Mzee Mwinyi awachomekea kizenji!

*Huyu ndiye aliua Azimio la Arusha lililokuwa linawabana mafisadi.
*Ni mdini mkubwa aliyeweka pazia mbele yake asionekane.
*Hana ubavu wa kusimama kwenye mkutano wa hadhara kuhutubia haya maana hakuna atakayekubali upuuzi na undumila kuwili wake.
*Anaweza tu kuyasema haya kwa vijana hawa wadogo wasiomjua na hasa kwa watu wa dini fulani tu. maana hawa ndiyo umualika mara nyingi katika hafla zao.
 
Badala ya kuchangia pointi aliyoi raise mzee ruksa!, tunamjadili tena yeye mzee ruksa, mwanakijiji angetaka si angeanzisha thread ya utawala wa mzee ruksa bana, lakini theme ya thread hii ni kauli ya "watu kusoma bila kuelimika", je kuna ukweli/mantiki au uwongo katika kauli hiyo?. otherwise mtu sasa mtataka akae kimya tuuu, eti kwa sababu alikoseaga zamani katika uongozi wake.

waswahili wanasema bora nusu shari kuliko shari kamili hivi kweli utawala wa mzee ruksa ulikuwa balaa sana au?, hata kama Mzee ruksa alikoseaga huko zamani, hivi kweli hafai kutoa nasaha za kutoa mwongozo katika mambo fulani fulani?. hivi kweli utawala wa mzee ruksa ulikwenda kombo kiasi hicho?

Mbona wananchi wengi wa kawaida wanamkubali sana mzee ruksa?.
 
Swali kubwa ambalo linakuwa implied ni maneno ya Mwinyi ni kuwa Je wasomi ndio wametufikisha hapa tulipo leo hii? maana kama nin vyeti na CV zenye nyota nyota na maandishi bwelele si uongo wanazo.
 
waswahili wanasema bora nusu shari kuliko shari kamili hivi kweli utawala wa mzee ruksa ulikuwa balaa sana au?, hata kama Mzee ruksa alikoseaga huko zamani, hivi kweli hafai kutoa nasaha za kutoa mwongozo katika mambo fulani fulani?. hivi kweli utawala wa mzee ruksa ulikwenda kombo kiasi hicho?

Mbona wananchi wengi wa kawaida wanamkubali sana mzee ruksa?.


My take is ...kila regime imekuwa na vimbwanga vyake... sasa utakapolinganisha ndo utasema afadhali x kuliko y! na ndiyo hulka yetu wanadamu.Tunapenda kusema bora aliyetangulia kuliko wa sasa. Hujawahikusikia hata wanandoa wakisifia waliowaacha kwa mateke na magumi kuwa ni afadhali kuliko the new ones? Maisha ndivyo yalivyo..binadamu hana jema!
 
Mwanakijiji,
Mkuu kitu kikubwa hapa ni Kupata hao Viongozi waadilifu.
Binafsi bila maelezo ya Mwinyi naamini kabisa kwamba mtu yeyote aliyesoma na akaelemika iwe katika fani yoyote ile iwe sheria,Uchumi,dini na kadhalika ni lazima elimu yake itamsukuma kuwa MUADILIFU. Kutokuwa Muadilifu ni ishara toka ya mtu huyo kutoelemika..
Hata Mnyama hujifunza kutokana na makosa iwe sisi binadamu jamani! Duh, Bongo inatisha jamani!
 
Kwa mtaji wa sera na utawala wa SISIEM, ufisadi hautaisha ng'o. Ulikuwepo tangia awamu ya kwanza na utaendelea milele!!!!!!!

Asije mtu akajifanya kuna awamu yake iliyokuwa takatifu hapa!!!!
 
Anataka kutuambia kuwa yeye hakusoma lkn alielimika ndio maana uongozi wake ulikua "BORA??" zaidi
 
mafisadi wote wanaongara kipindi hiki walilelewa kipindi chake cha uongozi. Aliacha mwanya ndio wanaufuata.
 
Kwa mzee Mwinyi kusema hayo maneno hana kosa lolote, kwangu mimi hata Lowassa, Chenge, na Rostam leo hiii wakiibuka na kuanza kukemea ufisadi, hawatapaswa kubezwa bali kuungwa mkono na kufuatiliwa nyendo zao ili wasirudi walikokua. Kama kuna ushahidi wa dhahiri wa mambo aliyoyafanya Mwinyi si tatizo yakaja kwa mkondo wake na kujadiliwa na haya aliyoyasema yasizimwe kwa kutumia mambo yaliyofanyika siku za nyuma. Kuna watu wana tuhuma zilizowakabili kama Dk. HAssy Kitine, Dk. Ngasongwa, Iddi Simba, Mporogomy, Mbilinyi na wengine wengi, ambao leo hii wakizungumza mambo mazuri kutuunga mkono katika vita ya ufisadi, tusiwazibe midomo. Tukiwaziba midomo tutakua tunataka kusema elimu dhidi ya ufisadi iwalenge watoto wanaozaliwa na viongozi mafisadi hawastahili kubadilika na kujiunga katika jeshi letu. Jambo la msingi ni kuwangalia kwa makini wasije kutuzuga ama kuja upande wetu kutimiza malengo yao ili wakiingia tena WATUMALIZE kwa kutorudia makosa ya kuacha mambo yao yajulikane. Tuwape nafasi sawa na kampeni za Mrema alipokuwa Waziri kuwataka Majambazi wajisalimishe.

Kuna msomi mmoja amependekeza kuwe na Tume ya Upatanishi ili mafisadi wajiunge katika kundi letu kwani pamoja na ufisadi wao, kuna mambo ambayo wanayaweza na yanahitajika kusukuma gurudumu letu la maendeleo.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WALAANI MAFISADI
 
Tanzania Daima

RAIS mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, amesema kukithiri kwa rushwa na ufisadi serikalini kunatokana na kuwa na viongozi waliosoma, lakini hawakuelimika.

Mwinyi alitoa kauli hiyo jana wakati wa sherehe za mahafali ya kidato cha nne na sita kwa wanafunzi wa Shule ya Kiislamu ya Markaz, iliyopo Chang'ombe, Dar es salaam.

"Kuna matatizo makubwa ya uongozi katika nchi yetu. Tumevamiwa na maovu mengi, ujambazi wa kutumia nguvu, uongo, ulaghai na ujanja. Karibu kila sekta ya maendeleo ya jamii inakabiliwa na tatizo la kukosa viongozi waadilifu. Kuna matatizo ya uongozi katika mpira, taasisi mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

"Na haya tunayoyasoma na kuyasikia kwenye vyombo vya habari kuhusu kukithiri kwa maovu serikalini, yanatokana na kuwa na viongozi ambao wamesoma lakini hawakuelimika. Wangeelimika wasingelitenda haya tunayoyashuhudia na kuyasikia leo," alisema.

Alisema viongozi waliosoma na kuelimika ni waadilifu kwa sababu elimu ni nguvu ya ajabu ambayo mtu yeyote anayeipata humwingia ndani ya moyo wake na kumbadilisha kitabia.

"Viongozi walioelimika ni waadilifu, wana msimamo, huruma, ubinadamu, wenye upendo kwa wanaowaongoza kama wanavyojipenda wao," alibainisha mzee Mwinyi.

Kutokana na hali hiyo, Mwinyi aliwasihi wahitimu hao kuongeza bidii katika masomo yao ya juu ili waweze kuelimika vizuri na kuziba pengo la uongozi lililopo sasa nchini kwa kulitumikia taifa kwa uadilifu mkubwa.

Akizungumzia umuhimu na faida za elimu, Mwinyi alisema elimu humsaidia mtu aliyeipata kumudu mambo ambayo awali hakuyaweza na hivyo kuweza kuboresha maisha yake.

Alibainisha kuwa ujinga ni adui namba moja wa kila jamii, kwani maadui wengine kama umaskini na maradhi hutokana kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa elimu.

"Tuna maadui watatu nchini - ujinga, umaskini na maradhi. Hata hivyo, mimi naamini ujinga ndiyo adui mkubwa na naweza kusema kuwa ni mama wa adui wengine wote, lazima tupigane vita vya jihadi kumtokomeza adui ujinga," alisema.

Alisema elimu ni safari ndefu ambayo mtu huianza mara tu anapozaliwa na inakoma pale anapofariki dunia.

Mwinyi aliwashauri wahitimu kusoma kwa bidii elimu zote, elimu ya duniani na ile ya dini na kutoitelekeza elimu ya dunia kwa sababu elimu hiyo ni muhimu mno kwa maisha ya bora ya duniani.

Kauli ya Mwinyi kuhusu viongozi wa umma kukosa uadilifu, imekuja wakati viongozi wengi serikalini wakikabiliwa na tuhuma mbalimbali za ulaji rushwa na ufisadi, wakati baadhi yao wamelazimika kujiuzulu uongozi.

My Take:
Kwanini Mzee Mwinyi naye asipate nafasi kama aliyopata Mwalimu Mei Mosi Mbeya ya kuhutubia Taifa? Hakuna kasherehe kakitaifa ambako Mzee wetu angeweza kuzungumzia masuala muhimu yanayolikabili Taifa hadi tumsikie anazungumzie pembezoni? Kama kuna mtu anahutuba yake hiyo ni vizuri tungeipata.

NB: Kuchomekea kizenji: NI kutuma ujumbe mzito kwa kucheza na lugha kama alivyo fanya mzee Mwinyi "kusoma na kuelemika". M.M. Original

Mzee Mwanakijiji wewe unaakili sana, hili neno limetumika sehemu muafaka sana. MAANA HII KABONYEZA KWELI KIZENJE MPK KAPITILIZA KIPEMBA lakini ninavyowakubali MAFISADI wala ndio kwanza wanaendelea "KUKAMUA NDAMA"
 
Raisi mstaafu Mwinyi hana jipya:
Matamshi ya raisi mstaafu Mwinyi kwamba rushwa na ufisadi ni kutokana na viongozi waliosoma lakini hawajaelimika ni upuuzi mtupu.

Hata mtoto mdogo anajuwa kwamba rushwa na ufisadi unaoshamiri sasa ni kutokana na uongozi mbovu wa ccm chama tawala ambacho kinawakumbatia mafisadi na wezi. CCM ikimuiona MTU ANAFEDHA INAMKUMBATIA na hata kumpa uongozi hata kama hastahili. Mfano walipomuona mama Rwakatare ana mahela mara moja wakampa ubunge, walpomuona RA ana mihela wakampa uongozi wa chama ili waweze kuyapata mahela yao. Mzee Mwinyi pumzika tusije tukakuanzishia mambo yako wewe na familia yako mliyoyafanya wakati wa utawala wako. Je, hujui uregevu wako ndio uluiosababisha nchi kudumaa kimaendeleo kutokana na sera zako za kijinga za ruksa. Tafadhali funga mdomo wako.
 
Na pia kumwachia Capt. Azizi mtoroshaji mwingine wa dhahabu ati kisa mamke Capt Aziz alimfuata na kumlilia Rais.

"Watanzania Si Mabwege Tena" Mh. Dk. Mwakyembe, MB (Kyela)

Ibrah rais anayo mamlaka ya kumwachia yoyote anytime...reasons aliyoitoa pia si mbaya..kaonesha Huruma kama mzazi!!!

So far Mwalim Alimwamchia Padri Huru kwa......tafuta hio ilikuwaje....
 
Kwa haya umesema ukweli. Umesahau kusema ni mdini wa ajabu ambaye kwa kujificha unaweza kudhani siye.

Wewe si mchukia ufisadi...wewe ni mpenda ufisadi...Nani mwenye UDINI? Mwinyi udini huo aliitetea DINI gani?...

Mngepata wapi kumuona Mungu wenu papa John Paul? mbona wakati wa Nyerere Hakufika? kaja wakati wa Mwinyi?

Mngepata wapi kuuza KITIMOTO Hovyo? kama vitisho mlivyokuwa mkimpa mzee Mwinyi? Hadi asili ya neno Rukhsa lilikuja kwajili ya kuwaruhusu wala Nguruwe wale kwa starehe zao?

UDINI wa Mwinyi ni upi? wa Kumpa Mamlaka Marehem Malima ktk Wizara ya Elimu na kutoa siri zenu za kuwadhulumu waislam?
 
chimbuko la ufisadi lilianzia kwake baada ya kukubali kulizika azimio la arusha sasa anatutonesha vidonda. kwanini na yeye tusimweke kwenye list ya akina NKAPA??

Wewe Jiwe lilokufa....Azimio la Arusha la kuwadhulumu watu nyumba zao waliochuma Kihalali?...Wewe ulizaliwa lini? Shida alizowakuta nazo Mzee Mwinyi wananchi wa Tanzania wazijua?....
 
kweli kabisa na ni mtu hatari sana huyu na hatosheki hivi sasa amempeleka mwanawe huko Zanzibar ili awe rais hatosheki na fitna zake.Tunamshukuru marehemu rais Abduli Wakil baada ya kuwachia huru wale yeye Mwinyi alitaka wadhibiwe adhabu kali kwenye maandamano ya Sofia Kawawa huyu Mwinyi ni mnafik mzandik
 
Date::10/20/2008
Mwinyi aonya mafisadi wataangamiza taifa

Na Patricia Kimelemeta, Bagamoyo
Mwananchi

RAIS mstaafu aliyeongoza serikali ya awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, amevunja ukimya baada ya kuibuka na kuonya kwamba, mafisadi ni watu hatari ambao wanapaswa kupigwa vita kabla ya kulipeleka taifa kubaya.

Mbali na kukemea dhidi ya ufisadi, rais huyo aliyeongoza nchi kuanzia mwaka 1985 hadi 1995, pia alieleza tabia ambazo zinawafanya mafisadi kutambulika kirahisi.

Kauli hiyo ya Mwinyi maarufu kama Mzee Ruksa imekuja wakati nchi ikitikiswa na kashfa za ufisadi, huku mamlaka husika zikionekana kusita kuchukua hatua ama kutoa ahueni.

Mwinyi hakutaja ufisadi ambao alikuwa akiukemea, lakini miongoni mwa kashfa za ufisadi zilizotikisa nchi ni pamoja na utoaji wa zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa Kampuni ya Richmond, uchotaji wa fedha kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) na ununuzi wa rada.

Mwinyi, kiongozi mtaratibu ambaye ana silka ya upole, jana alikuwa tofauti alipoamua kukemea ufisadi wakati akizindua Shule ya Sekondari ya Ali Hassan Mwinyi (AHMES).

Rais huyo wa zamani wa Zanzibar alisema tatizo hilo kwa sasa linapigiwa kelele na kulaaniwa duniani kote.

Huku akionekana kutosema bayana na akionekana dhahiri kuchukizwa na mafisadi, Mzee Mwinyi alisema watu wa namna hiyo sio wema na hawafai kwa sababu wamekosa heshima na wana uwezo wa kumponza mtu kwa kuonekana hafai kumbe chanzo ni wao.

"Jamii inapaswa kukemea vitendo hivyo kwa kuwalea watoto wao katika mzingira mazuri na ya kuridhisha, ili wasiweze kuiga tabia ya watu wa aina hiyo (mafisadi)," alionya Mwinyi.

Mwinyi alisema kila kona duniani watu wanalalamikia vitendo vya ufisadi kwa sababu havifai na vinarudisha nyuma maendeleo ya nchi na kutaka vikemewe, ili watoto wasiweze kuiga kwa sababu vinaweza kulipeleka taifa kubaya.

Rais huyo wa awamu ya tatu alisema mafisadi wengi wanajifanya wamesoma, wataalam na wajuzi wa mambo kuliko wenzao kwa kuwa wao wana elimu ya kutosha na ni wajanja, kwa sababu wana uwezo wa kuamua jambo bila ya kushirikisha viongozi wenzao, kumbe ni watu wenye utovu wa nidhamu na wasio na heshima kwa viongozi wao na jamii kwa ujumla.

“Ukiwaangalia mafisadi wengi nchini, wanajifanya wamesoma halafu wajanja, wajuzi wa mambo na wanajua kila kitu ambacho wewe hukijui, kumbe hakuna kitu chochote zaidi ya dharau, jeuri, ukaidi na utovu wa nidhamu, uliowazunguka viongozi wao hadi familia zao,” alisema Rais Mwinyi.

Alisema tabia nzuri huigwa na kila mtu, lakini vitendo vya ufisadi havipaswi kuigwa au hata kumfundisha mtoto wako kwa sababu haifai na kutaka wazazi na walezi wawajengee heshima watoto wao tangu wadogo, ili wasiige tabia kama hiyo.

Rais huyo mstaafu alisema ikiwa kila mzazi atachukia ufisadi, jambo la kwanza kufanya ni kufundisha watoto wake nidhamu na heshima ili aweze kujiwekea misingi mizuri ya maisha.

Mwinyi, ambaye aliongoza serikali iliyofanya mageuzi ya kisiasa na kiuchumi, aliunganisha ufisadi na wizi wa mitihani uliokithiri mwaka huu kiasi cha mtihani wa somo la hesabu kufutwa hadi Jumatatu ijayo, alisema vitendo hivyo vya wizi vinatokana na utovu wa nidhamu unaofanywa na baadhi ya wanafunzi hao.

“Kuiba mitihani ni sawa na ufisadi... mwanafunzi wa aina hiyo ana nidhamu na anashindwa kutumia akili yake ya kuzaliwa kwa kusoma vitabu ili aweze kufaulu kwa kutumia uwezo wa akili yake. Anataka kurahisisha safari ya elimu, hafai tena anapaswa kukemewa kwa sababu taifa linaweza kupata viongozi wadanganyifu na wasio na elimu,” alionya.

Alisema ili mtu upate elimu bora, ni lazima uwe na nidhamu ambayo itakuwezesha kutumia umahiri wako kwa kusoma na kutafuta njia mbadala ya halali, ambayo utaona inaweza kukuletea mafanikio katika elimu na si kughushi vyeti.

Mwinyi pia alisifia mpango wa serikali kujenga shule nyingi za sekondari katika kila kata akisema una lengo la kuboresha sekta ya elimu nchini.

Alisema ikiwa watajenga shule hizo na kutoa elimu bora kwa wanafunzi wake, kiwango cha kufaulu kitaongezeka kwa kuwa watoto watapata elimu bora na sio bora elimu.

"Tunajenga shule kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu nchini. Tutahakikisha kuwa watoto wanapata elimu bora ambayo itawasaidia katika maisha yao," alisema.

Kauli hiyo ya mzee Mwinyi, imekuja baada ya kimya chake cha muda mrefu katika kuzungumzia mambo mbalimbali nyeti na mazito katika nchi.

Kabla ya kifo chake hapo Oktoba 14, 1999, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alikuwa akionya hatari mbalimbali katika nchi, ikiwemo rushwa na kuvunjika kwa umoja wa kitaifa.
 
Naona taratiiiib, waume wameanza kujitenga na kinyesi kilicho juu ya meza.




.
 
Back
Top Bottom