kikoozi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2015
- 2,030
- 2,929
Habarini za siku, mimi ni kijana wa miaka 38 nadhani uko nyuma nilileta uzi wangu mnishauri maana baba alinifukuza kwake nilipokuwa nakaa kisa tu nilimshawishi awe na kadi ya Chama Cha Mapinduzi ambacho mimi ni mwananchama wake mtiifu aligoma na kunifukuza kwake.
Nilichoshangaa baba baada ya kunifukuza na kutafuta mtu wa kukaa mlangoni (mlinzi) kama ili kuzuia yeyote mgeni kuingia ndani bila ruksa nikiwepo mimi, jana jioni nasikia baba ameitisha kikao cha ndugu zangu wengine pasipo kuniita na mimi kwenye kikao kile.
Nasikia baba amegawa mali zake kwa wadogo zangu, naumiaa sana ndugu zangu wana jamiiforum nisaidieni, nahisi kufa naombeni mnishauri njia nzuri ya kwenda kumfungulia jarada mahakamani, mimi ni mtoto wake kabisa, kwanini hanishirikishi kwenye hizo mali, wakati mimi ni mkubwa nina uchungu na hasira sana, naombeni mawazo yenu wakuu.
Kwa sasa nipo kwa rafiki yangu nakaa kwao, sina pa kuanzia wakuu maana pale nilikuwa nimepanga kodi iliisha na kazi sina kabisa, rafiki yangu ameniambia nipigane juu chini nipate na mimi sehemu ya mali ili niweze kuanzisha maisha yangu.
Wataalamu wa sheria, na haki za vijana na urithi nisaidieni, mtoto wenu nataka kuzurumiwa na baba yangu kweupe kabisa
Nilichoshangaa baba baada ya kunifukuza na kutafuta mtu wa kukaa mlangoni (mlinzi) kama ili kuzuia yeyote mgeni kuingia ndani bila ruksa nikiwepo mimi, jana jioni nasikia baba ameitisha kikao cha ndugu zangu wengine pasipo kuniita na mimi kwenye kikao kile.
Nasikia baba amegawa mali zake kwa wadogo zangu, naumiaa sana ndugu zangu wana jamiiforum nisaidieni, nahisi kufa naombeni mnishauri njia nzuri ya kwenda kumfungulia jarada mahakamani, mimi ni mtoto wake kabisa, kwanini hanishirikishi kwenye hizo mali, wakati mimi ni mkubwa nina uchungu na hasira sana, naombeni mawazo yenu wakuu.
Kwa sasa nipo kwa rafiki yangu nakaa kwao, sina pa kuanzia wakuu maana pale nilikuwa nimepanga kodi iliisha na kazi sina kabisa, rafiki yangu ameniambia nipigane juu chini nipate na mimi sehemu ya mali ili niweze kuanzisha maisha yangu.
Wataalamu wa sheria, na haki za vijana na urithi nisaidieni, mtoto wenu nataka kuzurumiwa na baba yangu kweupe kabisa