Inawezekana mzazi au mlezi wako hakuwahi kukaa na wewe akakupa elimu kwa kina juu ya tahadhari za kuzingatia hasa unapokuwa umevunja ungo, hili jambo wazazi / walezi wengi tunafeli sana.
Mtoto /watoto wanapokua ni vema kukaa nao na kuwaelimisha kwa kina sana juu ya mabadiliko ya ukuaji wa miili yao na utendaji wa viungo vyao vya uzazi.
Unakuta mzazi / mlezi unaogopeka kwa watoto kiasi ambacho hawawezi hata kuelezea shida zao. Mathalani mtoto wa kike anapovunja ungo anafikia hatua ya kujificha na kuficha hali hiyo kwa hisia kwamba ataonekana hafai ( kuvunja ungo / kubalehe ) sio dhambi ni jambo la kawaida kwa binadamu.
Mzazi anafanya kukisia kisia tu kwamba bintiye au kijana wake kakomaa, matokeo yake anabaki tu kumwelezea maneno ya vitisho kama vile; ukikutana na mwanaume utapata mimba (how??????.....mfafanulie mtoto aelewe kila kitu kwa uwazi) au ukitembea na mwanaume wazazi wako wanakufa (really!!!!!...... seriously!!!!!!!......)
Wazazi na walezi tuseme na watoto, ikishindikana tutumie hata marafiki zetu tunaowaamini.