N. Korea vows 'merciless' war against US

N. Korea vows 'merciless' war against US

Huyu jamaa ana mikwara tu kama baba yake, sio mara ya kwanza naskia North Korea inamtishia Marekani but each time sijawahi kuona action

Mkuu USA ndio ina mikwara kuhusu nuclear ya jamaa lakini hamna kitu.
Kama watu wanadhani ni mchezo US anzishe vita 21C aone kazi ya nuclear, alipiga watu enzi zile sio hizi zama za technolojia, utandawazi na biashara huria.
 
Marekani haina sababu yoyote ile ya kuanzisha timbwili huko North Korea.

North Korea zaidi ya kelele za mbwa koko si tishio kivile na haina rasilimali zozote zile za kuifanya Marekani iingilie mambo yake ya ndani.

Nchi yenyewe imetengwa (au sijui imejitenga) na karibu dunia nzima.

Ila siku wakitaka kuwaona marines wa Kimarekani ndani ya Pyongyang basi ni ama waishambulie Seoul na kudondosha yale ma vikwangua anga au wafadhili magaidi wa kuishambulia Marekani kama alivyofanya Osama kwa msaada wa Taliban wa Afghanistan.

Hapo ndo utakuwa mwanzo wa mwisho wa akina Kim.

Zaidi ya hapo Marekani haitasumbuka nao na wala mikwara yao haikoseshi mtu usingizi.

Dogo acha kuota, jamaa wana nuke ila kibebeo ndo tatizo, namaanisha deliverance. Ila kama wanacho ni mtihani halafu hawana shida ya kupeleka america, wakipeleka kusini kwa ndugu zao tu ni tosha for reunification
 
Sidhani hizo nchi zingine, ukiondoa labda Afghanistan, licha ya kwamba na zenyewe zilikuwa au zinaendeshwa kidikteta, unaweza kuzilinganisha na Korea Kaskazini.

Hata Zimbabwe chini ya Mugabe sasa hivi ina nafuu maradufu kuliko Korea Kaskazini.

Mkuu nje ya mada kidogo
Kampuni za Samsung na LG zipo south au North Korea, hizi series tunazozifuatilia nazo niw za South au North?
 
Dogo acha kuota,

Na wewe acha kuota.

jamaa wana nuke ila kibebeo ndo tatizo,

Hata kama wanazo basi watakuwa nazo zile za kiwango cha chini kabisa na ipo siku yatawavujia na kuwaua wenyewe.

namaanisha deliverance.

Okay

Ila kama wanacho ni mtihani halafu hawana shida ya kupeleka america, wakipeleka kusini kwa ndugu zao tu ni tosha for reunification

Hata Kusini wanazo vilevile na hawatasita kuzirusha Pyongyang. Na zikirushwa sijui huyo Lil' Kim atakimbilia wapi....
 
Hapo napo kuna utata kwamba kanadanganya Ulimwengu kwamba kana kitu kizito, lakini wachunguzi wengi duniani wa mambo haya wanaamini jamaa anacho kitu kizito. Ndio sababu wanakuwa makini mno katika kukatia adabu.

mkuu BAK suala la North Korea kumiliki nukes si la kuaminika ni ukweli mtupu na hata wamarekani na washirika wao wanalifahamu hilo na wanaogopa ukizingatia sasa hivi anamiliki Taepodong 1na taepodong 2ambayo ni ICBM ambayo inauwezo wa kupiga mpaka upande wa mashariki wenye majimbo ya New York, New Jersey, North na South Carolina na mengineyo acha ule wa magharibi unaopakana nayo kwa bahari wenye LA, Frisco, nk. kwa hiyo America na South Korea wanajua nini IL sung, Jong IL na Jong un wanazungumzia.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Wabongo mnajua kujudge vitu sana, but nchi yenu yenyewe inateketea, hamna maamuzi magumu
 
Hicho kijamaa kinajua sana kuchimba biti.

Na hizo biti tumeshazizoea na wengine huwa zinatuchekesha sana.

Ni bora angejikita katika kuboresha maisha ya watu wake ikiwemo kuwapa uhuru wa kuona na kujua yanayoendelea nje ya hiyo nchi.

Hao watu wanaishi kama kuku wa kufugwa. Wanatia huruma. Wamechotwa akili.

Sielewi kwa nini mamiioni ya watu waweze kuchotwa akili na familia moja namna hiyo.

Halafu eti jina rasmi la hiyo nchi ni DPRK (Democratic People's Republic of Korea).

Hivi wanafanyaga hata chaguzi hao watu?

Vichekesho!!

Ni dhambi kurithishana madaraka kwa watoto na vitukuu. Huyo jamaa hana akili kabisa....halafu kwa size na akili anafanana kabisa na prince wetu hapa...mbunge wa lile jimbo aliloliacha baba baada ya kuingia ofisi kubwa. naye anataka kuwa Rais..
 
Wa awamu ya kwanza.

Halafu kwa size na akili anafanana na prince wetu...the lawyer na mbunge. Unaonaje baba angemuachia madaraka kuendeleza maendeleo yaliyoletwa na awamu ya nne? Ya wizi mkubwa mkubwa wa mali za umma??!!
 
Wabongo mnajua kujudge vitu sana, but nchi yenu yenyewe inateketea, hamna maamuzi magumu

Mjiinga sana ni wewe "unayejua" wabongo waajjinga halafu unategemea wafanye mambo ya wenye akili. . . . . umekaa nyuma ya jogoo unasubiri atage!!!
 
Ni dhambi kurithishana madaraka kwa watoto na vitukuu. Huyo jamaa hana akili kabisa....halafu kwa size na akili anafanana kabisa na prince wetu hapa...mbunge wa lile jimbo aliloliacha baba baada ya kuingia ofisi kubwa. naye anataka kuwa Rais..

Kinadharia tete, ukipewa uchaguzi wa kuzaliwa Tanzania au Korea Kaskazini utachagua uzaliwe wapi?
 
Mkuu USA ndio ina mikwara kuhusu nuclear ya jamaa lakini hamna kitu.
Kama watu wanadhani ni mchezo US anzishe vita 21C aone kazi ya nuclear, alipiga watu enzi zile sio hizi zama za technolojia, utandawazi na biashara huria.

Unapanua panua mdomo hujui hata unachoongea
 
Wabongo mnajua kujudge vitu sana, but nchi yenu yenyewe inateketea, hamna maamuzi magumu

Kila taifa lina vyombo vyake vya kufanya maamuzi liwe limestawi au linadorola, kwahiyo hatuwezi kuacha kuangalia wenzetu wanafanya nini eti kisa hicho unachokiita wewe kuteketea, unataka wote tuingie ikulu, bungeni, nk haiwezekaniiiii
 
Wanawake jeshini wanalia kwa kumtaka, hawa sio wa kuwaambia mambo kama hayo.

article-2612058-1D4F55B600000578-641_964x757.jpg

Duh!, wadada wako all over him na kumlilia kabsa!,...ama kweli kama kwako kipofu kwa mwenzio kengeza!
 
Back
Top Bottom