Mzumbe Sec Waandamana

Mzumbe Sec Waandamana

Kusema ukweli Mzumbe ni moja ya shule yenye watu watulivu na upendo kuanzia kwa wanafunzi hadi walimu. Ni shule yenye nidhamu ya kipekee miongoni mwa shule za serikali. Kila mtu akifika pale mazingira yanambadilisha. Ukiona hali imefikia hapa ujue mambo yamefika ukomo.

Mazingira ya shule ni mabaya, maji machafu. Kipindi cha mvua hasa kuanzia April - June, kunakuwa na magonjwa ya mlipuko kama kuhara na ugonjwa maarufu mpaka ukatungiwa jina, Zongwe, au jina la kisayansi 'Zongwelisis Mzumbeata'. Ugonjwa huu uambatana na watu kuvimba usoni, na kuwashwa sehemu za siri.

Kwa wanafunzi na shule wao ni "Determination is Our Motto". Wao ni kitabu tu kwenda mbele despite the difficulties.

Majengo ya shule yapo toka mkoloni, makuukuu hakuna matengenezo. Naungana na wengine kuiomba serikali kusikiliza kilio cha Wanamzumbe. Mchango wa shule hii katika ujenzi wa taifa ni mkubwa hasa kwa kuzalisha madaktari, waandisi na wanasheria kabla ya miaka ya hivi karibuni vijana wake kubadilisha muelekeo na kupendelea fani za uchumi na biashara.

"Shule yetu Mzumbe Sekondari, yasifika kote Tanzania, malezi ya Mzumbe, elimu yake, ni kamilifu ya kitanzania, daima mbele nyumba mwiko"..nukuu ya maneno kutoka wimbo wa shule.
 
Jamani musiingize siasa kwenye hili, sio kila kitu ni siasa, kwa waliopitia mzumbe wanaweza kufahamu kwanini vijana wanataka kuboreshewa mazingira ambapo serikali inaonekana kama imesahau. Kwa mazingira ya Mzumbe na culture ya Mzumbe, ukiona hili, basi ujue wamezidiwa.

View attachment 95557

Picha ya bweni mojawapo, sijaonesha kwa ndani kwani inatisha zaidi.


Vipaji Maalum wanaishi kwenye uchafu huo. Mabweni hayo yalipigwa rangi mwaka 1991 Mwezi January enzi za Mwalimu Bagenda mpaka leo, vyooni je kukoje huko?? Serikali ndiyo pekee inayoua vipaji vya vijana hawa. What could you expect from Philip Mulugo the Failure???
 
Mkuu wanafunzi wa mzumbe sio type za kukimbia mtihani! Ni wanafunzi ambao wanatamani mitihan kila saa!

I have been there so niko sure na hili

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Hiyo unayoongea ni nadharia ambayo watu wasiosoma Mzumbe ndio hudhani hivyo.

Shule zina makundi tofauti tofauti.

Umesoma Mzumbe kipindi gani?

Unalijua kundi moja linaitwa MAVI? Hili ni kundi la wanafunzi wa Mzumbe, je hawa MAVI (kama unawajua) walikuwa hawakimbii mitihani?

Tabia sio lazima iwe ya wanafunzi wote, kikundi kidogo tu kinaweza kuharibu hali ya hewa. Na siamini kuwa wanaofanya harakati hizo ni shule nzima.

Mtoto mwenye kipaji maalum hawezi kuamua kuandamana mpaka Bungeni, kwa sababu angeweza kuona kuwa hiyo siyo solution ya matatizo ya Mzumbe. More importantly, mtoto mwenye kipaji maalum hawezi kuanzisha harakati kipindi cha mitihani ya kumaliza muhula. Hao wanaoandamana ni deviants.
 
Hapo hujaelezea maji wanayokunywa kutoka kule Mongwe Mlimani yakiwa na vinyesi, jamani!!!
 
Duh!

Yani nimekumbuka mbali sana,nlivyopangiwa mzumbe na kukuta mazingira ya special school kama yale

Kiukweli ile shule imesahaulika sana,yan hadi nyoka wanaingia mabwenini

Kibaka kuingia kuiba mabwenini ni jambo la kawaida sana

Kilichonisikitisha zaidi ni kusikia hilo jina la huyo headmaster?NJAWA?????????
Trust me huyo mwalimu hana uwezo wa kuongoza watoto wa mzumbe coz I'm sure wamemzidi uwezo wa kufikiri!yan huyo hata shule ya kata hawezi kuongoza!

Yani alikuwa mwalimu wa michezo enzi hizo!kiingereza chake sasa,duuuuuuh!!unaweza ukazimia!
*people are burning maize
*nowadays girls are grinding each other
Hizo ni baadhi tu ya sentens zake za kiingereza!

Kiukweli atakuwa yeye ndo ya kwanza kuharibu hiyo shule! Hana BUSARA kabisa

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Hiyo unayoongea ni nadharia ambayo watu wasiosoma Mzumbe ndio hudhani hivyo.

Shule zina makundi tofauti tofauti.

Umesoma Mzumbe kipindi gani?

Unalijua kundi moja linaitwa MAVI? Hili ni kundi la wanafunzi wa Mzumbe, je hawa MAVI (kama unawajua) walikuwa hawakimbii mitihani?

Tabia sio lazima iwe ya wanafunzi wote, kikundi kidogo tu kinaweza kuharibu hali ya hewa. Na siamini kuwa wanaofanya harakati hizo ni shule nzima.

Mtoto mwenye kipaji maalum hawezi kuamua kuandamana mpaka Bungeni, kwa sababu angeweza kuona kuwa hiyo siyo solution ya matatizo ya Mzumbe. More importantly, mtoto mwenye kipaji maalum hawezi kuanzisha harakati kipindi cha mitihani ya kumaliza muhula. Hao wanaoandamana ni deviants.

Mkuu, naomba ufikiri zaidi. Unafikiri kuitwa shule ya wanafunzi wenye vipaji maalum kuna halalisha serikali kutoijali shule hiyo? Walisema walimu ni WITO na wakatumia kigezo hicho kuwakandamiza walimu mpaka walimu walipokuja kushituka sasa hivi nao wanaipigia kelele serikali. Najua, Mkuu wewe huwa unaitetea serikali huenda una hisa zako huko, lakini muhimu utambue kuwa pamoja na vipaji lakini hao pia ni watu sawa na watu wengine, wote huhitaji yote ambayo wengine wanayapata. Mpaka wamefika hapo bila shaka wamechoka.
 
Mkuu, naomba ufikiri zaidi. Unafikiri kuitwa shule ya wanafunzi wenye vipaji maalum kuna halalisha serikali kutoijali shule hiyo? Walisema walimu ni WITO na wakatumia kigezo hicho kuwakandamiza walimu mpaka walimu walipokuja kushituka sasa hivi nao wanaipigia kelele serikali. Najua, Mkuu wewe huwa unaitetea serikali huenda una hisa zako huko, lakini muhimu utambue kuwa pamoja na vipaji lakini hao pia ni watu sawa na watu wengine, wote huhitaji yote ambayo wengine wanayapata. Mpaka wamefika hapo bila shaka wamechoka.

Tatizo mnaongea kiuanaharakati.

Hapo ulipo hujui mimi personally ninafanya jitihada gani kuhusu kuboresha Mzumbe. Kwa hiyo shutuma zako ziweke akiba kwanza.

Ukisoma vizuri na kuweka uanaharakati pembeni utaelewa ninachosema. Ila kama lengo lako ni kupindisha taarifa ili kuhalalisha uanaharakati basi endeleeni, lakini kuweki aware kuwa HAMTAFANIKIWA kwa njia mliyochagua.

Ninachosema ni hiki:
1. Matatizo ya miundombinu ni matatizo ya muda mrefu. Je, ni kwanini wanafunzi wamesubiri mpaka kipindi cha mitihani ndio waamue kuandamana?
2. Je, tathmini iliyofanywa na wanafunzi hao inaonyesha kuandamana kutawezesha vipi kutartua matatizo ya miundombinu?
3. Je, ni jitihada gani zimeshafanyika mpaka kufikia uamuzi huo wa kuandamana? Mwali Msuka wa Mzumbe aliwafundisha wanafunzi siku zote kwa ukifanya mambo kwa kufuata "right channel" utafanikiwa. Je, ni channel ipi mmefuata?

Hawa wanafunzi mimi ni wadogo zangu, na wewe kama ni miongoni mwao basi ni mdogo wangu na ni vema mkawa watlivu kusikiliza ushauri tunaowapa.

Mwanafunzi wa sekondari anatumia kati ya miaka 2 na 4 shuleni. Kwa kipindi hicho ni muhimu sana kubalance vipaumbele.
Kufanya maandamano kwa mguu mpaka Dodoma kwanza kunaashiria tatizo la fikra na pili inaashiria kushindwa kupanga vipaumbele ipasavyo. Kipindi cha mitihani ni kipindi maalum ambacho wanafunzi hata muda wao wa kula na kulala unategemewa kubadilika, huu sio muda wa kuandamana kwa matatizo chronic.
 
Vipaji Maalum wanaishi kwenye uchafu huo. Mabweni hayo yalipigwa rangi mwaka 1991 Mwezi January enzi za Mwalimu Bagenda mpaka leo, vyooni je kukoje huko?? Serikali ndiyo pekee inayoua vipaji vya vijana hawa. What could you expect from Philip Mulugo the Failure???



Nchi ya wasanii na hiyo bluu ni mojawapo ya sanaaaaa!

mbavu sina
 
Hata mwalimu Nyerere alitembea kwa mguu kwenda kuunga mkono azimio la arusha
 
kiukweli ni kuwa kitu ambacho serikali inafanya kwa shule kama mzumbe ambayo imetoa maprofessa, madaktari, wanasheria wachumi, maengeneer na viongozi wengi wa serikali kuwa katika hali kama ile tena shule ya vipaji maalum....is not fair
 
kiukweli ni kuwa kitu ambacho serikali inafanya kwa shule kama mzumbe ambayo imetoa maprofessa, madaktari, wanasheria wachumi, maengeneer na viongozi wengi wa serikali kuwa katika hali kama ile tena shule ya vipaji maalum....is not fair

Unachosema ni sahihi, lakini usiishie hapo. Unapaswa pia kuuliza hawa maprofesa, madaktari, wanasheria, wachumi na maengineer wameikumbuka vipi shule yao iliyowafikisha hapo walipo?

To the best of my knowledge ni kwamba ipo mikakati ya kuwahamasisha waliosoma Mzumbe kugive back to their school. Taarifa inatakapowafikia wale wote waliosoma Mzumbe basi let them do something to show that they care about their school.
 
Unachosema ni sahihi, lakini usiishie hapo. Unapaswa pia kuuliza hawa maprofesa, madaktari, wanasheria, wachumi na maengineer wameikumbuka vipi shule yao iliyowafikisha hapo walipo?

To the best of my knowledge ni kwamba ipo mikakati ya kuwahamasisha waliosoma Mzumbe kugive back to their school. Taarifa inatakapowafikia wale wote waliosoma Mzumbe basi let them do something to show that they care about their school.

Walimu na vingozi waliopo pale wawe wabunifu! Niko tayari kuchangia! Naamini kuna wengine wengi wanaopenda kufanya hivyo kama shukrani kwa kile tulichokipata maana ndicho kilichotufanya tuwe jinsi tulivyo!

Mazingira ya Mzumbe sio mazuri kwa nje ni kweli na ningetamani yabadilike, ila sijawahi na sitakaa nijute kupita pale!
 
Walimu na vingozi waliopo pale wawe wabunifu! Niko tayari kuchangia! Naamini kuna wengine wengi wanaopenda kufanya hivyo kama shukrani kwa kile tulichokipata maana ndicho kilichotufanya tuwe jinsi tulivyo!

Mazingira ya Mzumbe sio mazuri kwa nje ni kweli na ningetamani yabadilike, ila sijawahi na sitakaa nijute kupita pale!

Mkuu,

Lipo group la facebook la Mzumbe. Tafadhali jiunge kwenye kundi hilo ili upate updates za jitihada zinazoendelea.
 
lengo halikuwa kwenda Dodoma wala bungeni, walikuwa waende kwa Mkuu wa mkoa hawakufika. Chadema hawausiki kwa taarifa zilizopo mpaka sasa. They are special.
 
Dah umenikumbusha mbali sana!yani njawa mwalimu wa michezo hata kiingereza hajui we unategemea nini?!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Umenikumbusha mbali sana. Kaka yetu alienda kusoma PhD Uingereza akiambatana na familia. Aliporudi vitoto vyake vikawa vinaongea Kiingereza, mzee mmoja akaviangalia vile vitoto na mwisho akatoa ya moyoni akasema kwa kaka, "kweli Ulaya ni Ulaya, yaani hata vitoto vyako mmemaliza navyo PhD unayosema ulikuwa unasoma?" kaka alipokanusha fikra za yule mzee, yule mzee akasema mbona vinaongea lugha ya nyie wasomi?

Hapa leo naaminishwa kuwa msomi wa kweli lazima abomoke kizungu bila hivyo msomi huyo ni Njawa! Nafikiri ni vema tuache fikra potofu kama hizo.
 
Haikuwa kwenda bunge Dodoma, walikuwa waende mjini kwa mkuu wa mkoa, ukitoa taarifa hakikisha ni sahihi ucpotoshe umma. Mzumbe ni vipaji kwa hakika.
Siasa hazihusiki katika hili swala.
 
Back
Top Bottom