N. Korea vows 'merciless' war against US

N. Korea vows 'merciless' war against US

Hitler alianza kwa staili hii kuzitisha nchi kubwa na dunia ikaogopa . Siku nchi kubwa zilipoamua kuwa inatosha walimzingira wakampiga kama mtoto na alipoona mambo magumu aliamua kujiua kwa sumu na kuamuru achomwe moto kuliko kukamatwa na warusi. Inaonekana huyu dogo hasomi historia au labda anataka historia ijirudie akiwa kama specimen.

Wakati hitler anaingia vitani ...Ujerumani ilikuwa Moja ya super powers ...sio Kama ilikua Taifa dogo tu ..hapana ...Baada ya Kushindwa vita Ujerumani ikawekewa vizingiti Vya kuimarisha jeshi lake ....Kama sehemu ya cease fire agreement ...au MKATABA wa Kushindwa vita .....
Ukivamia Nchi na ukaipiga unakua na haki Fulani ya kuingia MKATABA ya Siri na Nchi husika wenye lengo la kuizuia isijiimarishe na kutaka kuingia tena vitani na wewe ....tungeweza kuwafanya Hivyo Uganda ...
 
Hawajachotwa Akili Kama tunavyodhani ila wana descipline na Uzalendo ...kwa maendeleo ya Sayansi na technologia wanayoyafanya ...sio Taifa la kubeza ...wanapiga hatua kuliko hayo mataifa yenye Kupendwa na marekani

Hapana aisee. Hao wamechotwa akili.

Haiwezekani hiyo nchi itawaliwe na watu wa familia moja tu tena ambao hutoa amri kuwa watu wengine hawatakiwi kuwa na majina kama yao.

Sasa hivi huko NK ni marufuku kwa yeyote yule kuitwa Jong-Un.

Na wao wanafuata kweli hizo amri. Huo si uzalendo bali ni ufala.

Hata sayansi na teknolojia yao haitishi.
 
Hitler alianza kwa staili hii kuzitisha nchi kubwa na dunia ikaogopa . Siku nchi kubwa zilipoamua kuwa inatosha walimzingira wakampiga kama mtoto na alipoona mambo magumu aliamua kujiua kwa sumu na kuamuru achomwe moto kuliko kukamatwa na warusi. Inaonekana huyu dogo hasomi historia au labda anataka historia ijirudie akiwa kama specimen.

Mkuu Hitler alikuwa sio mdogo mziki wake ulikuwa mkubwa kipndi kile alikuwa super power Ufaransa mwenyewe alisalimu amri,jamaa waliingia adi Paris na nchi nyingne za Ulaya kama Poland,Belgium,bila Mrusi na Mmarekani kuingilia kati hata uingereza alikuwa anaondoka,mistake yake kubwa aliyofanya ni kuanzisha timbwili na Mrusi akawa anapigana vita mbili kwa wakati moja na hali ya hewa ya Urusi ya baridi kali ndio ikawa makabuli ya wanajeshi wake,lakn kama angepigana na Ulaya na bila Mmarekan na Mrusi kuingia Ulaya nzima angeshaiteka pamoja na Uingereza,huyu jamaa wa North Korea bado cha mtoto mtoto,huyo ni kama Sadam kelele nyingi mwisho wa siku unaenda kujificha kwenye shimo
 
Hakuna jipya hapo.

Wanachoweza kufanya ni kurusha tu hivyo vikombora vyao baharini na si mara yao ya kwanza kufanya hivyo.

Ni mwendelezo ule ule wa mikwara (hususan mazoezi ya pamoja ya kivita kati ya South Korea na Marekani yakiwa yanakaribia kuanza).

Ingekuwa wamerusha hivyo vikombora Seoul na kudondosha lile ghorofa la Samsung hapo labda ndo ingekuwa shida.

Lakini hii ya kurusha baharini wala si tatizo. Washafanya sana hivyo.

Acha kuishi kwa mazoea mkuu.mambo yanabadilika.dont you see it has been so long since NK Started the so called bit?why dont USA step into NK land?usa anajua kuwa mambo sio mchezo.ingekuwa n propaganda the way you say usa asingekuwa anapoteza time kupiga kelele ya nuclear na NK kama hakuna.then who is usa to dominate the whole world?sahz lazma anywee.akpga kelele ukraine ana mkuta putin,akzunguka kdogo anaonyeshwa ukaka na NK.NK keep it up,no body owns this planet neither usa nor europian countries
 
Acha kuishi kwa mazoea mkuu.

Wewe huishi kwa mazoea?

mambo yanabadilika.dont you see it has been so long since NK Started the so called bit?why dont USA step into NK land?

USA iende ikatafute nini huko NK? Marekani haiwezi tu kuivamia NK kisa NK wanapenda kuchimba mikwara. Mikwara si sababu ya kuanzisha vita vya silaha za moto wewe. Vita unaijua unaisikia?

usa anajua kuwa mambo sio mchezo.

Hata NK anajua kuwa kuanzisha timbwili na USA ndo utakuwa mwisho wake huo. Ndo maana huwa anaishia kubwabwaja tu kama mbwa koko.

ingekuwa n propaganda the way you say usa asingekuwa anapoteza time kupiga kelele ya nuclear na NK kama hakuna.

Hata USA nao huwa wanapiga hizo propaganda. No one is above it. Halafu si kwamba USA wanapoteza muda kivile kuhusu hivyo vibomu vya NK.

then who is usa to dominate the whole world?

The US of A is the world's sole super power. If you don't know now you know.

sahz lazma anywee.

In your dreams.

akpga kelele ukraine ana mkuta putin,

Huyo naye hana lolote.

akzunguka kdogo anaonyeshwa ukaka na NK.NK keep it up,no body owns this planet neither usa nor europian countries

Teh teh teh.....suck it.
 
Natural Resources


North Korea is one of the richer nations in Asia in terms of mineral resources. Major reserves are found of coal, iron ore, tungsten, magnesite, and graphite. Among the other minerals present are gold, silver, copper, lead, zinc, and molybdenum.


Hicho ndo anatafuta USA na mshirika wake SK. Aidha pamoja na Japan kuiba kwa miaka lukuki bado wana hazina ya kutosha na wanaitumia vizuri kuliko Miafrika inavyotumia mali zao.. Nyani Ngabu.
 
Last edited by a moderator:
Natural Resources


North Korea is one of the richer nations in Asia in terms of mineral resources. Major reserves are found of coal, iron ore, tungsten, magnesite, and graphite. Among the other minerals present are gold, silver, copper, lead, zinc, and molybdenum.

Hicho ndo anatafuta USA na mshirika wake SK. Aidha pamoja na Japan kuiba kwa miaka lukuki bado wana hazina ya kutosha na wanaitumia vizuri kuliko Miafrika inavyotumia mali zao.. Nyani Ngabu.

Nigga pliiiz.

Kama ni matajiri hivyo mbona huwa wanakufa njaa?
 
Hawa jamaa pamoja na shida zote ule mji mkuu wao Pyongyang uko bomba na adi wana treni za underground za umeme,sijui wasingekuwa na vikwazo na wasingekuwa wabishi wangekuwa sawa na ndugu zao wa South tena na kuwapita kwa sababu wana natural resources nyng kuliko South
 
Naamini huyu jamaa anajitambua. Ndoo maana hashabikii Hawa wakoloni weupe.
 
The same old primitive discussion,this proves that there is lack of relevant knowledge about international politics.Watu wanazungumza kwa kasumba na ushabiki bila hata kujijua.Ubongo wao umefungwa kujua ukweli ulivyo kuhusu siasa za dunia.Mimi sipingi watu kufahamu taarifa kama hizi,ila nashauri watu wajitahidi kupanua mawazo yao mbali zaidi nje ya maistream media,hapo ndipo mtakapojua ukweli.
-Ushabiki wa kwamba nani ana nguvu za kijeshi zaidi ya mwingine utatusaidia nini?

-Kuna watu wanasema NK inaongozwa kidikteta,je hawa watu wanajua kwamba marekani ni dikteta na gaidi namba moja duniani?Hakuna nchi hata moja duniani inayoongozwa kwa demokrasia,kama kweli mnajua maana ya demokrasia.

-Kuna watu wanasema kwamba watu wa NK hawapigi kura kuchagua kiongozi wao,je watu hawa wanajua kwamba raisi wa marekani hachaguliwi na wananchi wa marekani bali anawekwa na matajiri ambao hasa ndio wanaoongoza marekani ili kutimiza agenda zao?Na kama raisi hafuati maagizo ya matajiri hao anaondolewa madarakani au anauawa,remmember JF kennedy?

-Kuna mtu anasema NK inaongozwa na familia moja tu,je huyu mtu anajua marekani anayoishabikia kama inaongozwa na familia za watu wasiozidi saba na maraisi wa marekani kama vile Obama ni watumwa tu wa hizo familia?

-Kuna watu wanasema NK inafanya wananchi wake kama watumwa,je hawa watu wanajua kama marekani wanafanya watu karibu wa dunia nzima kuwa watumwa hasa nchi zetu za kiafrika?

-Hivi watu wanafahamu vizuri kweli historia ya NK na SK na kwa nini ziko katika hali hii tunayoiona leo?Au tunaongea kwa ushabiki tu?

-Hayo maswali ni sehemu ndogo tu ya mambo ambayo watu wanatakiwa kuyajua na si propaganda za vyombo vya habari vya magharibi ambavyo hurubuni akili za watu kila kukicha.

-Nashauri tupende kutafuta habari nje ya mainstream ambapo ndio mambo yaliyojificha hufunuliwa.Tuache ushabiki usio na tija kwa kuwa ipo siku mtu ataathirika kwa kukosa taarifa sahihi.Mfano:Kwa uelewa huu niliuona hapa watu wenye kasumba nilizoainisha hapo juu wana uwezekano mkubwa sana kwamba wanajua HIV/AIDS haina tiba ilihali tiba ipo lakini hawajui kwa sababu ya kung'ang'ania ushabiki wa kijinga kwa marekani.Najua kuna watu wataniona mm kichaa,fuatilia haya kwanza ndipo utagundua kwamba hao wamarekani mnaowashabikia wamefanya blunder ya karne kwenye hili la HIV/AIDS.Watu wanaoshabikia marekani inabidi wafahamu kwamba hao tunaowasifia ndio wanasababisha leo hii waafrika na maeneo mengine wanakufa kama kuku kwa magonjwa yanayotibika(kansa/saratani,kisukari,AIDS nk) na vita vya wenyewe kwa wenyewe.Amkeni,we real need to RE-LEARN.

Mpui Lyazumbi ni mmoja wa watu ambao watakuwa wamenielewa vizuri maana anaonekana anajua vizuri siasa za marekani.
 
The same old primitive discussion,this proves that there is lack of relevant knowledge about international politics.Watu wanazungumza kwa kasumba na ushabiki bila hata kujijua.Ubongo wao umefungwa kujua ukweli ulivyo kuhusu siasa za dunia.Mimi sipingi watu kufahamu taarifa kama hizi,ila nashauri watu wajitahidi kupanua mawazo yao mbali zaidi nje ya maistream media,hapo ndipo mtakapojua ukweli.
-Ushabiki wa kwamba nani ana nguvu za kijeshi zaidi ya mwingine utatusaidia nini?

Hebu ngoja tuone na wewe umeandika nini.

-Kuna watu wanasema NK inaongozwa kidikteta,je hawa watu wanajua kwamba marekani ni dikteta na gaidi namba moja duniani?

Nitajie dikteta mmoja wa Marekani, tafadhali. Na katika kufanya hivyo weka kabisa na fasili ya neno 'dikteta' ili tuweze kupata msingi mzuri wa hoja.

Hakuna nchi hata moja duniani inayoongozwa kwa demokrasia,kama kweli mnajua maana ya demokrasia.

Wewe unaijua maana ya demokrasia? Kama unaijua tueleze basi na si wengine ambao umedokeza kuwa hatuijui.

-Kuna watu wanasema kwamba watu wa NK hawapigi kura kuchagua kiongozi wao,je watu hawa wanajua kwamba raisi wa marekani hachaguliwi na wananchi wa marekani bali anawekwa na matajiri ambao hasa ndio wanaoongoza marekani ili kutimiza agenda zao?

Hao matajiri ni akina nani [wataje majina yao] na agenda zao ni zipi[ziorodheshe ukiambatanisha na vyanzo]?

Na una ushahidi gani kuwa rais wa Marekani "hachaguliwi na wananchi wa marekani bali anawekwa na matajiri ambao hasa ndio wanaoongoza marekani"?

Na kama raisi hafuati maagizo ya matajiri hao anaondolewa madarakani

Madai makubwa kama haya huhitaji ushahidi mkubwa na madhubuti. Lete vyanzo na ushahidi wa haya madai yako.

au anauawa,remmember JF kennedy?

Kennedy aliuwawa na hao matajiri kwa sababu hakufuata maagizo yao? Okay, sawa, lete ithibati ya madai yako hapa.

-Kuna mtu anasema NK inaongozwa na familia moja tu,je huyu mtu anajua marekani anayoishabikia kama inaongozwa na familia za watu wasiozidi saba na maraisi wa marekani kama vile Obama ni watumwa tu wa hizo familia?

Zitaje hizo familia saba ukiambatanisha na ithibati madhubuti.

-Kuna watu wanasema NK inafanya wananchi wake kama watumwa,je hawa watu wanajua kama marekani wanafanya watu karibu wa dunia nzima kuwa watumwa hasa nchi zetu za kiafrika?

Kabla ya kwenda mbali, tuanze na fasili ya neno 'utumwa'. 'Utumwa' ni nini? Baada ya hapo lete ushahidi wa Marekani kuifanya dunia nzima kuwa watumwa hasa hizi nchi zetu za Kiafrika.

-Hivi watu wanafahamu vizuri kweli historia ya NK na SK na kwa nini ziko katika hali hii tunayoiona leo?

Wewe unaifahamu? Kama unaifahamu na unaona siye wengine hatuifahamu, tufahamishe basi kile ambacho wewe unakifahamu ambacho siye hatukifahamu.

Au tunaongea kwa ushabiki tu?

Kama kuna aliyeandika kishabiki tu basi wewe ndo unaongoza kwani hujatoa ithibati, ki/vidhibiti, wala ushahidi wowote ule kuambatana na madai yako ya kipuuzi kabisa uliyoyatoa.

-Hayo maswali ni sehemu ndogo tu ya mambo ambayo watu wanatakiwa kuyajua na si propaganda za vyombo vya habari vya magharibi ambavyo hurubuni akili za watu kila kukicha.

Nchi za Mashariki zenyewe hazina propaganda zinazorubuni watu wenye akili kama zako? Manake kama kuna mhanga wa propaganda basi wewe utakuwa juu kwenye orodha ya watu hao.

-Nashauri tupende kutafuta habari nje ya mainstream ambapo ndio mambo yaliyojificha hufunuliwa.

Wapi huko? Kwenye mitovuti ya ma conspiracy theorists, birthers, truthers, holocaust deniers, na kadhalika? Huko ndiko ulipoyatoa hayo ma conspiracy theory yako uliyoyatapika humu? Unachekesha!

Tuache ushabiki usio na tija kwa kuwa ipo siku mtu ataathirika kwa kukosa taarifa sahihi.

Tatizo la washabiki ni kuona watu wengine kuwa ni washabiki na wao kutokujiona kuwa ni washabiki. Mambo ya projection hayo!!

Mfano:Kwa uelewa huu niliuona hapa watu wenye kasumba nilizoainisha hapo juu wana uwezekano mkubwa sana kwamba wanajua HIV/AIDS haina tiba ilihali tiba ipo lakini hawajui kwa sababu ya kung'ang'ania ushabiki wa kijinga kwa marekani.

HIV/ AIDS ina tiba? Iko wapi hiyo tiba yake? Nani anayo? Na wewe umejuaje kuwa ipo? Ulipata AIDS ukaitafuta na kuitumia halafu ukapona?

Najua kuna watu wataniona mm kichaa,

Teh teh teh....walau umejistukia mapema. Maana kwa huu utumbo ulioutapika hapa sidhani kama ungekuwa na akili timamu ungefanya hivyo.

fuatilia haya kwanza ndipo utagundua kwamba hao wamarekani mnaowashabikia wamefanya blunder ya karne kwenye hili la HIV/AIDS.

Blunder gani hiyo ya karne ambayo Wamarekani wameifanya?

Watu wanaoshabikia marekani inabidi wafahamu kwamba hao tunaowasifia ndio wanasababisha leo hii waafrika na maeneo mengine wanakufa kama kuku kwa magonjwa yanayotibika(kansa/saratani,kisukari,AIDS nk) na vita vya wenyewe kwa wenyewe.Amkeni,we real need to RE-LEARN.

Wewe hebu wahi ukamwone daktari wa magonjwa ya akili kabla hujajidhuru au kudhuru wengine!!

ni mmoja wa watu ambao watakuwa wamenielewa vizuri maana anaonekana anajua vizuri siasa za marekani.

Pwa! Ha! Ha! Ha! Ha! Ha! Inawezekana hujajiita hilo jina lako [Deception] kwa bahati mbaya.

GO USA :usa2::usa2::usa2::usa2::usa2::usa2::usa2::usa2::usa2::usa2::usa2: GO!
 
Wakuu, lakini mnajua kuwa North Korea wamewahi kupigana na USA kwenye vita vya Korea na US wakachemsha? Nashangaa watu mnalisahau hilo mapema hivi! Majigambo yao yanatokana na hiyo vita, ambayo wao wanaona ulikuwa ni ushindi dhidi ya hili li-nchi lenye mabavu mengi na uwezo mkubwa wa kivita. Hata Vietnam US hawakutemea kuwa wangegaragazwa vibaya hiyo na kukimbia. Historia itukumbushe kujifunza.
 
Kumbe nani aliivumbua? Kim Il Sung?

Collection ya watu mbali mbali ndo wali develop Internet hapa duniani. Mrusi kachangia sehemu kubwa sana. Ndo maana yeye anaweza ku hack net za USA lakini USA hawezi ku hack net za russia. Mkuu kinachokuaribu ni kuwa na ushabiki wa kupitiliza. Inaonekana wewe ndo wale wabeba maboksi.
Mara ya mwisho umetoka lini America? au bado hupo huko?.....LOL
 
Wengi hawaelewi kuwa technolojia nyingi iliyo mtaani ni ile ambayo tayari US waliitumia na kuiacha baada ya kuona haiwafai tena au yahitaji kupata nyingine hivyo wakaileta public, kuanzia GPS hadi Internet etc
 
Deception umeeleza vizuri zaidi, naona lengo la Nyani Ngabu ni kuomba kufafanuliwa hujuma za USA katika kulinda maslahi yake kama "Super Power". Hapa panaweza kusaidia japokuwa anahitaji kufanya home work zaidi. Kudos mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Hicho kijamaa kinajua sana kuchimba biti.

Na hizo biti tumeshazizoea na wengine huwa zinatuchekesha sana.

Ni bora angejikita katika kuboresha maisha ya watu wake ikiwemo kuwapa uhuru wa kuona na kujua yanayoendelea nje ya hiyo nchi.

Hao watu wanaishi kama kuku wa kufugwa. Wanatia huruma. Wamechotwa akili.

Sielewi kwa nini mamiioni ya watu waweze kuchotwa akili na familia moja namna hiyo.

Halafu eti jina rasmi la hiyo nchi ni DPRK (Democratic People's Republic of Korea).

Hivi wanafanyaga hata chaguzi hao watu?

Vichekesho!!

wewe wanakuhusu nin?alaf mbona unapenda kuzungumza kwa niaba ya wamarekan?
 
Collection ya watu mbali mbali ndo wali develop Internet hapa duniani. Mrusi kachangia sehemu kubwa sana. Ndo maana yeye anaweza ku hack net za USA lakini USA hawezi ku hack net za russia. Mkuu kinachokuaribu ni kuwa na ushabiki wa kupitiliza. Inaonekana wewe ndo wale wabeba maboksi.
Mara ya mwisho umetoka lini America? au bado hupo huko?.....LOL

Weka ushahidi wa mchango wa huyo Mrusi.
 
Back
Top Bottom