Mzazi asiyejielewa ndiye atampeleka mtoto wake Pre-form one

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Mar 11, 2020
2,705
6,503
Kwa mzazi ambaye kichwa kina chaji hawezi ruhusu huu uhuni, hii inawezekana kwa wazazi wapumbavu pekee, ambao kiwango cha kuwaza ni zero.

Mtoto kasoma miaka 7 sasa kamaliza shule, huyu hapumziki, anaunganishwa aanze kitu kinaitwa Pre-form one, atapigishwa Pre-form one hadi December then January aanze shule.

Na wazazi wengi tulivyo wapumbavu tunaona ndio njia sasa ya kumfanya mtoto aje kuwa kama Elon Musk wa Tesla au Mark Zuckerberg wa Facebook na Whatsapp. Yaani njia ya kumfanya mtoto aweze hata kuvumbua chombo cha kwanza cha Tanzania kwenda Mwezini ni kumpelekea Pre- form one.

Watoto hawana muda wa kupumzisha akili, na hii njia za Pre-form one ni njia za Wazazi kukwepa majukumu, Wazazi wa Kiafrika hawataki kukaa na watoto wao hata kuwafundisha elimu ya Duniani, kumfundisha maisha.

Wahindi sio wajinga kwenda na Watoto wao wa miaka 6 Dukani au Offisini kwao.

Ila sisi Wabongo tunaofanya Biashara eti hatutaki kwenda na Watoto wetu kwenye maeneo ya Biashara angalau waangalie kile tunachofanya, tunadanganywa na wahuni kwamba watoto wanapaswa kwenda Pre-form one kujifunza.

Ni vitu gani wanajifunza huko Pre-form one ambavyo hawatajifunza Sekondari?
 
Mtoa mada ni kama ulikuwa katika kichwa changu.

Mtoto kapigika mwaka mzima kwa maandalizi ya darasa la saba (Ni kupigika maana walikuwa wana force waende shule siku 7 za wiki zote kwa miezi 9 mfululizo).
Kamaliza mitihani tu unamtupa pre form one akasome masomo ambayo atarudia kufundishwa akiingia form 1.

Na kiuhalisia hakuna anachofundishwa zaidi ya English course.

Wamiliki wa vi tuition uchwara vya pre form one watakuja kukushukia kama mwewe, jiandae. Maana hapa unahatarisha maandalizi yao ya xmass.
 
Na wazazi wengi tulivyo wapumbavu tunaona ndio njia sasa ya kumfanya mtoto aje kuwa kama Elon Musk wa Tesla au Mark Zuckerberg wa Facebook na Whatsapp.Yaani njia ya kumfanya mtoto aweze hata kuvumbua chombo cha kwanza cha Tanzania kwenda Mwezini ni kumpelekea Prform one.
Stop these sweeping statements. Tell this nonsense to your own self not inclusive of others.
 
Hiyo kuwaita wapumbavu ilikua na ulazima gani?.kwasababu ungeweza kutoa hoja yako vizuri bila kuita wazazi wapumbavu.kwasababu kwenye haya maisha kila mtu anafanya kile anachokiona kinamfaa yeye na familia yake kutokana na uwezo alio nao.Kwahiyo hakuna sababu yakulazimishana kwenye jambo linalohusu uwezo wa mtu na maamuzi yake.Hoja yako ingekua na maana kama ungeileta kama ushauri/maoni badala ya dhihaka.
 
Na nadhan pia mtoto anakua hatarini. Wanawaacha wanavaa visurual kuna siku nilibak kushangaa vitoto vya pre form one vimevaa utafikir huko alipotoka kaachwaje. Uje beach sasa darasa ndio linahamia huko. Na imekua ni biashara tu watu wameona fursa.
 
Inaweza kuonekana kuwa ni mzaha lakini kiukweli safari ya elimu imegeuka kuwa mateso na kero kwa vijana wetu.......

Safari ya elimu imewapokonya haki na mazingira ya utoto vijana wetu kiasi kwamba......mtoto anakuwa bize na masomo mpaka anaona ni gereza........

Lakini kwa uchunguzi wangu nimegundua mateso hayo yapo kwa sisi wa hali ya chini lakini kwa wenzetu kidogo wanasoma kwa kurelax
 
Kwa mzazi ambaye kichwa kina chaji hawezi ruhusu huu uhuni, hii inawezekana kwa wazazi wapumbavu pekee, ambao kiwango cha kuwaza ni zero.

Mtoto kasoma miaka 7 sasa kamaliza shule, huyu hapumziki, anaunganishwa aanze kitu kinaitwa Preforma one, atapigishwa Preform one na wahuni hadi December then January aanze shule.

Na wazazi wengi tulivyo wapumbavu tunaona ndio njia sasa ya kumfanya mtoto aje kuwa kama Elon Musk wa Tesla au Mark Zuckerberg wa Facebook na Whatsapp.Yaani njia ya kumfanya mtoto aweze hata kuvumbua chombo cha kwanza cha Tanzania kwenda Mwezini ni kumpelekea Prform one.

Watoto hawana muda wa kupumzisha akili, na hii njia za Preform one ni njia za Wazazi kukwepa majukumua, Wazazi wa Kiafrica hawataki kukaa na watoto wao hata kuwafundisga elimu ya Duniani, kumfundisha maisha.

Wahindi sio wajinga kwenda na Watoto wao wa miaka 6 Dukani au Offisini kwao.

Ila sisi Wabongo tunao fanya Biashara eti hatutaki kwenda na Watoto wetu kwenye maeneo ya Biashara angalau waangalie kile tunacho fanya, tunadanganywa na wahuni kwamba watoto wanapaswa kwenda Preform one kujifunza.

Ni vitu gani wanajifunza huko Preform one ambavyo hawatajifunza Secondary?

Fanya unavyoona ni sawa, na wao wafanye wanavyoona ni sawa, miezi mi 3 ya mtoto teen kukaa nyumbani bila shughuli, bora pre form one.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom