Nadhani mnaanza kumuelewa Jingalao!

Nadhani mnaanza kumuelewa Jingalao!

Sijamshabikia Magufuli kwa bahati mbaya.
Nilimshabikia kwa imani kubwa juu yake.

Nilimshabikia kwa kuwa nilijua ni mteule na ni mteule wa kweli mwenye kusimamama katika kweli.

Nilimshabikia kama mzalendo Mtanzania bila kulipwa chochote na asiyetegemea kulipwa chochote.

Nilimshabikia kwa kuwa yuko genuine!

Nilimshabikia SANA ili nchi yetuisitumbukie kwenye mikono ya mafisadi.

Kamwe sitajutia kumshabikia Magufuli kwa kuwa watanzania wa hali ya chini kama mimi watafaidika.

Nilikubali kejeli na matusi yote ili tu watanzania wapate kilicho bora.

Niliuvaa ujinga ili tu watoto na vijana wetu wanielewe.

Niliuvaa utoto na ujana kwa maslahi ya mama Tanzania!

Watanzania watakuwa wananielewa sasa kile nilichokishabikia kwa ukweli au propaganda ni kipi hasa.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

we unashabikia ccm wala si Magufuli
 
Hata jk alikuwa na hotuba nzuri zaidi ya hii. ,lakini vitendo Zero

Unaweza kuiweka hapa tuione uzuri wake au tuelezee tu kwa kifupi alikuwa na vipaumbele gani maana ni miaka 10 imepita tangu alipohutubia Nina doubt hata kama unaikumbuka ila ni chuki tu zimekujaa
 
......hotuba ilikuwa nzuri lakini alipofika kwenye katiba mpya alituboa hadi watu waliokuwa wamasikiliza wakaanza kuponda...
 
Unatia aibu mama!!ni 3million and not 3billions,hivi kwa nini hua mnakurupuka na mambo ya uongo?

wewe ndo muongo.milion tatu?? hata maintanance ya photocopy machine inazd m 3
 
wewe ndo muongo.milion tatu?? hata maintanance ya photocopy machine inazd m 3

Wewe nae nitolee upuuzi wako hapa!kwanini usisome comment zote ukaelewa nilichokua namaanisha?!
 
Ukawa ni mashetani, wao wanasubiri wakosee ccm, yaani hawaitakii mema nchi yetu, nawachukia sana
Mudawote, huwatendei haki wapinzani. Madudu mengi ndani ya serikali yanaibuliwa na wapinzani. Au hujui kazi ya upinzani? Usiwachukie!!!
 
Last edited by a moderator:
Hebu acheni mihemuko nyie watu.

Mtu hata mwezi hajamaliza lakini nyie mnahemuka tu.

Msiwe watu wa kuongozwa na hisia hovyo hovyo tu.

Tumieni akili zenu [kama hata mnazo].

Kazi ndio imeshaanza wewe unasubiri nini tena?

Kamata ilani ya ccm na ahadi zake anza kuzifuatilia...utaendelea kutoamini lakini ndio hivyo tena kaskazi ameshavuma huyo!

Mihemko mlikuwa nayo ninyi mliokuwa mnazungusha mikono ..eti mabadilikooo...
 
......hotuba ilikuwa nzuri lakini alipofika kwenye katiba mpya alituboa hadi watu waliokuwa wamasikiliza wakaanza kuponda...

Amekuboa kwa sababu ulitegemea awe mnafiki kwa kuumauma maneno.

Yeye amesema ni muumini wa serikali mbili na atamalizia kiporo cha katiba pendekezwa.

Ameheshimu maoni ya wananch,tume ya warioba na michango na michanyato ya wabunge wa bunge la katiba na ataendelea na mchakato huo kulingana na matakwa na kanuni zilizopo.

Isitoshe hakuahidi kitu juu ya katiba wakati wa kampeni na watanzania walimchagua ikimaanisha tatizo la msingi ls watanzania sio katiba mpya(aliwahi kusema kinana) bali tatizo la msingi ni utekelezaji na usimamizi wa yale yaliomo kwenye katiba.

Hao waliojipachika jina la Umoja wa katiba ya wananchi ni wanafiki wakubwa baada ya kujigeuza kuwa kigenge cha wanasiasa matapeli,vilaza,mafisadi na mahawara zao wakishirikiana na wageni ili kuingia kwenye sekta za umma na kuanza kushibisha matumbo yao.

"KWA MTANZANIA MUAMINIFU,KWA IMANI YAKE HATAKUWA NA KIGUGUMIZI KATIKA KUWA MSTARI WA MBELE KUPAMBANA NA UFISADI"...JPJM-2015

Ukawa imeingia kwikwi katika kusimama na kupambana na ufisadi na sasa imegeuka kuwa mke mwenye visa ili apigwe majirani wasikie.
 
Taratibu za manunuzi zifuatwe!!


Pamoja na yote, aliyoyasema ni kilio chetu na ndo chanzo cha opposition parties hapa kwetu. Aliongea kama mwana Ukawa zaidi ya mwana CCM, na ili afanikiwe anahitaji supportb yetu kubwa NA YEYE ANALIJUA HILO KWAMBA HAPASWI KUONGOZA NCHI KWA ITIKADI YA CHAMA CHAKE.

Anaelewa kabisa kwamba hakuchaguliwa na wananchi (wananchi hawakitaki CCM), na hivyo basi vita ya RUSHWA ni mtihani wake mgumu wa kwanza ......... ataweza kukata kuyatumbua majipu bila ganzi kama alivyoahidi? THUBUTU?
 
Tatizo si "mtu",tatizo ni mfumo,na hapa tatizo ni "uccm","uwenzetu" na "ukada".
JPM kama mtu anaweza akawa msimamizi na mtendaji mzuri sana sana,lakini kama ataendekeza ukada,uccm na uwenzetu,hapo anaweza kushindwa.
Embu jiulize,mtoto wa mwenyekiti wa ccm na mbunge mmoja wana kampuni ya catering ambayo wanapata tenda zote za sherehe za kiserikali,ukifuta chakula katika sherehe za kiserikali,huyo mtoto,mbunge na familia ya huyo mtoto watafurahi?Si ndio wataanza kufanya "sabotage" kwa serikali?Mh. mbunge ana travel agency ambayo wateja wake wakubwa ni viongozi wazurulaji huko nje,atafurahia kukatwa kwa safari za nje?
Mke wa x pm ana tenda ya kusupply refreshments kwenye wizara na idara za serikali ambapo yai moja hulipiwa elfu 2,leo JPM akifuta hiyo bajeti unategemea hawa watu wamwangalie tu?
Swali la msingi ni je,yupo tayari kutumbua majipu yaliyopo mwilini mwake halafu akakubaliana na machungu?
 
Taratibu za manunuzi zifuatwe!!

Ununuzi wa hiki kivuko taratibu zilifuatwa?Unajua kwa nini amesema sheria ya manunuzi ipitiwe upya?Mnyika aliipigia kelele wana ccm mkamuona hana hoja,leo JPM amesema mnashangilia.
 
Tatizo si "mtu",tatizo ni mfumo,na hapa tatizo ni "uccm","uwenzetu" na "ukada".
JPM kama mtu anaweza akawa msimamizi na mtendaji mzuri sana sana,lakini kama ataendekeza ukada,uccm na uwenzetu,hapo anaweza kushindwa.
Embu jiulize,mtoto wa mwenyekiti wa ccm na mbunge mmoja wana kampuni ya catering ambayo wanapata tenda zote za sherehe za kiserikali,ukifuta chakula katika sherehe za kiserikali,huyo mtoto,mbunge na familia ya huyo mtoto watafurahi?Si ndio wataanza kufanya "sabotage" kwa serikali?Mh. mbunge ana travel agency ambayo wateja wake wakubwa ni viongozi wazurulaji huko nje,atafurahia kukatwa kwa safari za nje?
Mke wa x pm ana tenda ya kusupply refreshments kwenye wizara na idara za serikali ambapo yai moja hulipiwa elfu 2,leo JPM akifuta hiyo bajeti unategemea hawa watu wamwangalie tu?
Swali la msingi ni je,yupo tayari kutumbua majipu yaliyopo mwilini mwake halafu akakubaliana na machungu?

acha uongo kwa katiba iliyopo ndio ina mpa madaraka raisi yoyote kutengeneza mfumo imara au dhaifu maana mamlaka yote anayo raisi
 
Mudawote, huwatendei haki wapinzani. Madudu mengi ndani ya serikali yanaibuliwa na wapinzani. Au hujui kazi ya upinzani? Usiwachukie!!!
Unajua Eli79 wapinzani wanachukiwa sana kwa sasa kwa sababu ya unafiki wao juu ya lowasa. Hiyo kitu itawagharimu sana. Na kibaya zaidi uanaharakati kwa sasa ndiyo utawamaliza zaidi. Chuki yangu kubwa ni jinsi wanavyomdharau Dr Magufuli. Maana mpaka sasa wao wanaonesha dharau tu. Maana ktk tz ya sasa hakuna rais afaaye kama Dr Magufuli, ila wao wanabeza kila kitu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom