Mimi ni mdada mwajiriwa wa serikali.Nilitokea kuwa na mahisiano na mwanaume mmoja ambae hajaajiriwa na yupo chuo kikuu flani cha afya jijini Mwanza,alinitambulisha kwa baadhi ya ndugu zake akiwepo baba na shangazi yake pamoja na baadhi ya marafiki zake.Nilikuwa tayari kwa chochote licha ya dini zetu kuwa tofauti nilikuwa tayari kubadili hata Kama wazazi wangu pamoja ndugu zangu wangenipinga.Wazazi wake wametengana hawaishi pamoja.Na hili jambo ndugu wa baba walikubali lakini ndugu wa mama walipinga hivyo yule kijana akaamua kusitisha Mipango yote na Mimi,Pia ndani ya mwezi mmoja alitangaza ndoa na mwanamke mwingine.Niliumia Sana na kwa jinsi ambavyo nilijitoa kwaajili yake na ndugu zake wengine ni Mungu pekee ndiye anaejua.Ndoa yao imeshapita.Naamini Mungu ni mkubwa siku moja na Mimi atanipatia wanguambae atanipenda kwa dhati na hatimae kuwa mke halali na nikasahau machungu yote ninayopitia.