Mokaze
JF-Expert Member
- Aug 3, 2018
- 14,370
- 14,945
Kama utahisi masihara basi we hisi hivyo, ila me ndo nimeamua hivyo,
Nimefaulu vizuri ila shule nimeshindwa kwenda kwa hali ngumu, napambana na maisha lakini mwangaza siuoni, sina mbele wala nyuma, wachawi kila siku wananiwinda ili kunirudisha nyuma
Mama yangu ananipenda ila hana maisha na ana hali ngumu huku akinitegemea pamoja na mdogo wangu,
Baba yangu hana msaada na mimi na pia hana chochote, kiukweli nahisi nilizaliwa KIMAKOSA TU
sioni haja ya kuishi
Kweli wewe ni mjinga na mpumbavu kwelikweli, Kwani kukosa msaada katika hiyo shida yako ndio mwisho wa maisha yako??!-- kwani watu wote duniani walifanikiwa katika njia ya mteremko??, kwani ni wote wamefanikiwa kupitia kusoma??, vipi kama ungalikuwa kipofu au kiwete au mlemavu usiyejimudu??, unashindwa kumshukuru Mungu aliyekupatia nguvu, akili, uwezo nk, vitu ambavyo kwavyo unaweza kuvitumia katika mapambano kimaisha, jua kwamba kuna watu wanazo shida kubwa kuliko hiyo shida yako na bado wanapambana isitoshe wapo watu walipitia shida kubwa na walipambana bila kukata tamaa na Mungu aliwaona na leo ni watu wenye mafanikio makubwa, usikate tamaa na rehema za Mungu na umtegemee Yeye katika shida zako huku ukijibidiisha na pia usiogope kuomba msaada kwa watu kwani wapo watu wanaoweza kukusaidia.