Sijijui
JF-Expert Member
- Jan 14, 2018
- 7,879
- 8,800
Wewe ni utopoloMada inalenga kukebehi Serikali ya sasa kwa kumkariri Kikwete kana kwamba amekanusha yanayosemwa na Serikali. Mada inapotosha aliyoyasema Kikwete kuhusu mafanikio ya Serikali ya sasa ambayo wewe unayaita 'propaganda', kwa kumsingizia kwamba amekanusha yanayosemwa na Serikali. Ukweli wa mambo ni kama ifuatavyo.
Pato la wastani wa chini ya USD 1,000 huhesabiwa kuwa Low Income. Kuanzia USD 1,000 hadi USD 3,000 ni Middle Income; na juu ya hapo ni High Income. Ukiisha vuka USD 1,000 unaingia Lower Middle Income na ukikaribia kiwango cha juu cha USD 3,000 unahesabiwa kuwa kwenye Upper Middle Income. Malengo ya Serikali, tangu wakati wa Kikwete, yalikuwa kwamba ifikapo mwaka 2025 mosi, Tanzania iingie uchumi wa kati, yaani kuwe na pato la wastani wa zaidi ya USD 1,000; na pili, kipato cha wastani kiwe takriban USD 3,000.
Serikali ya Magufuli imefikia lengo la kwanza mwaka huu, ikiwa ni miaka mitano kabla ya tarehe iliyopangwa. Hatua hii ilitangazwa na World Bank yenyewe. Ni dhahiri kwamba mada yako inapotosha ukweli kwa kusema Kikwete amekanusha 'propaganda' za Serikali. Hakuna lo lote alilokanusha Kikwete. Yeye ameishia kutaja lengo la tangu Serikali yake ya kufikia uchumi wa kati mwaka 2025. Serikali ya Magufuli imefanikisha hilo miaka mitano mbele na hilo likatangazwa na World Bank yenyewe. Hakuna cha propaganda hapo. Serikali iliendelea kusema kwamba kipato cha wastani, kufuatana na World Bank, ni USD 1,038. Wewe unamkariri Kikwete kwamba amesema Serikali inadanganya kwa kusema kiwango cha wastani ni USD 3,000. Serikali haijtamka hivyo. Mtu ambaye hakusikiliza hotuba ya Kikwete ataamini kwamba uyasemayo ni ukweli, ambapo si kweli. Tusubiri tuone kama lengo la pili la wastani wa mapato litafikiwa hapo mwaka 2025. Kwa kuangalia kasi iliyofikiwa katika miaka mitano tunayoimalizia, bila shaka lengo hilo litafikiwa pia. Mungu ibariki Tanzania na utulinde na habari potofu zinazoweza kuwaghafirisha wananchi.