Mzee Kikwete aweka rekodi sawa, Uchumi wa Kati waliopanga na Mkapa ni wastani wa dola 3,000 kila Mtanzania

Wewe ni utopolo
 
Wewe ni utopolo
Onyesha 'utopolo' wangu uko wapi. Nimekutajia vigezo vilivyopo, nani aliyeviweka na nani alivitaja mintarafu Tanzania. Bado unaniita 'utopolo', neno ambalo wala sijui maana yake ingawa nahisi linaashiria uduni, ujinga, upumbavu, n.k. Kwa kushindwa kwako kujadili hoja zangu na badala yake unakimbilia kutukana, hudhani kama dhihaka hizo zinakufaa wewe mwenyewe kuliko mimi?
 
Uchumi upi utakaoimarika kwa kuwekeza reli ambayo inaelekea kusiko na mzigo wowote wa maana? ratio iliyopo ni 30% kwa central corridor vs 70% kwa njia ya Tanzam,kwa hesabu hizo unaona kuna uchumi gani utakua hapo?
Pili unawekeza kwenye umeme kwa matilioni afu umeme utakuwa iddle hautumiki,so far tuna umeme excess na uko cheapest kuliko Kenya na nchi nyingine za EAC lakini je wapi kuna wawekezaji wengi? tatizo sio uhaba wa umeme wala gharama bali masuala mengine ya kiurasimu ikiwemo sera zisizotabilika na kukandamizana kwenye makodi hovyo..Tungeweza kujenga bwawa 1 tu la let say mg 400 zingedumu miaka zaidi ya 15 ili mapesa mengine yakafanye mambo mengine badala ya kuwekeza mationi kwenye umeme wa mgwt 2000 lakini tunatumia nusu tu ya huo na mwingine utakuwa iddle kwa miaka mingi huku maintanance cost zikiwa palapale
Tatu miradi yote hiyo pamoja na kuwa haina tija sasa wala baadae inagharamiwa kwa zaidi ya 60% kwa mikopo ya kibiashara sasa huoni kila awamu watanzania watakuwa wanaumia kwa kukosa focus nzuri ya kuwekeza pesa? maana awamu hii imekopa pesa nyingi haijawahi tokea kiasi kwamba awamu ijayo itakua kulipa madeni tu,kumbuka mkapa alipata nafuu ya msamaha wa madeni ndio uchumi ukaanza kufufuka sasa huyu anaturudisha kulekule kwa kukosa strategic thinking na proper allocation of resources
 

Hayo maneno ya Mh. Kikwete ni propoganda. Sasa hiyo programu anayosema ambayo haikuandikwa popote wala kutangazwa popote na wala haiko kwenye ilani yoyote ya CCM ila tu iko kichwani mwa mtu itaaminiwa vipi?. Na bahati mbaya anasema alipanga na mtu ambaye hawezi kuhakikisha kwa sababu ni marehemu. Kikwete hapo amebujiiii
 

Au nae ni msaliti!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…