N. Korea vows 'merciless' war against US

N. Korea vows 'merciless' war against US

Kana kitu kizito ndicho kinachompa kibri na kalivyo na akili finyu haka kajamaa kanaweza kukiachia kitu kizito na kuathiri sehemu kubwa ya dunia kwa miaka chungu nzima ijayo.

Kinachoshangaza ni Marekani kuwaacha waendelee na mikwara yao, kwanini asiwaswage kama Saddam?
 
Haka kajamaa ni stubborn kweli, sijui kwanini Marekani wameiacha hii familia kuendelea kutamba mpaka leo!

Marekani haina sababu yoyote ile ya kuanzisha timbwili huko North Korea.

North Korea zaidi ya kelele za mbwa koko si tishio kivile na haina rasilimali zozote zile za kuifanya Marekani iingilie mambo yake ya ndani.

Nchi yenyewe imetengwa (au sijui imejitenga) na karibu dunia nzima.

Ila siku wakitaka kuwaona marines wa Kimarekani ndani ya Pyongyang basi ni ama waishambulie Seoul na kudondosha yale ma vikwangua anga au wafadhili magaidi wa kuishambulia Marekani kama alivyofanya Osama kwa msaada wa Taliban wa Afghanistan.

Hapo ndo utakuwa mwanzo wa mwisho wa akina Kim.

Zaidi ya hapo Marekani haitasumbuka nao na wala mikwara yao haikoseshi mtu usingizi.
 
Kana kitu kizito ndicho kinachompa kibri na kalivyo na akili finyu haka kajamaa kanaweza kukiachia kitu kizito na kuathiri sehemu kubwa ya dunia kwa miaka chungu nzima ijayo.
Na aendelee kukitunza ili heshima iendelee kuwepo!!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kana kitu kizito ndicho kinachompa kibri na kalivyo na akili finyu haka kajamaa kanaweza kukiachia kitu kizito na kuathiri sehemu kubwa ya dunia kwa miaka chungu nzima ijayo.

Mimi siwaamini kivile hao jamaa. Hata hivyo vibomu vyao sijui vya nyuklia vinaweza vikawalipukia wenyewe na kuwadhuru kabla hata havijadhuru wengine.

Na pamoja ya kwamba kanaonekana hakana akili nzuri bado siamini kwamba ni kapumbavu kiasi cha kuweza kuanzisha timbwili na Marekani maana nchi nzima itaangamizwa.

Hata kuanzisha timbwili na South Korea hakawezi maana kanajua ndo utakuwa mwisho wake.

Sana sana huwa kunakuwa na rabsha rabsha tu za hapa na pale kati ya South na North lakini huwa hazifikii level ya full-blown war.
 
Hapo napo kuna utata kwamba kanadanganya Ulimwengu kwamba kana kitu kizito, lakini wachunguzi wengi duniani wa mambo haya wanaamini jamaa anacho kitu kizito. Ndio sababu wanakuwa makini mno katika kukatia adabu.

Mimi siwaamini kivile hao jamaa. Hata hivyo vibomu vyao sijui vya nyuklia vinaweza vikawalipukia wenyewe na kuwadhuru kabla hata havijadhuru wengine.

Na pamoja ya kwamba kanaonekana hakana akili nzuri bado siamini kwamba ni kapumbavu kiasi cha kuweza kuanzisha timbwili na Marekani maana nchi nzima itaangamizwa.

Hata kuanzisha timbwili na South Korea hakawezi maana kanajua ndo utakuwa mwisho wake.

Sana sana huwa kunakuwa na rabsha rabsha tu za hapa na pale kati ya South na North lakini huwa hazifikii level ya full-blown war.
 
wanapata acces ya intanet toka china na kwa taarifa yako wanajua kila kinacho endelea duniani Okey?

Hahahaaa dude, China kwenyewe intaneti inachungwa na kuna baadhi ya tovuti ni marufuku.

North Korea sanasana mwenye access na internet labda ni Kim na ukoo wake na alivyo mpumbavu huenda keshapiga marufuku watu wengine wote kuwa na access kama alivyopiga marufuku watu wengine kuwa na jina linalofanana na yeye.
 
Hapo napo kuna utata kwamba kanadanganya Ulimwengu kwamba kana kitu kizito, lakini wachunguzi wengi duniani wa mambo haya wanaamini jamaa anacho kitu kizito. Ndio sababu wanakuwa makini mno katika kukatia adabu.

Operative word hapo ni 'wanaamini'. Hivyo hawajui.

Lakini hata kama anacho, sidhani wana uwezo na utaalamu wa kutosha wa kuweza kuki-handle.

Na sidhani anazo mechanisms za kutosha za kuweza kutishia nchi za mbali kama Marekani, Uingereza, au Ufaransa.

Kwa sasa aendelee tu na kutupatia comic relief ya biti kali za ki-mbwa koko.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mikwara ya hivi hata Saddam na Gaddafi walikuwa nayo

Sijui Saddam alisomea kuchimba biti huko North Korea maana na yeye alikuwa stadi sana wa kuchimba biti.

Sijui 'mother of all battles' mara sijui hawezi kukamatwa akiwa hai....matokeo yake akaja kukamatwa akiwa kajificha kwenye kishimo.....a far cry from his palatial homes.



Halafu unamkumbuka huyu jamaa? Eti alikuwa anabisha vifaru vya Marekani havipo Baghdad wakati dunia nzima ilikuwa inaona tanks za Marekani zikijivinjari kwenye mitaa ya huo mji.

 
Last edited by a moderator:
kwani ccm mmeacha kuiba kura halafu kwanini unapenda kumweka nyerere in those bars

Akiandikia gazeti la "The London Observer" mwaka 1963, mwaka mmoja tu tangu kuanzishwa kwa nafasi ya "Rais Mtendaji" nchini, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, aliwahi kukiri jambo hili kwa kusema: "…kusema kweli, Katiba (hii) inanifanya dikteta kwa kigezo chochote kile cha kidemokrasia".

- See more at: Raia Mwema - Madaraka ya Rais asiyeambilika yanazaa udikteta
 
Hicho kijamaa kinajua sana kuchimba biti.

Na hizo biti tumeshazizoea na wengine huwa zinatuchekesha sana.

Ni bora angejikita katika kuboresha maisha ya watu wake ikiwemo kuwapa uhuru wa kuona na kujua yanayoendelea nje ya hiyo nchi.

Hao watu wanaishi kama kuku wa kufugwa. Wanatia huruma. Wamechotwa akili.

Sielewi kwa nini mamiioni ya watu waweze kuchotwa akili na familia moja namna hiyo.

Halafu eti jina rasmi la hiyo nchi ni DPRK (Democratic People's Republic of Korea).

Hivi wanafanyaga hata chaguzi hao watu?

Vichekesho!!

Mkuu unazungumzia uhuru wa kujua mambo ya nchi nyingine kama ule America na allies waliopeleka misri, Afghanistan, Syria, Iraq, Libya na nyinginezo?
 
Mkuu unazungumzia uhuru wa kujua mambo ya nchi nyingine kama ule America na allies waliopeleka misri, Afghanistan, Syria, Iraq, Libya na nyinginezo?

Sidhani hizo nchi zingine, ukiondoa labda Afghanistan, licha ya kwamba na zenyewe zilikuwa au zinaendeshwa kidikteta, unaweza kuzilinganisha na Korea Kaskazini.

Hata Zimbabwe chini ya Mugabe sasa hivi ina nafuu maradufu kuliko Korea Kaskazini.
 
Back
Top Bottom