BABA TUPAC
JF-Expert Member
- Sep 30, 2015
- 1,526
- 3,802
Wakuu,
Leo nilikuwa kwenye kanisa moja lililopo Kitunda, kwa wasio pafahamu, ili kufika kitunda unaingilia njia ya Banana iliyopo barabara ya Gongo la Mboto.
Kama una shida yoyote ile na unahitaji kumuona Nabii huyo basi utatakiwa kulipia laki moja na nusu kama "consultation fee"
Nabii huyo, huwa anauza mafuta yake kwa waumini wake. Bei ya hayo mafuta ni kuanzia sh. 150,000
Hivyo wenye pesa huanza kununua mafuta kwa laki na nusu, baadae bei inashuka inafika laki moja, badae elfu hamsini na mwisho kabisa ni buku mbili.
Yani mafuta yale yale ambayo wengine wamenunua kwa laki na nusu lakini wewe unanunua buku mbili, nini maana yake? Kimsingi nabii hataki urudi nyumbani na pesa, yani pesa yoyote ile uliyonayo anaitaka na ndiomana huwa anaanzia bei ya juu huku akiendelea kushusha ili kuhakikisha kuwa kila mtu ametoa.
Endeleeni tu kwenda kanisa wakuu
Leo nilikuwa kwenye kanisa moja lililopo Kitunda, kwa wasio pafahamu, ili kufika kitunda unaingilia njia ya Banana iliyopo barabara ya Gongo la Mboto.
Kama una shida yoyote ile na unahitaji kumuona Nabii huyo basi utatakiwa kulipia laki moja na nusu kama "consultation fee"
Nabii huyo, huwa anauza mafuta yake kwa waumini wake. Bei ya hayo mafuta ni kuanzia sh. 150,000
Hivyo wenye pesa huanza kununua mafuta kwa laki na nusu, baadae bei inashuka inafika laki moja, badae elfu hamsini na mwisho kabisa ni buku mbili.
Yani mafuta yale yale ambayo wengine wamenunua kwa laki na nusu lakini wewe unanunua buku mbili, nini maana yake? Kimsingi nabii hataki urudi nyumbani na pesa, yani pesa yoyote ile uliyonayo anaitaka na ndiomana huwa anaanzia bei ya juu huku akiendelea kushusha ili kuhakikisha kuwa kila mtu ametoa.
Endeleeni tu kwenda kanisa wakuu