Tatizo si "mtu",tatizo ni mfumo,na hapa tatizo ni "uccm","uwenzetu" na "ukada".
JPM kama mtu anaweza akawa msimamizi na mtendaji mzuri sana sana,lakini kama ataendekeza ukada,uccm na uwenzetu,hapo anaweza kushindwa.
Embu jiulize,mtoto wa mwenyekiti wa ccm na mbunge mmoja wana kampuni ya catering ambayo wanapata tenda zote za sherehe za kiserikali,ukifuta chakula katika sherehe za kiserikali,huyo mtoto,mbunge na familia ya huyo mtoto watafurahi?Si ndio wataanza kufanya "sabotage" kwa serikali?Mh. mbunge ana travel agency ambayo wateja wake wakubwa ni viongozi wazurulaji huko nje,atafurahia kukatwa kwa safari za nje?
Mke wa x pm ana tenda ya kusupply refreshments kwenye wizara na idara za serikali ambapo yai moja hulipiwa elfu 2,leo JPM akifuta hiyo bajeti unategemea hawa watu wamwangalie tu?
Swali la msingi ni je,yupo tayari kutumbua majipu yaliyopo mwilini mwake halafu akakubaliana na machungu?