Fekifeki
JF-Expert Member
- Nov 18, 2011
- 1,453
- 570
Kumbe mpaka humu watu wanaCOPY na kuPASTE!!!Mimi ni Mkatoliki die hard. Huyu nabii alimpagawisha wife wangu na kutaka kulazimisha tuhamie kwake. Niligoma na amani nyumbani ilitoweka!.Nilipomuona kwenye TV, ni full mkorogo, katinda nyusi full mawanja ya kupitiliza na nywele za marehemu au artificial, nikachoka, nikamsomesha wife hivi kwa naked ayes only jinsi nabii anavyoonekana, unapata picha ya wazi anamtumikia nani!. Thanks to God, somo limeeleweka wife amerejea Katoliki na amani imerejea!.Bwana wetu Yesu Kristu, alisema "sio wote wanaita Bwana Bwana ni wangu!, watakuja watu watatoa mapepo kwa jina langu, lakini sio wangu"!.Wakamuuliza jee tutawatambuaje?.Yesu akajibu " Mtawatambua kwa matendo yao"!.Wito kwa wana jf wenzangu, imani zenu zisitetereshwa kwa miujiza ya manabii hawa, fuatilia matendo yao utawatambua!. Nadhani mwisho wa dunia umekaribia. Manabii wanazaliwa kama uyoga.