Tanzania Nchi Yetu Sote
JF-Expert Member
- Mar 12, 2017
- 505
- 852
Dear walimu wa watoto wetu,
Wazazi wote wa wahitimu wa darasa la saba wako wanakimbizana kupata shule bora za watoto wetu. Na hii imekuwa biashara nzuri hasa kwa wenye shule.
Shule inatambua kabisa kuwa ina nafasi 120 za kidato cha kwanza, lakini inafanyisha usahili watoto 4,000.
Mnapata income ya watoto 4,000 kwa 30,000 sawa na mil 120. Alafu mnatoa matokeo baada ya siku mbili. Mmesahisha kwa umakini na kutoa majibu. Aksanteni sana.
Baada ya kupata hii cream bora kabisa, mnakuja kutuambia waje pre form one. Pre form one ya nini walimu wetu?
1. Sylabus ya form 1 imewekwa kwa mwaka 1, January to December. Kwa nini muda hautoshi?
2. Na sisi tulisoma, tena kayumba tulitumia miezi 4 ya kwanza kufanya English Course kabla ya kuanza masomo ya form one na tulimaliza vema kabisa.
3. Mmechukua cream kati ya watoto 4,000. Mna haraka gani kuwafanyia pre form one. Mngesema mnachukua watoto waliofeli na wasio na uwezo ndio mnawafanyia pre form one tungeona mna ukweli.
Sisi wazazi tunaruhusu huu utaratibu kuwa rasmi na kimsingi tunasahau kuwa hizi ni biashara za shule za private kuendelea kusumbua:
1. Watoto wanakosa kupumzika na kupata nafasi ya akili kupumua, mwisho wa siku tunapata wasomi waliochoka na hawana ari ya kazi
2. Wazazi wanalipa ada ya pre form one na form one baadaye. Ni hasara kwa wazazi kwa kuwa Hakuna hela ya kuchezea kwa sasa.
Imefika mahali shule zianze kuomba vibali vya kuendesha pre form one kwa watoto na iwe kwa ajili ya watoto wenye uwezo mdogo kama msaada na sio biashara ya kuingiza kipato kwa kuwachosha watoto na kutia hasara wazazi.
Mzazi mtazamaji
Pia soma: Waziri wa elimu tusaidie. Wazazi tunateseka.
Wazazi wote wa wahitimu wa darasa la saba wako wanakimbizana kupata shule bora za watoto wetu. Na hii imekuwa biashara nzuri hasa kwa wenye shule.
Shule inatambua kabisa kuwa ina nafasi 120 za kidato cha kwanza, lakini inafanyisha usahili watoto 4,000.
Mnapata income ya watoto 4,000 kwa 30,000 sawa na mil 120. Alafu mnatoa matokeo baada ya siku mbili. Mmesahisha kwa umakini na kutoa majibu. Aksanteni sana.
Baada ya kupata hii cream bora kabisa, mnakuja kutuambia waje pre form one. Pre form one ya nini walimu wetu?
1. Sylabus ya form 1 imewekwa kwa mwaka 1, January to December. Kwa nini muda hautoshi?
2. Na sisi tulisoma, tena kayumba tulitumia miezi 4 ya kwanza kufanya English Course kabla ya kuanza masomo ya form one na tulimaliza vema kabisa.
3. Mmechukua cream kati ya watoto 4,000. Mna haraka gani kuwafanyia pre form one. Mngesema mnachukua watoto waliofeli na wasio na uwezo ndio mnawafanyia pre form one tungeona mna ukweli.
Sisi wazazi tunaruhusu huu utaratibu kuwa rasmi na kimsingi tunasahau kuwa hizi ni biashara za shule za private kuendelea kusumbua:
1. Watoto wanakosa kupumzika na kupata nafasi ya akili kupumua, mwisho wa siku tunapata wasomi waliochoka na hawana ari ya kazi
2. Wazazi wanalipa ada ya pre form one na form one baadaye. Ni hasara kwa wazazi kwa kuwa Hakuna hela ya kuchezea kwa sasa.
Imefika mahali shule zianze kuomba vibali vya kuendesha pre form one kwa watoto na iwe kwa ajili ya watoto wenye uwezo mdogo kama msaada na sio biashara ya kuingiza kipato kwa kuwachosha watoto na kutia hasara wazazi.
Mzazi mtazamaji
Pia soma: Waziri wa elimu tusaidie. Wazazi tunateseka.