Na alaniwe kila atoae mimba isemwe ameen.

daah nimekuwa down mno kwa kuona hii pic, just more info please, huyu inaweza kuwa ni kiumbe wa miezi mingapi? maana ni binadamu kabisa aliyekamilika na natafakari na kuelewa kuwa watu wanaposema mtoto akiwa tumboni kwa mama yake anasikia na kuelewa kama unaongea nae na anaumia na kufurahi yaania anakuwa na hisia zote kama binadamu maana hapo ni full binadamu

Hii ni kati ya wiki ya 12 mpaka 16, hapa hata mapigo ya moyo yanaweza sikika vizuri tuu kwa kutumia sonogram.
 
Alaaniwe amlaainie binadamu mwenzake.
God is the judge

Kumbukumbu la Torati:27: 16 -26


16 Na alaaniwe amdharauye baba yake au mama yake. Na watu wote waseme, Amina.

17
Na alaaniwe aondoaye mpaka wa jirani yake. Na watu wote waseme, Amina.

18
Na alaaniwe ampotezaye kipofu akakosa njia. Na watu wote waseme, Amina.

19
Na alaaniwe apotoaye hukumu ya mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe. Na watu wote waseme, Amina.

20
Na alaaniwe alalaye na mke wa baba yake, kwa kuwa amefunua mavazi ya babaye. Na watu wote waseme, Amina.

21
Na alaaniwe alalaye na mnyama wa aina yo yote. Na watu wote waseme, Amina.

22
Na alaaniwe alalaye na umbu lake, binti ya babaye, au binti ya mamaye. Na watu wote waseme, Amina.

23
Na alaaniwe alalaye na mkwewe, mamaye mkewe. Na watu wote waseme, Amina.

24
Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri. Na watu wote waseme Amina.

25
Na alaaniwe atwaaye ujira wa kumwua asiye makosa. Na watu wote waseme, Amina.

26
Na alaaniwe asiyeyaweka imara maneno ya torati hii kwa kuyafanya. Na watu wote waseme, Amina.


 
532515_551513274886987_2038712070_n.jpg



DON'T IGNORE TO COMMENT: STOP ABORTION

na watu wote waseme amina
 
Sie wanadamu tuko tofauti sn..Mungu atuhurumie sn wandugu. Wote tuliochangia uzi huu tumekazania "alaaniwe, alaaniwe" Mbona tunahukumu dhambi ya uuaji tu hapo vipi kuhusu dhambi ya uzinzi ambayo asilimia kubwa tunaitenda kila siku iwe kwa kuwaza, kunena au kutenda? Tukumbuke aliyeamrisha "USIUE" ndiye huyohuyo aliyeamrisha "USIZINI" tena ametuambia "TUSIHUKUMU TUSIJE TUKAHUKUMIWA" jiulize tangu asubuhi umevunja amri ngapi za MUNGU? Tumesaidia maskini au hadi watukuombe? Hatujasengenya wanafki sie?? ALIESEMA USIZINI NDIYE ALIYESEMA USIUE..UKIVUNJA AMRI MOJA UMEVUNJA ZOTE KUMI..
 
mungu atusamehe napata uchungu nnapoona dada ang akiwa anatafuta mtoto zaid ya miaka kumi lakini wengine wakiwa hawawataki na kuwatoa
 
Tena na alaaniwe....na wengi wao huwa hawana amani na maisha yao..damu za vitoto zinawazunguka
 
Back
Top Bottom