Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
Baraza la Taifa na Elimu ya ufundi (NACTE), sasa limebadilishwa jina na litajulikana kama Baraza la Taifa la Elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (NACTVET), mabadiliko hayo yamefanywa kufuatia Bunge kufanya mabadiliko mbalimbali ya Sheria ikiwemo Sheria namba 4 ya 2021.
Mabadiliko hayo madogo yameliongezea Baraza jukumu la urekebu na udhibiti wa mafunzo ya ufundi stadi ambayo awali yalikuwa yakifanyika chini ya mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya ufundi stadi (VETA)
Shabaha ya marekebisho haya ni kuongeza ufanisi katika usimamizi, urekebu na udhibiti wa ubora wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi yanayotolewa hapa nchini.
Kufuatia marekebisho ya sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte), jina la baraza hilo kwa sasa limebadilishwa na kuwa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NactVet).
Mabadiliko hayo ya sheria yameliongezea baraza hilo jukumu la urekebu na uthibiti ubora wa mafunzo ya ufundi stadi ambayo hapo awali yalikuwa yakifanyika chini ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta).
Taarifa iliyotolewa leo Februari 22 na Katibu Mtendaji wa NactVet Dk Adolf Rutayuga inaeleza kuwa mabadiliko hayo yanalenga kuongeza ufanisi.
Amesema shabaha ya marekebisho hayo ni kuongeza ufanisi, urekebu na uthibiti ubora wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi yanayotolewa nchini.
“Kwa mabadiliko haya ya sheria jukumu la urekebu na udhibiti ubora wa mafunzo ya ufundi stadi yamehamishiwa rasmi kutoka Veta hadi NactVet,” alisema Dk Rutayuga
Kufuatia hilo alisema maombi ya usajili wa vyuo, vituo na mafunzo ya ufundi stadi yanatakiwa kuwasilishwa NactVet ambako majukumu yamehamishiwa.
Katika hatua nyingine baraza hilo limetoa wito kwa vyuo na vituo vyote vilivyosajiliwa kutoa mafunzo ya ufundi stadi kuendelea kuendesha mafunzo hayo kwa mujibu wa sheria.
“Baraza litaendelea kushirikiana na wadau ikiwa ni pamoja na vyuo katika kuendeleza na kukuza utoaji wa elinh bora kwa ajili ya maendeleo ya taifa,”.
Mabadiliko hayo madogo yameliongezea Baraza jukumu la urekebu na udhibiti wa mafunzo ya ufundi stadi ambayo awali yalikuwa yakifanyika chini ya mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya ufundi stadi (VETA)
Shabaha ya marekebisho haya ni kuongeza ufanisi katika usimamizi, urekebu na udhibiti wa ubora wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi yanayotolewa hapa nchini.
Kufuatia marekebisho ya sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte), jina la baraza hilo kwa sasa limebadilishwa na kuwa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NactVet).
Mabadiliko hayo ya sheria yameliongezea baraza hilo jukumu la urekebu na uthibiti ubora wa mafunzo ya ufundi stadi ambayo hapo awali yalikuwa yakifanyika chini ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta).
Taarifa iliyotolewa leo Februari 22 na Katibu Mtendaji wa NactVet Dk Adolf Rutayuga inaeleza kuwa mabadiliko hayo yanalenga kuongeza ufanisi.
Amesema shabaha ya marekebisho hayo ni kuongeza ufanisi, urekebu na uthibiti ubora wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi yanayotolewa nchini.
“Kwa mabadiliko haya ya sheria jukumu la urekebu na udhibiti ubora wa mafunzo ya ufundi stadi yamehamishiwa rasmi kutoka Veta hadi NactVet,” alisema Dk Rutayuga
Kufuatia hilo alisema maombi ya usajili wa vyuo, vituo na mafunzo ya ufundi stadi yanatakiwa kuwasilishwa NactVet ambako majukumu yamehamishiwa.
Katika hatua nyingine baraza hilo limetoa wito kwa vyuo na vituo vyote vilivyosajiliwa kutoa mafunzo ya ufundi stadi kuendelea kuendesha mafunzo hayo kwa mujibu wa sheria.
“Baraza litaendelea kushirikiana na wadau ikiwa ni pamoja na vyuo katika kuendeleza na kukuza utoaji wa elinh bora kwa ajili ya maendeleo ya taifa,”.