Mzumbe Sec Waandamana

Mzumbe Sec Waandamana

wanafunzi wa kipaji maalum mzumbe wameandamana wakielekea kwa mkuu wa mkoa ili kumuelezea matatizo yao ambayo yamekuwa yakipuuzwa na uongozi wa shule na hivyo kupelekea kufungwa kwa muda barabara Morogoro lringa kabla ya kuzuiwa na askari.source redio one breaking news
 
Na hili ndilo linalowawia vigumu ccm kuiongoza nchi kwani awali ilikuwa ikiongoza waoga na wajinga na sasa ni wasomi na wajanja mtaacha kutoka madarakani kweli?

Ni kweli kabisa Shine. Ukisikia "kusoma alama za nyakati" hapo ccm ndipo ilitakiwa kuelewa na pengine badala ya kueneza propaganda dhidi ya vyama vya upinzani ingekuwa vema waanze kujipanga kukabdhi nchi kwa wenye uwezo bila kuleta matatizo nchini mwetu kama alivyofanya Mbeki kule SA.
 
Na hili ndilo linalowawia vigumu ccm kuiongoza nchi kwani awali ilikuwa ikiongoza waoga na wajinga na sasa ni wasomi na wajanja mtaacha kutoka madarakani kweli?
Mkuu habari ya asubuhi!ngojanikusalimu kwa salamu hii ,kidumu chama tawala na zidumu fikra za mwenyekiti daktari
 
Du embu tusikie baadae wangapi watadondokewa na vitu vyenye ncha kali

Katika hili sidhani kama litatokea maana nawaona wanafunzi ni watulivu kupita kiasi. Ila wakiwalazimisha jambo, hakika watarudi shule lakini lolote kama kuchoma shule, kupiga hasa headmaster wao, n.k. baada ya hapo linaweza kutokea. Tuombe serikali isikie kilio chao.
 
wanafunzi wa kipaji maalum mzumbe wameandamana wakielekea kwa mkuu wa mkoa ili kumuelezea matatizo yao ambayo yamekuwa yakipuuzwa na uongozi wa shule na hivyo kupelekea kufungwa kwa muda barabara Morogoro lringa kabla ya kuzuiwa na askari.source redio one breaking news

Endelea kufuatilia sakata hili, wale wanafunzi wamejigawa katika makundi na lengo lao si kwenda kwa Mkuu aw Mkoa bali Bungeni Dodoma. Na baadae utasikia malalamiko yao yamefika mjengoni maana wapo waliokamatwa na bila shaka wako ambao watafikisha ujumbe wao.
 
umepotoshwa mkuu walipanga kwenda kwa mkuu wa mkoa morogoro sio dodoma

Unafikiri kwa kupotosha napata faida yoyote? Mleta habari, niko katika jumuiya husika ingawa sifanyi kazi hapo. Unasikiliza sehemu ya ujanja wa wanafunzi hao kutoka redio one Dar na unaamini huku ukiniona mleta habari toka eneo la tukio napotosha watu na huniamini! Poa!
 
kwa aliyewahi fika ilboru,kwenye ubao wa matangazo,kuna picha za mzumbe alafu wameandika ''mazingira mabovu,taaluma bora tz'',,kwa hakika wana haki ya kuandamana kwani mzumbe panatisha wakuu sio ka ilboru,alafu mnataka adminstrators wa baadae wasiwe mafisadi,,
 
Unafikiri kwa kupotosha napata faida yoyote? Mleta habari, niko katika jumuiya husika ingawa sifanyi kazi hapo. Unasikiliza sehemu ya ujanja wa wanafunzi hao kutoka redio one Dar na unaamini huku ukiniona mleta habari toka eneo la tukio napotosha watu na huniamini! Poa!

ukweli utajulikana tu
 
Wengi watazimia njiani na wengine watakufa kama Benjamini wa azimio la Arusha,labda watembee kwa siku mbili au wapande magari.
 
Ni nyuma kidogo ya Kasanga, Maliasili. Matatizo yao ni mengi. Ujue shule ya Mzumbe ni ya siku nyingi, imechoka! Na Headmaster, Njawa, ni kijana na hana uwezo wa kuwavuta wakubwa huko serikalini ili waendelee kujali shule hiyo. Hivyo matatizo yaliopo Mzumbe ni makubwa kuliko umri wa huyo headmaster. Na serikali inataka kuziweka shule zote kuwa za kata kwa ukata! Inaumiza hata shule zake za wanafunzi wenye vipaji?! Bogus government!

Matatizo Mzumbe kweli yapo.

Nimeona picha za Mzumbe za hivi karibuni, hali si nzuri.

Hata hivyoi, bado sijaelewa uamuzi wa kwenda Bungeni umedhamiria vipi kutatua matatizo yaliyopo.

Je, ni kwanini wameamua kwenad leo? kwanini hawakwenda jana au kesho? Nategemea kusikia hatua mbalimbali zilozofuatwa mpaka kufikia uamuzi huo wa kwenda Bungeni.

Mara nyingi terminal exams zikikaribia kuna wanafunzia ambao wanabehave abnormally. Je, hiki ni kipindi cha mitihani ya muhula? If yes, kwanini harakati hizo zifanyike kipindi cha mitihani?
 
Jamani, Mzumbe imefikia hapo! Tatizo ni nini hasa? Uongozi? Siasa za sasa? Walimu? Siapati jibu maana niliwahi kufanya kazi hapo na kwa namna ninavyoifahamu Mzumbe Sekondari sikutegemea kama shule ile inaweza kufika ilipofika. Anyway, tuwaombee wote mambo yao yaishe salama maana kama wengine walivyosema hatuchelewi kusikia wanafunzi wengine wamedondokewa na vitu vizito!
 
Jamani musiingize siasa kwenye hili, sio kila kitu ni siasa, kwa waliopitia mzumbe wanaweza kufahamu kwanini vijana wanataka kuboreshewa mazingira ambapo serikali inaonekana kama imesahau. Kwa mazingira ya Mzumbe na culture ya Mzumbe, ukiona hili, basi ujue wamezidiwa.

970761_4335056153444_995427663_n.jpg

Picha ya bweni mojawapo, sijaonesha kwa ndani kwani inatisha zaidi.
 
Huyu ni mwanafunzi tu amepost kufurahisha keyboard, Mzumbe nayoijua mimi haina wanafunzi wasiofikiria ovyo kiasi hicho tena wote wakakubaliana kuandamana kwa mguu hadi Dodoma, hawatofika hata kama wangeanza kutembea asubuhi, labda kama wanaandamana kwenda kwa ofisi yoyote hapohapo Morogoro. Sijui watakua wamefanywa nini hadi kufikia hatua hii, mwaka huu tu nimeiacha Mzumbe ikiwatulivu na wanafunzi hua ni wabumilivu sana kila mtu ana muda wake, hiyo ndiyo Mzumbe nayoijua mimi.. Duh kazi kweli kweli kama hawa Wapole wamefikia hatua hiyo Sijui shule nyingine itakuaje
 
Shule yetu Mzumbe secondary...
Yasifika kote Tanzania,
Malezi ya Mzumbe,elimu yake,ni kamilifuu ya Kitanzania,daima mbele nyumaa mwiko.
Kwa juhudi pia na nidhamu,tutaendeleza sifa zake...
Naukumbuka vizuri huu wimbo wa shule yetu pendwa.
 
Shule yetu Mzumbe secondary...
Yasifika kote Tanzania,
Malezi ya Mzumbe,elimu yake,ni kamilifuu ya Kitanzania,daima mbele nyumaa mwiko.
Kwa juhudi pia na nidhamu,tutaendeleza sifa zake...
Naukumbuka vizuri huu wimbo wa shule yetu pendwa.

Dah umenikumbusha mbali sana!yani njawa mwalimu wa michezo hata kiingereza hajui we unategemea nini?!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Matatizo Mzumbe kweli yapo.

Nimeona picha za Mzumbe za hivi karibuni, hali si nzuri.

Hata hivyoi, bado sijaelewa uamuzi wa kwenda Bungeni umedhamiria vipi kutatua matatizo yaliyopo.

Je, ni kwanini wameamua kwenad leo? kwanini hawakwenda jana au kesho? Nategemea kusikia hatua mbalimbali zilozofuatwa mpaka kufikia uamuzi huo wa kwenda Bungeni.

Mara nyingi terminal exams zikikaribia kuna wanafunzia ambao wanabehave abnormally. Je, hiki ni kipindi cha mitihani ya muhula? If yes, kwanini harakati hizo zifanyike kipindi cha mitihani?

Mkuu wanafunzi wa mzumbe sio type za kukimbia mtihani! Ni wanafunzi ambao wanatamani mitihan kila saa!

I have been there so niko sure na hili

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom