Tatizo mnaongea kiuanaharakati.
Hapo ulipo hujui mimi personally ninafanya jitihada gani kuhusu kuboresha Mzumbe. Kwa hiyo shutuma zako ziweke akiba kwanza.
Ukisoma vizuri na kuweka uanaharakati pembeni utaelewa ninachosema. Ila kama lengo lako ni kupindisha taarifa ili kuhalalisha uanaharakati basi endeleeni, lakini kuweki aware kuwa HAMTAFANIKIWA kwa njia mliyochagua.
Ninachosema ni hiki:
1. Matatizo ya miundombinu ni matatizo ya muda mrefu. Je, ni kwanini wanafunzi wamesubiri mpaka kipindi cha mitihani ndio waamue kuandamana?
2. Je, tathmini iliyofanywa na wanafunzi hao inaonyesha kuandamana kutawezesha vipi kutartua matatizo ya miundombinu?
3. Je, ni jitihada gani zimeshafanyika mpaka kufikia uamuzi huo wa kuandamana? Mwali Msuka wa Mzumbe aliwafundisha wanafunzi siku zote kwa ukifanya mambo kwa kufuata "right channel" utafanikiwa. Je, ni channel ipi mmefuata?
Hawa wanafunzi mimi ni wadogo zangu, na wewe kama ni miongoni mwao basi ni mdogo wangu na ni vema mkawa watlivu kusikiliza ushauri tunaowapa.
Mwanafunzi wa sekondari anatumia kati ya miaka 2 na 4 shuleni. Kwa kipindi hicho ni muhimu sana kubalance vipaumbele.
Kufanya maandamano kwa mguu mpaka Dodoma kwanza kunaashiria tatizo la fikra na pili inaashiria kushindwa kupanga vipaumbele ipasavyo. Kipindi cha mitihani ni kipindi maalum ambacho wanafunzi hata muda wao wa kula na kulala unategemewa kubadilika, huu sio muda wa kuandamana kwa matatizo chronic.
Hatujatofautiana, ninacho penda unielewe na ambacho hata wewe unakubaliana nacho ni kusahaulika shule hiyo kama zilivyosahaulika shule zingine ili hali mabilioni ya fedha yanafichwa Uswisi! Tofauti ya shule hii na shule zingine ni kwamba zingine zimejengwa baada ya Mzumbe enzi hizo ikiitwa Kichwere. Vijana wanaopita hapo wameonyesha jitiada ya kuwasikia walimu hata wakati fulani enzi za Mzee Mwasha (headmaster aliyemfuata Mzee Msuka) walipata kiburi wakadai kufanya vizuri katika mitihani kunatokana na juhudi zao wenyewe na si walimu!
Wanafunzi hawa si wa kwanza kuandamana na kuandamana si jambo jipya hapa nchini na nje ya nchi yetu. Kuandamana ni hatua ya mwisho inayochukuliwa na wahusika katika kufikisha ujumbe kwa ngazi nyingine na kwa jamii. Kama nawe una kiri kuwa Mzumbe kuna chronic problems, serikali iko wapi kuwaweka wanafunzi hao katika hali nzuri? Baada ya maandamano haya naomba uniamini, ujumbe umesogea na utaona kitu fulani kimefanyika shuleni hapo japo kitakuwa kidogo. Na sehemu zingine walikoandamana tuliona mabadiliko, na Mzumbe utaona yatakayotokea.
Labda nikuulize, kuna raha gani kufanya mitihani ili hali una matatizo? Mfano, pale Mzumbe pana wanafunzi 700 na wanafunzi hao wawapo darasani hutumia tundu moja la choo! Kuna wakati unakuta wamepanga foleni kwenda kujisaidia. Ni nini hiyo? Mitihani hiyo si ya taifa, inaweza kuahirishwa na hiyo haitakuwa mara ya kwanza. Tatua matatizo kwanza, mitihani baadae.
Unauliza kwanini hawajatoa madai hayo muda mrefu uliopita, hapa natamani ungeongea nao usikie kilio chao. Mpaka wamefika hapo hakika wametoka mbali kutoa madai yao. Lakini madai yao ni mengi na karibu yote yanahitaji fedha toka serikalini na serikali yetu nawe unajua hali yake kifedha. Na Mkuu wa shule Bw. Njawa hawezi kutoa mshahara wake ili atatue matatizo ya wanafunzi, jambo ambalo hata wewe usingeweza kulifanya. Ingawa katika hoja zako unadai una namna unayotaka kuisaidia Mzumbe. Naamini hutatoa mshahara wako kwani kwa mshahara wako kamwe huwezi kutatua matatizo yaliopo hapo.
Ushauri unapotolewa hupokelewa na si lazima utumike. Na udogo si kigezo cha kila utakachoshauriwa basi ukipokee tu. Na mimi si mwanafunzi wa Mzumbe Sekondari. Kiumri inawezekana nimekuzidi, mimi ni mtumishi wa serikali ninayehesabu miaka iliyobaki ili nisitaafu maana ndiyo michache na rahisi kuhesabu kuliko niliyotumikia nchi hii. Na si mwanaharakati, kama umeona kauli za kiuharakati; hiyo ni kwasababu ya maonezi hasa ya uongozi wa serikali yetu hasa ya sasa kwetu watumishi.
Aidha naomba nikueleweshe kuwa nimeongea na baadhi ya wanafunzi, walimu na wafanyakazi wasio walimu. Hakika Mzumbe ina matatizo makubwa lakini miongoni mwa madai ya wanafunzi ni ya kipuuzi mno. Mfano, tundu moja la choo lingeweza kutatuliwa na wanafunzi wenyewe. Kwa umri wao wangeweza kuchimba mashimo ya choo na wakaomba msaada aw serikali iwajengee sehemu itakayokuwa imebaki, hili sisi tulilifanya wakati tunasoma shule ya msingi na liliwezekana. Wanadai kile kitengo cha Mzumbe Book Project kiondoke kwa vile hakiwapi faida wao! madai Kama hiyo Mimi nimeyadharau bila kudharau maandamano yao.
Kama nimekukwaza, nisamehe sana Mkuu wangu