Nahisi kama nimefikia hatua ya Kukata Tamaa kiwango cha Mwisho. Naomba msaada wenu Ndugu zanguni

Status
Not open for further replies.
Mkuu mimi niliwahi kupoteza kazi katika mazingira kama hayo mbaya zaidi ndio ilikuwa kipindi namchumbia mke wangu.Nakuelewa unachomaanisha Sasa naomba nikuunganishe na jamaa zangu Fulani hope watakusaidia ila naomba tusifahamiane na hata ukifanikiwa usinitafute tujuane pili nitumie namba yako ya mpesa au tigo pesa inbox Mimi nitafanya muamala kea wakala tu pole sana mkuu // Soma kitabu cha ayubu ukumbuke mapito aliyopitia na jinsi Mungu alivyomuinua Tena baadae.

Superbug.
Mungu akubariki na kukuongezea ulipotoa na akumbuke msaada unaoutoa
 
Labda Limbwata uliloomba ndo limesababisha yote ayo
Screenshot_2020-12-04-11-00-48.jpg
 
Kwanza uyo mke hakuwahi kua na upendo wa dhati kwako hata siku moja ...

kama wewe ni christian nitafute nikuelekeze sehem ambayo utaombewa huo mguu na ukapona kabisa huo ndio msaada wangu ....na nna uhakika na kupona kwako...wala haiitaji pesa ni bure yaan ni wewe na muda wako tu na trust me utapona kabisa.....sababu hata mama mkwe wangu alikua na tatizo kama lako alikua hawezi hata kuchuchumaa alishatumia dawa nyingi bila mafanikio lakin saiv mzima kabisa...miaka 30+ ni mdogo sana bado unahitajika kulijenga taifa hili....

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni dar?
 
Maisha ni fumbo kubwa sana.huyu ni msomi aliekuwa na sifa za kuitwa boss,mmiliki wa magari na assets za kila namna.Lakini leo amerudi kuwa dhalili ,sembuse mimi!.Kuna chakujifunza hapa.

Sent from my HUAWEI CUN-L01 using JamiiForums mobile app
 
Pole sana mkuu, usikate tamaa. Pambana mpaka dakika ya mwisho ambayo mungu atauchukua uhai wako.
Usiache kuomba/kufanya dua kwa imani yako mkuu. Nimeguswa na natamani kukusaidia ila sina uwezo.
 
Lakini mkuu kwenye Uzi wako hujasema au kutaja mapungufu yako ambayo binafsi naamini unayo kama binadamu ambayo yanaweza kuwa kwa kiasi fulani yamechangia either kushuka kiuchumi au kumkwaza mkeo naona umeongea mazuri tuu na mabaya ya mkeo wewe hujasema.

Yawezekana tukimuita mkeo aje akuseme hapa tunaweza kukimbiana na wengine wakadharau unachojiekeza !

Hujawahi kubugi hadi wife akamind ??

Hujawahi haribu home au kiuchumi ikasababisha ujilaumu ?

Unadhani ni upepo tu mbaya ndo umekufanya uko hivo au na wewe umechangia ??

Sorry hii ni mara ya pili kuchangia
 
Nilikuwa nauona huu uzi najikuta sitaki kusoma ..
Daah, huu mtihani mkubwa chief.

Tuseme ukweli awamu hii ya tano watu wengi wanapitia changamoto kama zako hasa watu waliokuwa sekta binafsi.

Sina hata cha kukushauri ... Uza gari kaezeke vyumba viwili au vitatu, choma grill na kuweka wavu wa mbu dirishani kisha hamia kwako hivyo hivyo.

Utalima hata mchicha huku ukitafuta njia ya kurudi kwenye mstari.
 
Kwa kweli Kupanga ni kuchagua.. na Akili ni nywele kila mtu ana zake..

Hivi unaanzaje kununua Gari moja la kutembelea kabla hujajenga? Unaona tena halikutoshi, Unanunua tena gari la pili kabla hujajenga, unaona magari mawili hayakutoshi unaamua tena kununua gari la 3 la kutembelea kabla ya kujenga kweli??? Labda kama kweli ni lile limbwata uliloomba mkeo akufamyie katika uzi wako 2016.
 
Mmhh,.maneno yamenikosa mimi😞😞ila kuna wanawake Mungu anawaona aki vilee,ina maana kile kiapo cha kwa shida na raha hakukielewa vizuri au?? useless woman,😏
 
Sodoku kwenye hii thread yako kuna quotation marks "" je ni wewe au umecopy na kupaste.

Na hiyo kampuni unayoisema naijua.

Ni PC iko mtaa wa Libya.
Sidhani kama watakuwa walifikia hali mbaya hivyo wakati 2019 walikuwa wanataka kuajiri mwalimu wa uchumi kwa level ya certificate na diploma.

Hiyo kampuni ni inakua.

Tafadhali kama hii umecopy mahala na kuiweka hapa ili uchangamshe jukwaa ni vyema ukafuta na kuomba msamaha.

Umeumiza wengi na kama ni kweli pia pole tunaweza wasiliana pm.


So far mtu ninayemfahamu hapo nayeye hayupo kwa kampuni.

Na kwa muonekano ile kampuni pamoja na kutengeneza tender za serikalini lakini pia ilipata tenders kubwa za petrol stations hapa bongo na ina chuo kinachokua.
Sidhani kama kwa kampuni iliyopitia hayo miaka 3 ningeweza kuikuta kwenye hali ile.

Nakataa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom