Mzee Sumaye: Ukiwa na Bunge la chama kimoja unaruhusu Upinzani utoke ndani ya chama, hii ni mbaya zaidi

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,965
141,969
sumaye.jpg

Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye

Waziri Mkuu Mstaafu mzee Sumaye amesema Bunge la chama kimoja halina afya kwa maendeleo ya nchi na kwamba bunge la namna hiyo huifanya Serikali ilale usingizi.

Sumaye amesema unapoubana upinzani nje ya chama maana yake ni kuwa unakaribisha upinzani ndani ya chama ambao ndio mbaya na hatari zaidi.

Ni lazima CCM iwe na uvumilivu wa kisiasa ili iweze kulikuza taifa letu ambalo kimsingi ni moja.

Chanzo: Star tv
 
Hawa wazee wa ccm wamevurugwa kweli....Nyani haoni kundule...
Huyo anajua anachokiongea,hakuna mwana ccm waleo aliyejifunza kwa vitendo kutoka pande zote mbili kama yeye na pengine hata mwanaccm wakumpinga kwa anachowafundisha,atakaye fanya hivyo ni katika kulinda maslahi yake tu au ugali wake.
 
... matapeli tu hao! Juzi unautukana upinzani baada ya kupokelewa huko ulikopokelewa; leo unajifanya kuwaasa wale dhulumati waliokupokea kwamba upinzani ni kitu kizuri! Kama sio unafiki ni nini?
 
Mzee Sumaye kapoza maneno tu. Upinzani hautoki ndani ya chama tu bali utatoka kila upande ikiwemo ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama. Sijui hawa Viongozi wa CCM kuna yeyote aliye kaa akajiuliza nguvu za Lissu zilitoka wapi kwenye kampeni za uchaguzi 2020?
 
Back
Top Bottom