Mzee wetu Askofu Zachary Kakobe yuko wapi?

Mzee wetu Askofu Zachary Kakobe yuko wapi?

BiancaEA

Member
Joined
Nov 23, 2025
Posts
41
Reaction score
80
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) jijini Dar es Salaam, Bishop Zachary Kakobe ni miongoni wa watu wenye umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania, kutokana na huduma zake za kiroho kama Mtumishi wa neno la Mungu.

Lakini si hivyo tu, Bishop Kakobe ni mmoja wa watu wenye ushawishi hasa kwa waumini wake na hata wale wasiokuwa waumini lakini wanapenda kumfuatilia.

Katika kumbukumbu mwaka 2010, Askofu Kakobe aliwahi kuingia kwenye mvutano mkali na Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) akipinga utekelezaji wa mradi wa kupitisha umeme wenye msongo mkubwa mbele ya Kanisa lake lililopo eneo la Lufungira-Mwenge jijini Dar es Salaam.

Si hivyo tu, Askofu Kakobe amewahi kukumbana na matukio mengi nje ya Injili kama;
- Kudai Serikali ya Tanganyika
-Kuhojiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
- Kushtakiwa kwa kesi madai ya ubadhirifu
-Kushawishi watu kukubaliana na chanjo ya Corona

Pamoja na hayo machache kuhusu Askofu Kakobe, katika kipindi hiki ambacho Tanzania inapitia misukosuko ya matukio mabaya kama utekeji, watu kupotea, kuingiliwa kwa uhuru wa kuabudu, ufisadi kushika hatamu, kukandamizwa kwa uhuru wa vyombo vya habari, utoaji maoni na waandamanaji kuuliwa hajawahi kusikika popote akizungumza aidha kuwa kutoa maoni yake au akikemea wala kuzungumzia lolote juu ya hayo na sio kawaida yake.

Kuna nini kinaendelea? hata asipoongelea kuhusu yanayoendelea hapa nchini basi hata Kanisani kwake tumsikie.
 
Wanasema anaandika vitabu waumini wake lakini ni mda hawajamuona wala kumsikia pia
 
Anakula pension take Ila hataki kuwa gen z kama wengine
IMG-20251205-WA0000.jpg
 
Yupo buza kwa mama kibonge anaandaa kitabu chake cha maisha ya utume kwa nyakati zile 1980's had 2015 ambapo mjamaa magufuli alipomvuruga

Kuhusu kanisa lake pale mwenge nimemuuliza anasema atalitolea ufafanuz juu ya hili
 
Yupo buza kwa mama kibonge anaandaa kitabu chake cha maisha ya utume kwa nyakati zile 1980's had 2015 ambapo mjamaa magufuli alipomvuruga

Kuhusu kanisa lake pale mwenge nimemuuliza anasema atalitolea ufafanuz juu ya hili
Buza kwa mama bonge ndipo anapoishi?,halafu mbona kuandika kitabu sio jambo la kumficha kiasi cha miaka yote hii, au ana jambo lingine?
 
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) jijini Dar es Salaam, Bishop Zachary Kakobe ni miongoni wa watu wenye umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania, kutokana na huduma zake za kiroho kama Mtumishi wa neno la Mungu.

Lakini si hivyo tu, Bishop Kakobe ni mmoja wa watu wenye ushawishi hasa kwa waumini wake na hata wale wasiokuwa waumini lakini wanapenda kumfuatilia.

Katika kumbukumbu mwaka 2010, Askofu Kakobe aliwahi kuingia kwenye mvutano mkali na Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) akipinga utekelezaji wa mradi wa kupitisha umeme wenye msongo mkubwa mbele ya Kanisa lake lililopo eneo la Lufungira-Mwenge jijini Dar es Salaam.

Si hivyo tu, Askofu Kakobe amewahi kukumbana na matukio mengi nje ya Injili kama;
- Kudai Serikali ya Tanganyika
-Kuhojiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
- Kushtakiwa kwa kesi madai ya ubadhirifu
-Kushawishi watu kukubaliana na chanjo ya Corona

Pamoja na hayo machache kuhusu Askofu Kakobe, katika kipindi hiki ambacho Tanzania inapitia misukosuko ya matukio mabaya kama utekeji, watu kupotea, kuingiliwa kwa uhuru wa kuabudu, ufisadi kushika hatamu, kukandamizwa kwa uhuru wa vyombo vya habari, utoaji maoni na waandamanaji kuuliwa hajawahi kusikika popote akizungumza aidha kuwa kutoa maoni yake au akikemea wala kuzungumzia lolote juu ya hayo na sio kawaida yake.

Kuna nini kinaendelea? hata asipoongelea kuhusu yanayoendelea hapa nchini basi hata Kanisani kwake tumsikie.
Halafu juzi kati nimemuota eti kawa fundi radio...mtihani sana,
 
Back
Top Bottom