The Assassin
JF-Expert Member
- Oct 30, 2018
- 4,355
- 17,321
Kwa hali niliyonayo nahisi hii ni covid 19 3rd wave Delta.
Kwa muda wa wiki nzima hii inayoisha kesho nimekua naumwa ugonjwa usiojulikana. Nimeenda hospitali zaidi ya 2 bado sionyeshi ugonjwa wowote.
Kuanzia jumamosi iliyopita nilikua naumwa kichwa kisicho cha kawaida, nikapewa dawa za kutuliza maumivu lakini wapi, jumatano nikaenda hospitali nyingine nikabadilishiwa dawa kichwa kimeacha kuuma ila mwili hauna nguvu, nimekua mnyonge na dhaifu sana.
Sina ladha ya chakula na wala sitaki kula, nataka muda wote niwe nimelala hadi mbavu zinauma, sihisi harufu yoyote lakini pia nimeanza kuhara mara moja moja na kukohoa kifua kinawasha washa.
Naomba kufahamu hapa Dar ni wapi naweza kwenda kupima covid. Ingawa nimeanza kuona improvement lakini natamani nipime niwe na uhakika.
Ahsante.
Kwa muda wa wiki nzima hii inayoisha kesho nimekua naumwa ugonjwa usiojulikana. Nimeenda hospitali zaidi ya 2 bado sionyeshi ugonjwa wowote.
Kuanzia jumamosi iliyopita nilikua naumwa kichwa kisicho cha kawaida, nikapewa dawa za kutuliza maumivu lakini wapi, jumatano nikaenda hospitali nyingine nikabadilishiwa dawa kichwa kimeacha kuuma ila mwili hauna nguvu, nimekua mnyonge na dhaifu sana.
Sina ladha ya chakula na wala sitaki kula, nataka muda wote niwe nimelala hadi mbavu zinauma, sihisi harufu yoyote lakini pia nimeanza kuhara mara moja moja na kukohoa kifua kinawasha washa.
Naomba kufahamu hapa Dar ni wapi naweza kwenda kupima covid. Ingawa nimeanza kuona improvement lakini natamani nipime niwe na uhakika.
Ahsante.