Naanza kuhisi harufu fulani ITV

Naanza kuhisi harufu fulani ITV

Sioni hoja

Habari za Lowasa huoneshwa kila leo Channel 10;Clouds Tv na ITV...
 
Acha uongo wako Leo ITV nimeona wasira,lowassa,mtangaza nia mmoja (balozi)fulani
 
Sasa kaka tuache kuangalia habari za EL unataka tuangalie za Sitta na Wasira ? Hata lake zone kuna Tiivii waambie wawarushe kina Wasira. Leo EL alikua Bunda yaani sitting room kwa Wasira lkn waliojitokeza ni mara mia ya waliomsikiliza Wasira.
Mmeanza kuweweseka wakati hata kampeni bado. Mtazuia mafuriko na kikono.....
 
Chuki mbaya sana, unaweza kulichukia hata jiwe, ukalivunja eti unalikomoa!
 
Ukanda hapa una nafasi hata watu wajitutumue vp kuhusu hlo.Hata kipindi cha NIPASHE asubuhi, karushwa peke yake. Mangi ni mwizi sawa na Edo. Pia Mangi nı mbınafsı na amejaa hila nyingi.

Kumjoin Edo pia ni kutaka kumkomoa JK anayeonekana kuwa na gubu (gugu) kwake. Hawa jamaa wa kule wamejipanga na hata ukıangalia maeneo watokayo hawa wanaomshambulia mtoa mada ni ni North-Easterners. Hao ndo wanaoliibia sana taifa hili na ndio wameweka mtandao kulinda maslahi yao kila sekta.

Ndo maana unamwona Edo kazama kanda ya Ziwa, huko North anajua hapana matata, jamaa wapo kimaslahi sana. Hii nchi itatafunwa endapo Edo akishirikiana na wenzake akina Rosta, Mangi, n.k.Narudia, Mangı sio mtu mzurı msipaparikie.
 
Ni IPP kwa ujumla. Huoni hata gazeti la Nipashe? Mengi ndio kaanza kisasi kwa JK kupitia Lowassa. Hako kazee kanafiki kanafikiri Edo atakasamehe maovu ya miaka ilee kwake akipata urais ambao Masikini haupati.

Umenighusa kamanda.Majority are always wrong.Kale kajamaa nukusi hatare.Hapa ana mawili, mosi ni Ukanda(hili ni kweli bila hata tone ya shaka), pili nı bifu na JK.Kweli kama CCM wamebaki na umakını japo hata Kidogo na wana uchungu japo hata kidogo na nchii hii, wajihadharı kabisa na Lowasa pamoja na kundi lake.Hawa jamaa nı waizi sana.Pia huyu babu hakupendezwa na uwekezaji wa Dangote ndo msingi wa kelele zake za uzawa.
 
Chuki mbaya sana, unaweza kulichukia hata jiwe, ukalivunja eti unalikomoa!

Mamvi kaonyeshwa kla sehemu alipo enda kusaka wadhamini ukianza na Zanzibar, Mwanza, geita na mara na leo pia ataonyeshwa je hao wengine hawatafuti wadhamini ni yeye tu? kuna nini kiliendelea hapo?
 
UKIkaidi;
Weye wasema utapigwa2 miye nasema utampenda tu. CCM hamna mtu mwingine mtakayemleta kwetu bali Lowassa tu. Wote ni wachafu, basi mtamleta mwenye uwezo hata wa kuwalainisha watu kwa vijisenti vyake.

EL rais mtarajiwa. Usiichukie ITV bureee kwa visingizio hafifu ka hivi vyako ati hujakurupuka, ungekuwa umetulia sijui ungeandika nini ka hivi si kukurupuka.

Dah! Hali ngumu kweli maccm, mkiandikwa kosa, mkiacha kuandikwa kosa, yaani Tbccm haiwatoshi hadi mwaitaka na hii ya watu binafsi. Poleni, kipindi cha mtu kujitangaza yeye tu kimepitwa.

Mkuu mbona unaonesha uwezo mdogo sana??

Yaani unatuaminisha ni heri hata atakae lainisha wananchi na "vijisenti" vyake?...mkuu nyie ni wasomi tuliowasomesha kwa kodi zetu mtusaidie halafu ndio unanishauri hovyo hivi kumchagua rais au kiongozi yeyote?

Aisee kama wewe nimfurukutwa wa Lowassa ni sawa,una haki hiyo lakini usituwekee mavi mdomoni tule,usiwe unapenda kulazimisha imani yako wenzio waifuate,utaonekana hayawani tu...Tushajua wewe ni mtu wa Lowassa,inatosha,vingine vitafanya tu-question your IQ
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mbona unaonesha uwezo mdogo sana??

Yaani unatuaminisha ni heri hata atakae lainisha wananchi na "vijisenti" vyake?...mkuu nyie ni wasomi tuliowasomesha kwa kodi zetu mtusaidie halafu ndio unanishauri hovyo hivi kumchagua rais au kiongozi yeyote?

Aisee kama wewe nimfurukutwa wa Lowassa ni sawa,una haki hiyo lakini usituwekee mavi mdomoni tule,usiwe unapenda kulazimisha imani yako wenzio waifuate,utaonekana hayawani tu...Tushajua wewe ni mtu wa Lowassa,inatosha,vingine vitafanya tu-question your IQ

LebronWade;
Naomba nikutoe hofu kabisa. Mimi na Lowasa ni paka na panya. Hakuna siku hata moja nitampa kura yangu ila nakuhakikishia kuwa huko ccm hawana mtu mwingine yeyote watathubutu kumsimamisha na upinzani haswa UKAWA. Hivyo, kwa sababu, ccm pesa ndo nguvu yao watamsimamisha Lowasa atumie njuluku zake kulainisha watu angalao ccm wapate kura mbili tatu za kuonesha walitikisa UKAWA. Usiogope mkuu nitakuwa wa mwisho kushabikia maccm. Pole kwa kunielewa vibaya, nisamehe kwa andiko lililokuchefua mkuu. UKAWA daima
 
Ni kweli mkuu nakubaliana na wewe. Kuna kitu kati ya Lowasa na ITV. Kila kukicha Lowasa, Lowasa, utadhani udhamini anatafuta peke yake. Wengine wanaoneshwa kimagumashi tu ili kuzuga isionekane wazi kama wanaupendeleo maalum kwa mzee mamvi. Lkn ukweli unabaki palepale kuwa ITV wana kitu na Lowasa
 
Back
Top Bottom