Mwongozo Chadema baada ya uchaguzi mdogo

Wadau,

Vichwa vya habari vya baadhi magazeti ya leo vimewanukuu baadhi ya viongozi wa ccm wakikibeza cdm eti kwa ushindi finyu wa uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika hivi karibuni nchini. Nimesoma pia humu jamvini maoni ya watu ambao inawezekana ama ni wanachama wa cdm au viongozi wa cdm wakitoa maelezo yanayodhihirisha kukatishwa kwao tamaa na matokeo hayo. Kwanza nianze kwa keeleza jambo moja ambalo ni bayana kwamba kuking'oa chama tawala siyo kazi ya lelemama na muda mfupi kama wengi wetu tunavyodhani. Ni kazi nzito na inahitaji nguvu kubwa na yenye mabonde na milima mingi. Kwa hiyo, inahitaji uvumilivu mkubwa sana. Binafsi, nakishukuru sana cdm kwa kutuonyesha watanzania kuwa ni chama kilicho na dhamira ya dhati ya kumwondoa mkoloni wa pili ambaye ni ccm. Vyama vingine viliibuka kwa nguvu hiihii na sasa vinaelekea kaburini au tayari vipo kaburini.

Waswahili wanasema siku njema huonekana asubuhi. Matokeo ya chaguzi ndogo zilizofanyika nchini hadi sasa yanaashiria cdm ina-gain na ccm ina-lose. Ukichora graph ya ushindi wa ccm tangu mwaka 2005 bila shaka utabaini hiki ninachoandika hapa. Wakati upande huo wa ccm ukiwa hivyo, upande wa cdm unaendelea kuongeza ushindi yaani graph inapanda. Huo ndiyo ukweli na utaendelea kubaki kuwa ukweli.

Kwa wana ccm makini na wasomi kamwe hawawezi kufurahia matokeo ya kupoteza kata 4 na kuziacha ziende kwa wapinzani wao cdm. Hali kadhalika, kwa wana cdm makini na wasomi hawawezi kusikitika kupata ushindi kwenye kata chache ikilinganishwa na ccm wakati katika kata walizopata, 4 ni mpya.

Ndugu zangu wana cdm na wapenda mabadiliko, tafadhali msikate tamaa kabisa. Ushindi upo na endeleeni kuongeza bidii. Sumu iliyowekwa na ccm kwenye vichwa vya watanzania ni kali. Inahitaji utaalam na commitment ya hali ya juu kuiondoa na kuwakomboa watanzania.

Kama ulisoma paragraph ya kwanza katika mada yangu utagundua nimeongelea hicho unachokisema kwa kifupi sana kama ifuatavyo:
Uchaguzi mdogo wa madiwani ulikamilishwa na wapiga kura nchini Jumapili October 28, Chadema kimepata funzo kubwa lenye kutoa tafsiri kadhaa zenye kuleta matumaini kwa wenye moyo mkuu au kufifisha kwa wenye moyo mchache.
Wewe ni mmoja kati ya wenye moyo mkuu wa kutambua hayo, wengine wamekata tamaa na kusema wameshauri uongozi hawasikii sasa bai. Hayo sikubaliani nayo, siasa ni sayansi lazima kusoma upepo unavyokwenda na pia huhitaji muda kupata mang'amuzi katika nyanja hizi.

Mambo ambayo tunayaona kama yameweza kusababisha ndiyo tunayojadili hapa ili viongozi wahusika wayafanyie kazi. Kunyang'anya viti vilivyoshikwa na chama tawala si lelemama.
 
Daftari la wapiga kura ni moja kati ya sababu kuu! fikiri vizuri, Mangine umeongea sawa ila kunasehem umepotoka kiasi.

Viti ambavyo Chadema wameshinda hakukuwa na matatizo ya daftari la wapiga kura kama vituo ambavyo wameangukia pua? Nadhani sehemu walizoshinda Chadema walisimamisha wagombea wanaokubalika
 
Kuna tatizo kubwa katika kuteau wagombeaji,ieleweke wazi kuna watu wazuri wenye uwezo wa kugombea na kushinda lakini hawajitokezi,sababu haijulikani bado,ni wazi vilevile watu wanachagua mtu na sio chama,ccm walijitahidi kuteua watu wanaokubalika,hilo ndio tatizo kubwa

Eneo hilo la kuandaa wagombea wenye sifa ambao watakubalika kwa wapiga kura ndilo linalotakiwa kupewa kipaumbele na kufanya kampeni kali ya vijijini nyumba kwa nyuma na mtaa kwa mtaa pia kukiwa na mabalozi wa nyumba kumi ili kuweza kuhakiki vema wanachama.
 
Sitaki kuamini kama maneno haya yameandikwa na Candid scope.

Ni aibu kubwa sana kuandika vitu bila kufanya utafiti wa kina.

*Nitarudi kufafanua zaidi

Nathibitisha kwamba ni mimi Candid nimeandika, niko wazi, sina kigugumizi katika kuonyesha ukweli kwa nia njema ya kujenga mageuzi ya kweli. Mficha maradhi mwisho humwumbua. Bora tuwe transparent.
 
Umeona eeh......Magamba yanajua nguvu yao ya dola kuzuia M4C imestukiwa na ulimwengu mzima wanataka sasa kuja na ushauri nasaha ili ku-derail hii silaha muhimu ya CDM.

Inaonekana milango mingi kuingilia CDM imefungwa sasa naona wanatafuta madirisha ili waweze kuingia kwakuweka chambo.....Pamoja na mengine yote haiingii akilini kuleta hoja ya Katibu kulipwa mshahara kumbuka huyu analipwa ujira wake kwa kazi ailiyoifanya kwa CDM..

Si kuwa hao wengine si muhimu bali hata wao bila wale wa mwanzo kujitoa kafara leo hii wasigetamani kuwa one among CDM.....Huu ujamaa usiozingatia malipo halali ni hatari sana.

Ndiyo hasa kilichafanya CCM ikageuka kuwa ya mafisadi....Na kila mtu kuanza kuishi kiujanja badala ya kufanya kazi na kulipwa inavyostahili.....

Jamani njaa inaweza kusababisha matatizo mengi, walao kidogo kinasidia kuwajengea uvumilivu kwamba ipo siku mambo yatakamilika. Amini posho ni muhumu. Huenda wanapata, sijafanya utafiti wa kutosha kama wanapata au la. Hilo ni pendekezo langu kama hawapati basi kuwepo na utaratibu fulani utakaosadia nao kupata angalo kidogo cha kupangusa jasho wanalotaabikia.
 
Mleta mada acha kuishi kwa hisia bali kwa uhalisia.

*Ni ujinga mkubwa kubeza mafanikio madogo ya CHADEMA kupitia matokeo ya chaguzi hizi za udiwani bila kuangalia kwanza mwenendo mzima wa uendeshaji wa uchaguzi ulivyokuwa.

Hatujafikia kiwango cha kuanika matusi hapa, naoni ni mbalimbali, lete unayoona yanafaa kwani mimi nimeleta ya kwangu, na katika kujadiliana tutafikia mwafaka kwamba tuyapange vipi kwa kutangulizana kadiri ya umuhimu wa kwanza. Labda penye shaka kwa ustaarabu ulio nao ungeniuliza nitolee ufafanuzi na usiporidhika hapo unaweza kunieleza utelezi wangu.
 
Mbinu za Chadema kujitanua zibadilishwe kuendana na upepo unavyovuma.
Yale maandamano na mikutano ya hadhara inaonekana kutokuwa na nafasi kubwa kwa watanzania leo,​
Pendekezo kwa Chadema ni:


  • [*=1]Kuachana na maandamano kwani yanachelewesha watu kuwajibika katika kujenga uchumi wa nchi
Mkuu Candid Scope umeupackage ushauri wako kwa uongozi wa CDM kidiplomasia zaidi.
Fujo na kupimana ubavu na vyombo vya dola hakukiasidii chama chenu CDM.

Ushauri huu ungezingatiwa pengine Daudi Mwangosi angekuwa hai leo.
 
Ni aibu kubwa sana kuandika vitu bila kufanya utafiti wa kina.

*Nitarudi kufafanua zaidi......

Hata mimi imenistua sana......Its like this, let me expose them maana shetani hapendi mwanga anapenda giza zaidi..M4C imeleta damage kubwa sana kwenye magamba na hawana ubavu wakuendelea kutumia nguvu kubwa iliyodhahiri kuisitisha..Na inawezekana kabisa hata haya matokeo ya udiwani si ya kweli...Kwanini?

Walikuwa wanajua what they are after kwamba kisiasa kuonyesha jamii na CDM wenyewe hiyo M4C haijawa na impact kubwa kama wanavyodhani..Na kwakua hakuna data base ya huhakika Tz kutokana na mfumo mbaya wa governance..(Hata local government nyingi hazina socio-economic profile zao kujua who is who and where are they na ili kutengeneza hili si kazi ya siku moja na inahitaji resources) so wakajua inahitaji akili sana na intelligence syatem kwa CDM kung'amua hili then wamepanga usanii wao waki system na nje wanakuja kama washauri kumbe ndiyo wale wale...

Kwanini nasema haya kwasababu haiingii akili kwa true member wa CDM kuja na vitu public vya kuibomoa zaidi kuliko kuijenga..Tena hizo advice zi reflect kabisa matukio halisi....Ingekuwa inafanywa na watu in-experienced ningeelewa lakini wale wenye akili zao timamu na wenye uwezo wa ziada..CDM kumbukeni maneno ya Wasira......M4C ndiyo dawa pekee ya kuwafikishia elimu ya uraia watu wengi hasa wale ambao siyo elite maana wengi wako emotional na siyo rational..Then on top sasa mjitahidi kutafuta jinsi ya kuwa-retain kwa incentive based mechanisms ambayo wala si garama sana kama tutajipanga vizuri..Ni coordination tu inayohitajika wala si financial facility kubwa just a seed money.[/QUOTE]

Pole sana, mimi si member wa Chadema, ila tu ni mpenzi wa Chadema. Si mwanachama wa Chadema ila napenda movement zao na hata sera zao. Uwazi wazo na nguvu ya hoja waliyo nayo bungeni na uraiani. Samahani kama ulifikiri mimi ni mwanachama la hasha ila ni mpenzi chama.

Sipendi kuwa mwanachama wa chama cho chote cha siasa kwa sababu ya kutouruhusu utashi wangu kuwa na ushabiki wa rangi badala ya ukweli wa hali halisi. Ndio maana umeniona hata wabunge na wengine kutoka CCM wanaofanya vizuri naandika mada zao hapa na kuwapa sifa stahiki. Hapa JF walinipopoa mawe sana nilipoanza kuleta hoja za utendaji mzuri wa Filikunjombe na kupata tafsiri nyingi, lakini leo wengi wamekuja kutambua ukweli huo ingawa huyo mtu sijamtia hata machoni mwangu.

Siasa za vyama si uadui, kinachoshindaniwa ni njia ambayo kila chama inaona nibora zaidi katika kuongoza taifa kwa mafanikio. Chama chenye kuvutia wananchi wengi kwa sera zao ndicho kinachopewa jukumu. Sina chuki na CCM kwani wana sera nzuri sana ila viongozi ni ovyoooo! Utekelezaji wa sera ni ovyoooooo! Uozo na ubovu wa uongozi wa CCM vinatia kichefuchefu. Ndio maana wanafalsafa wanasema:
'Hachukiwi mtu ila matendo yake!'

JF tunatakiwa kuwa na upeo wa kuchambua mambo si kushabikia kama timu ya mpira. Kuchambua uwezo na udhaifu wa viongozi wa kisiasa ni haki yetu na ni njia ya kuwajenga. Hata nionane nao ana kwa ana nitafanya hivyo na watanielewa vema kuliko unavyonielewa wewe na baadhi ya wengine wanaopinga maoni yangu hapa.

Mambo ya zidumu fikra za mwenyekiti ndio hata akiteleza ni kupigia makofi tu na matokea ndio haya tunayolalamikia CCM kwa sababu pamoja na Kikwete kuvurunda huku Chama bado hakuna wa kumnyoshea kidole kama ANC walivyomwadabisha aliyemfuata Mandela.


Tunatakiwa tuwe great thinker, na katu siko tayari kufunika yale ambayo yanaweza kuhatarisha uhai wa chama tunachokitegemea kuwa mkombozi wetu wa kwali.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
... Kwanza nianze kwa keeleza jambo moja ambalo ni bayana kwamba kuking'oa chama tawala siyo kazi ya lelemama na muda mfupi kama wengi wetu tunavyodhani. Ni kazi nzito na inahitaji nguvu kubwa na yenye mabonde na milima mingi. Kwa hiyo, inahitaji uvumilivu mkubwa sana. Binafsi, nakishukuru sana cdm kwa kutuonyesha watanzania kuwa ni chama kilicho na dhamira ya dhati ya kumwondoa mkoloni wa pili ambaye ni ccm. Vyama vingine viliibuka kwa nguvu hiihii na sasa vinaelekea kaburini au tayari vipo kaburini.....

Wengi walifikiri CDM imeshafika, hivyo walitarajia ushindi wa kishindo tu kuanzia sasa. Wameshindwa hata kuiona hatua iliyopigwa hapo. Hatuna budi kuuona ukweli kwamba watanzania wengi bado sana kuamka toka kwenye mitizamo finyu ya maisha ya leo leo na kushabikia vihongo vya hapa na pale badala ya kupigania mabadiliko ya kweli katika maisha yao. Tatizo la kasi ndogo hii si CDM; ni sisi wote tusiochukua hatua za dhati.
 
Mimi sikubaliani na suala la kusitisha maandamano na mikutano. Tukumbuke kuwa CDM ya leo ni matokea ya operation sangara ambayo ni mkutano na maandamano, sasa unaposema wasiandamane una maana waache siasa. Siasa ni maandamano na mikutano. Viongozi wakifuata ushauri wa huyu bwana katika eneo hili wajue kuwa wanaitoa CDM kweye ramani ya siasa. PEOPLE'S POWER iko kwenye mikutano na maandamano.

Napendekeza kama kawa, mikakati yote iende pamoja. PEOPLE'S POWER (MAANDAMANO) NA USHAWISHI WA MTU MMOJA MMOJA NA NYUMBA KWA NYUMBA.

Sijasema mikutano na maandamano yasiwepo kabisa, kuna nafasi kadhaa hayawezi kuepukika. Lakini dhana ya kwamba chama kitajengwa kwa maandamano na mikuano tunatakiwa kuwa wapana wa kuelewe na kusoma mambo yanavyokwelda.

Kwenye mkutano wanaokuja ni mashabiki ambao tumeshuhudia muda mrefu kuanzia kipindi cha Mzee wa Kiraracha, nilikuwa Tabora alivyojaza uwanja mkubwa wa Michezo wa Ali Hasan Mwinyi huwezi kuamini na kilichotokea wakati wa uchaguzi palepale Tabora. Mikutano ni propaganda za kisiasa, lakini si njia mahsusi ya kujenga msingi wa wanachama wenye kukipigia kura. Ndio maana tunapendekeza njia ambazo CCM wamejizatiti ndizo Chadema waende huko kuvunja ngome yao kwa kuanzisha balozi wa nyumba kumi wenye kulinda matawi ya chama na wanachama. Huko utokeapo uchaguzi ni source ya hakika kujua kuna wanachama hai wangapi.

Mikutano tu ikiisha kila mmoja anarudi home nini kinaendelea mitaani?
 


Pendekezo kwa Chadema ni:


  • [*=1]Kuachana na maandamano kwani yanachelewesha watu kuwajibika katika kujenga uchumi wa nchi
    [*=1]Kupunguza mlolongo wa mikutano kwani inapoteza nguvu na rasilimali za chama wakati chama sera zimeshafahamika.
    [*=1]Kuanza mkakati wa kupeleka wajumbe vijijini na mitaani kwa kusaka wafuasi watakao kuwa wanachama hai nyumba kwa nyumba na mtaa kwa mtaa hapo uchaguzi ujapo Chadema itakuwa na uhai wa kura kuanza kuhesabu wanachama hai walio nao kama CCM ifanyavyo, la sivyo watabaki kuvimbisha mishipa usoni majwakwani na kuambulia patupu kura zipigwapo.
    [*=1]Zoezi la kuwapata wanachama mijijini liwe endelevu na kuimarisha kuwa na wajumbe wa nyumba kumi wenye kuhakiki wanachama kwa kulinda na kuhamasisha uhai wao chamani.
    [*=1]Chama kuweka msingi vijijini na kuwa na wanachama ni mtaji mkubwa kwani ndiko kwenye wapiga kura wengi na majimbo mengi ya uchaguzi.
    [*=1]Chambo cha mawasiliano kitaifa iwe ni radio au TV ili harakati na sera za chama ziweze kuwafikia wengi badala ya kutumia tu blog kwa njia ya online ambayo mwenye kufikiwa ni Candid Scope badala ya walengwa wapiga kura walio wengi wa vijijini.

Posho za watumishi wa matawini
Kufanya kazi kwa ridhaa kuna madhara yake. Mfano, unaposikia Katibu Mkuu wa Chadema analipwa Tsh. 7,000,000 huku watumishi wa matawini, katani, mikoa na wengineo wakifanya kazi kwa ridhaa huathiri utendaji na ukuaji wa chama. Chama kiwe na mkakati maalumu kuwapa posho walao kidogo kinachowezekana hawa watumishi.

Ruzuku inayopewa isielekezwe kwenye mikutano na maandamano tu, bali watumishi wa mawawini, katani, mkoani na wengineo wafikiriwe ili wafanya kazi kwa moyo wa matumaini zaidi. Pengine ongezeko la wadiwani sasa hivi litapandisha dau la ruzuku, hivyo ongezeko hilo bora lingeelekezwa kuwapa posho watumishi hao kila mwezi kila inapowezekana ili kupunguza manung'uniko ya hapa na pale na hivyo kuathiri utendaji na uwajibikaji wao. Kumbuka CCM inatumia mwanya wa ukata wa vyama vya upinzani kuwarubuni wapiga kura.​

Kuandaa wagombea nafasi mbalimbali wenye sifa
Jitihada kubwa zinatakiwa kuwekwa katika kuandaa nguvu ya kutosha katika kuwaandaa wagombea katika chaguzi mbalimbali zijazo kwa kipindi kirefu kutosha. Isitumike ila ya zima moto. Kama alifanikiwa Nasari wa Arumeru mashariki kwa mtindo wa zima moto tusitazamie mtindo huo huo utatumika kufanikisha chaguzi nyingine, kwani wagombea wanatakiwa umma uwafahamu kwa kipindi cha kutosha na hivyo wanatakiwa kuwa karibu na maeneo yao wanakotegemea kugombea mara kwa mara.​


Nakubaliana na wewe kuhusu
  • CHADEMA kuachana na maandamano yasiyo ya lazima badala yake ifanyike mikutano ya hadhara kwa lengo la kueneza sera na kupata wanachama wapya. Viongozi wasitumie muda mwingi kulaumu CCM tu; pia wawaeleze wananchi ni kinapaswa kufanywa ili kuachana na udhaifu wa CCM
  • CHADEMA kuwa na radio na TV kwa ajili ya kueneza sera za chama
  • Watumishi wa chama kulipwa mshahara au posho ili kujenga morali ya utendaji. Si vibaya kumlipa Dr. Slaa milioni saba kama chama kina uwezo; Nafikiri kwa sasa CHADEMA isitumie fedha nyingi kuwalipa viongozi wa juu tu badala yake viongozi wa juu walipwe mshahara unaowawezesha kuendesha maisha yao e.g. 2,000,000/= zinatosha; fedha zingine zitumike kuwalipa posho viongozi wa chini. Tusidanganyane eti watumishi wa ngazi za chini watatenda siku zote kwa kujitolea.
  • Viongozi na makada wa chama waandaliwe kwa kupatiwa mafunzo ya uongozi. Chama kianzishe chuo cha uongozi. Wapo wanachama wengi wanaoweza kufanya kazi katika chuo hicho.
 
Sijasema mikutano na maandamano yasiwepo kabisa, kuna nafasi kadhaa hayawezi kuepukika. Lakini dhana ya kwamba chama kitajengwa kwa maandamano na mikuano tunatakiwa kuwa wapana wa kuelewe na kusoma mambo yanavyokwelda.

Kwenye mkutano wanaokuja ni mashabiki ambao tumeshuhudia muda mrefu kuanzia kipindi cha Mzee wa Kiraracha, nilikuwa Tabora alivyojaza uwanja mkubwa wa Michezo wa Ali Hasan Mwinyi huwezi kuamini na kilichotokea wakati wa uchaguzi palepale Tabora. Mikutano ni propaganda za kisiasa, lakini si njia mahsusi ya kujenga msingi wa wanachama wenye kukipigia kura. Ndio maana tunapendekeza njia ambazo CCM wamejizatiti ndizo Chadema waende huko kuvunja ngome yao kwa kuanzisha balozi wa nyumba kumi wenye kulinda matawi ya chama na wanachama. Huko utokeapo uchaguzi ni source ya hakika kujua kuna wanachama hai wangapi.

Mikutano tu ikiisha kila mmoja anarudi home nini kinaendelea mitaani?

Hivi wewe, umeshafanya tafiti za kina za HUJUMA ZA CCM KWENYE CHAGUZI NA UKAZIJUA KISAWASAWA NA KIUNDANI NA IMPACT ZAKE KWA CDM? au umefanikiwa tuu kuchambua kasoro za CDM???
 
Twende kihesabbu kidogo
Ruzuku 233,000,000/=
Pos
ho ya makatibu wa mikoa iwe 400,000/=x30=12,000,000/=
makatbu wa wilaya iwe 250,000/=x140=35,000,000/=
makatibu wa majimbo iwe 200,000/=x239=47,800,000/=
makatibu wa kata iwe 50,000/=xkata2800=140,000,000/=
jumla bila wa matawi ni shilingi 234,800,000/=

Hivyo matawi bado hayajapigiwa hesabu na itambuliwe kuwa hata ukimpa katibu wa mkoa laki nne bado hawezi kujaza mafuta mwezi mzima pikipiki yake kweda kijiji cha wilayani km 200 na hatazaidi.

Wala laki mbili tu ya katibu wa jimbo huwezi kusemani kikubwa kiasi cha kumfanya azunguke jimbo zima mwezi mzima. Elfu hamsin sijui kama kweli ingekutia hamasa mwanajamvi kama katibu kat uache shughuli zako za kukupatia mkate wako ili uhamasishe chama kila sku katani kwako kama si moyo wa kujitolea tu.

Lakini kwa hesabu hiyo chama kitakuwa kinadaiwa 1,800,000/= kila mwezi! bila kujumuisha posho za watendaji makao makuu, kulipia mapango ya ofisi mbalimbali, kununua magari hayo muonayo ya M4C, pikipiki zilizoagizwa, operesheni mbalimbal, kesi, uchapaji kadi nk

Mkikaaga kwenye laptop huwa hamjui hali halisi kiasi kwamba hamjui kuwa watu wengine wakiwa partime hata hizo hekaheka zinazotisha CCM hamtaziona.

Kwa nini kama watu mna uchungu hamjitolei walau kumlipa posho ya katibu wa mkoa mmoja ili kujenga moyo wa wengine kujitolea,. Maneno tuuu
 
Nakubaliana na wewe kuhusu
  • CHADEMA kuachana na maandamano yasiyo ya lazima badala yake ifanyike mikutano ya hadhara kwa lengo la kueneza sera na kupata wanachama wapya. Viongozi wasitumie muda mwingi kulaumu CCM tu; pia wawaeleze wananchi ni kinapaswa kufanywa ili kuachana na udhaifu wa CCM
  • CHADEMA kuwa na radio na TV kwa ajili ya kueneza sera za chama
  • Watumishi wa chama kulipwa mshahara au posho ili kujenga morali ya utendaji. Si vibaya kumlipa Dr. Slaa milioni saba kama chama kina uwezo; Nafikiri kwa sasa CHADEMA isitumie fedha nyingi kuwalipa viongozi wa juu tu badala yake viongozi wa juu walipwe mshahara unaowawezesha kuendesha maisha yao e.g. 2,000,000/= zinatosha; fedha zingine zitumike kuwalipa posho viongozi wa chini. Tusidanganyane eti watumishi wa ngazi za chini watatenda siku zote kwa kujitolea.
  • Viongozi na makada wa chama waandaliwe kwa kupatiwa mafunzo ya uongozi. Chama kianzishe chuo cha uongozi. Wapo wanachama wengi wanaoweza kufanya kazi katika chuo hicho.
Je umefanya utafiti ukagundua kuwa vyama vya upinzani visivyofanya maandamano kama CUF UDP NCCR au TLP vimefanya vizuri kuliko CHADEMA ya maandamano? Pumba Kweli
 
Back
Top Bottom