Mzee wangu Kinana mbona kimya sana?

Mzee wangu Kinana mbona kimya sana?

EasyFit

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2011
Posts
1,269
Reaction score
1,082
Tangu kumalizika kwa uchaguzi wa serikali za mitaa sijawahi kumsikia mzee wangu huyu sijui amepatwa na masahibu gani. Tafadhali Kinana chama kinakutegemea jitokeze kifua mbele tumeshinda ingawa si kama tulivyotegemea, aliwahi kusema katibu mkuu wetu wa zamani Kolimba RIP kuwa "ushindi ni ushindi tu hata wa kura moja'.

Jitokeze bana tunataka mbinu zaidi ya kubeba matofali au umeridhika na ushindi wa 60%?
 
Mkuu Ccm imepigwa kinachowauma ni wingi wa kura walizopata UKAWA.
 
​Baada ya kupiga posho ya kuzunguka nchi nzima sasa yupo mbugani kwaajili ya ndovu
 
Ataongea nini Escrow inamhusu,yeye ndo alikuwa Mwenyekiti wa benki ya Stanbic yalipobebwa mabilioni ya Escrow Account kwa rumbesa na mifuko ya rambo;usishau pia kashfa ya uagizaji wa sukari ya magendo anakohusika yeye na Waziri Mkuu Pinda,stay tuned ngoma bado mbichi
 
Kote alikopita akiigiza filamu na Nape Matokeo ni kichefuchefu
 
dili hili limebuma amerudi kwenye tembo wake
 
Labda safari hii akabebe kifusi na kokoto labda wananchi watamuonea huluma,hii sarakasi yakubeba matofari na kuendesha baiskel zawatoto zimepita atuonyeshe kipaji zaidi
 
sisi kina gogo la shamba tulishamuambia Kinana mapema kwamba, ccm inayoifikiria yeye sio ccm ya Kikwete
 
Wamempa onyo....Haiwezekeni kusimanga na kukiaibisha chama na serikali yake hati 'hawafanyi kazi'....'kuna waziri mizigo'......Amekiri udhaifu wa chama chake na sasa ameamuliwa kukaa kimyaaa.....

Ukithubutu kukiri makosa ndani ya ccm imekula kwako....hata wakiua sema hawajaua, wakiiba sema hawajaiba, wakishindwa uchaguzi sema wameshinda uchaguzi.....ccm ilishakuwa kama mpinga Kristo....you must go against every fact in its politics.
 
Na yule mwenzake, kijana wa mzee Moses Nnauye. Kushindwa kwa kishindo ni noma sana!
 
Ccm inasema kinana alicheza ngoma za upinzani wakati ule alipoizunguka nchi
 
Back
Top Bottom