishi tu, na haya matatizo mmejaribu vipi kuyatatua as in third part imehusishwa?(wazazi mmewahusisha matatizo yenu na walifanya nini?)Ulisema ulimrudisha kwao kwasababu gani? Je , hana hata kaka zake au babake ? Nashindwa kuamini sababu ipo familia yenye tatizo kama lako lakini mlalamikaji ndiye hasa tatizo.
 

Wala usihangaike na nyani kutoona nyuma ya kwake akaanza kucheka za wenzake eti zinatoa damu. Nilikuwa na mpango wa kuichambua habari yake lkn kuna mjanja akaniita mi kiaz nikaona nitabishana na hamnazo. Kila neno la huyu mleta thread amejipendelea. Ni rahisi kiasi cha kutohitaji mpelelezi au wakili kumshushua lkn nimekula pozi. Ni bahati mbaya kuwa wengi wa wana jf ni mashabiki wa kila jambo na hawataki ukweli. Ngoja kwanza nakula pozi nikiwa nimeuchambua ujumbe wake usio na chembe ya ukweli. Nitakuja km itabidi.
 
I have a feeling the jamvi is being taken for a ride. This story is too biased to be true. Hivi huyu jamaa yeye ni malaika?! Mleta stori kajipange uje tena, vinginevyo hii ni tungo kama nyingine tu.
 
Ninajua kutunza mwanamke, ukikutana nae kama hajabeba watoto utasema ni binti hajazaa. Watu huwa hata hawaamini kama hao watoto kawazaa yeye, angekuwa amechoka angekuwa mtulivu sana.

Samahani mleta mada ila statement kama hii hapa ndio zinanifanya nizidi kutokukuamini kwa asilimia mia. Unisamehe kwa hili.
 

Pole mkuu kwa changamoto mnazo zipata, ila nahisi utofauti wa elimu( mkeo ana inferiority complex) unaweza ukawa una changia. Jaribu kuongea nae, ikishindikana, kaongee na wazazi wake, pengine anaweza akaelewa somo
 
Maisha ni mafupi na hatuishi mara mbili. Mimi nadhani furaha yako ni muhimu kuliko kusema jamii itakuelewa vipi. Hakuna mapenzi tena kati yenu, na huwezi kulazimisha yarudi.
La msingi ninaloliona ni wawili nyie kuachana. Hakuna zaidi ya hapa ikiwa hata uwepo wako ndani ya nyumba hautambuliwi.
Kigezo cha kuishi kwa mateso sababu ya watoto kimepitwa na wakati, unachohitaji ni faraja ya moyo wako na si vinginevyo. Kama hii huwezi kuipata kwa mkeo, huna sababu ya kua nae.
Nakutakia kila la kheri, ufanye maamuzi ya busara.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 

Ana pelekeshwa kwa sababu ka mdondokea ki mapwenzi
 
Kaushauri kidogo tu. Talaka si dawa, pia kumwona mkeo kuwa ndo mbaya si vyema. Jiulize, umewapataje hao watoto wako 3?? Je, ulikuwa unamwekea kwa mrija au ni kukutana naye kimwili?? Lazima kuna kamapenzi flan hivi kati yenu.
Huenda huyu mama amekupenda mno kiasi kwamba anatafuta mbinu ya kukaa na weye kila saa. Hujatuambia kama unapokuja week ends huwa una nafasi zaidi na mkeo au ni kama mtu aliyekuwepo hapo nyumbani. Mkeo kukutuhumu kuwa una wanawake (Wake wengine) mpaka anakuona utamletea ukimwi. Ni mashitaka mabaya mno, huenda ukija hujui mwenzio amekungoja kwa hamu kuu. Unaingia na kuzama ghafla hujui katosheka unaanza mipango ya safari kesho kurudi kazini.
Mke si jengo la nyumba, ni zaidi ya hicho. Mke si kumzalisha watoto, ni zaidi ya hilo, mke ni wewe kupata nafasi na yeye. Kabla hujawaza kuachana, hebu tafuta njia ya kupata nafasi nzuri na yeye, umshibishe ukimwondoa genye zake. Mwanamke (Naomba msamaha kwa nitakaye mwudhi hapa) akiwa na hamu ya mumewe ni hatari. Anaweza kutumia chochote kilicho mbele yake na hataki kuguswa guswa bila mtu kumtoa hamu. Fikiri kwanza kabla hujachukua hatua.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…