Mwongozo Chadema baada ya uchaguzi mdogo

Hivi wewe, umeshafanya tafiti za kina za HUJUMA ZA CCM KWENYE CHAGUZI NA UKAZIJUA KISAWASAWA NA KIUNDANI NA IMPACT ZAKE KWA CDM? au umefanikiwa tuu kuchambua kasoro za CDM???

Majimbo na viti vingine vya udiwani ambako Chadema wameshinda hujuma hizo hazikuwepo? Kama Chadema ilifanikiwa kuzima hujuma katika viti walivyovichukua kwa nini ishindikane hilo viti vingine ambavyo hawakuvichukua?

Chadema isimamishe watu wenye sifa ambao wanauzika kwa wapi kura amini Chadema itazoa viti vingi. Akina Samwel Sitta walishaliona hili waliposema Chadema hawana safu ya kutosha, ndio hapo. Kufanya jitihada kusimamisha watu wanaokubali ndio ushindi si wa kuokoteza wasio na ushindani.

Kumbuka kuwa kushindanisha watu kadhaa katika kutafuta mgombea wa kiti ndiko kupata anayefaa, lakini sehemu nyingi utakuta Chadema anajitokeza mmoja tu kama mbovu au mzuri, anauzika au hauziki ndiye ataakayepeperusha bendera ya chama dhidi ya vyama vingine. CCM wanao wengi na anayeibuka huwa amewazidi wenzake na hivyo kuuzika katika kampeni.

Pamoja na kuwa makini hujama katika chaguzi, lakini tusifikirie msingi wa ushindi CCM ni hujuma tu, la hasha, sifa ya mgombea inawasaidia zaidi.
 
Huyu mtoa mada au muongozo inaonekana hajui hata uongozi wa tawi ukoje. uongozi wa chadema wa chini unaazia kwenye misingi ngazi ya kitongoji na msingi moja una viongozi .18. sasa fanya hesabu vitongoji vya nchi mzima mara 18 tawi lina viozozi 12 fanya vijiji vyote nchi mara 12 kata ina zaidi ya viongozi 14 fanya kata zancinini mara 14 jimbo lina zaidi ya viongozi 15 fanya majimbo yote mara 15 haya kila kiongozi mpe posho ya 5,000/ utatakiwa kutoa kiasi gani. ndio maana nasema wewe mtoa mada hujui hata tawi.
 
Twende kihesabbu kidogo
Ruzuku 233,000,000/=
Pos
ho ya makatibu wa mikoa iwe 400,000/=x30=12,000,000/=
makatbu wa wilaya iwe 250,000/=x140=35,000,000/=
makatibu wa majimbo iwe 200,000/=x239=47,800,000/=
makatibu wa kata iwe 50,000/=xkata2800=140,000,000/=
jumla bila wa matawi ni shilingi 234,800,000/=

Hivyo matawi bado hayajapigiwa hesabu na itambuliwe kuwa hata ukimpa katibu wa mkoa laki nne bado hawezi kujaza mafuta mwezi mzima pikipiki yake kweda kijiji cha wilayani km 200 na hatazaidi.

Wala laki mbili tu ya katibu wa jimbo huwezi kusemani kikubwa kiasi cha kumfanya azunguke jimbo zima mwezi mzima. Elfu hamsin sijui kama kweli ingekutia hamasa mwanajamvi kama katibu kat uache shughuli zako za kukupatia mkate wako ili uhamasishe chama kila sku katani kwako kama si moyo wa kujitolea tu.

Lakini kwa hesabu hiyo chama kitakuwa kinadaiwa 1,800,000/= kila mwezi! bila kujumuisha posho za watendaji makao makuu, kulipia mapango ya ofisi mbalimbali, kununua magari hayo muonayo ya M4C, pikipiki zilizoagizwa, operesheni mbalimbal, kesi, uchapaji kadi nk

Mkikaaga kwenye laptop huwa hamjui hali halisi kiasi kwamba hamjui kuwa watu wengine wakiwa partime hata hizo hekaheka zinazotisha CCM hamtaziona.

Kwa nini kama watu mna uchungu hamjitolei walau kumlipa posho ya katibu wa mkoa mmoja ili kujenga moyo wa wengine kujitolea,. Maneno tuuu

Uchanganuzi wako umejengeka katika kuangalia pato la ruzuku tu kama ilivyo. Hii ni sawa nawe mshahara unaoupata uufanyie uchanuzi wa matumizi kama ulivyo bila kulifanyia kazi ya ziada pato lako ili kulirudufu liwe na mafao zaidi.

Chadema kama chama kikuu cha upinzania kinatakiwa kiwe na mbinu za:

  • Kujijenga kisiasa na kujitanua
  • kubuni miradi ya kiuchumi
  • kutumia ruzuku kama mtaji mojawapo wa kuendeshea miradi ya uzalishaji
  • Matumizi ya chama yangetakiwa yawe faida baada ya mzunguko wa pesa katika kuchuma nyingine
  • Kushirikiana na vyombo vya kimataifa katika kupata misaada ya kuboresha miradi ya maendelo ya chama kiuchumi na kisiasa.

NB: CCM haijajenga uchumi wake tokana na mapato ya


  1. [*=1]ada za uanachama tu
    [*=1]kujimilikisha mali za taifa kama majumba, viwanja vya michezo, vyombo vya habari tu
    [*=1]Kuhodhi viwanja na kuvijenga kwa kupangisha watu tu
    [*=1]CCM imepata misaada mingi kutoka nchi za kijamaa za Urusi na nchi nyingine za mahariki kujenga miradi ya uchumi kama:


  • [*=1]Ofisi Kuu Dodoma ni msaada kutoka nchi za Mashariki
    [*=1]Jengo la mikutano lililokuwa ilipo chuo kikuu Dodoma ilikuwa ni msaada toka nchi za kijamaa za mashariki
    [*=1]Jengo la makao madogo Lumumba walipewa

Chama kinatakiwa kuwa na wataalamu wa uchumi si kwa malengo ya kisiasa tu, bali pia kwa nia ya kukijenga chama kiuchumi. Kutegemea Ruzuku si vema kwani kutatokea muhula viti kupungua hapo shughuli za chama zitaendeshwaje?

Chama kinahitaji kuwa na malengo ya muda mfupi na mrefu katika kujenga kisiasa, kiuchumi na kimtandao.

Note:
Hakuna chama cha siasa kilichoimarika bila kusaidiwa
 
Huyu mtoa mada au muongozo inaonekana hajui hata uongozi wa tawi ukoje. uongozi wa chadema wa chini unaazia kwenye misingi ngazi ya kitongoji na msingi moja una viongozi .18. sasa fanya hesabu vitongoji vya nchi mzima mara 18 tawi lina viozozi 12 fanya vijiji vyote nchi mara 12 kata ina zaidi ya viongozi 14 fanya kata zancinini mara 14 jimbo lina zaidi ya viongozi 15 fanya majimbo yote mara 15 haya kila kiongozi mpe posho ya 5,000/ utatakiwa kutoa kiasi gani. ndio maana nasema wewe mtoa mada hujui hata tawi.

Nimeleta mapendekezo au maoni yangu, kuna ambayo wachangiaji wataona yanafaa au la, lakini jambo la msingi chama kiwe na malengo ya kuwapa pasho watumishi wake, na kama pato halitoshi kuna umuhimu wa kubuni vyanzo vya kiuchumi ili chama kijitoe na ukata wa pato la matumizi yake. Rejea mchanganuo wangu kuhusu mapendekezo kuhusu namna inayotakiwa chama kujijenga kisiasa na kiuchumi katika bandiko #64 katika mada hii. Ina maana Chama kiwe na malengo ya muda mfupi na mrefu na pia kutafuta wahisani kimataifa kama CCM ilivyofanya ili kupata mitaji ya kuendeshea miradi ya kiuchumi kwa ajili ya kuendeshea chama.

Chama kuomba pesa na kuzitumia tu ni sawa na ombaomba ambaye anachokipata ni kula kisha kesho anarejea tena barabara kuomba. Chama kina wasomi wengi na wachumi wengi na wapenzi wengi nje na ndani ya nchi.

Mpango wa kununua Chopper
Nilisikia kama wana mpango wa kununua chopper, ni jambo zuri kwani chopper hizo zinapohitajika na chama kama katika kampeni na kusafirisha maofisa wake itakuwa ni ukombozi. Lakini chopper hizo zinaweza kuwa pia vitega uchumi katika nchi hii katika nyanja za kibiashara na utalii jambo ambalo litakisaidia chama kiuchumi kukua zaidi badala ya kuwa tegemezi.​

Huwa nafurahi kama chama kinaomba misaada ya kuweka vitega uchumi badala ya pesa ya matumizi ambayo ni utumwa wa kurudia kuomba tena kesho.
 
images
images
images

Uchaguzi mdogo wa madiwani ulikamilishwa na wapiga kura nchini Jumapili October 28, Chadema kimepata funzo kubwa lenye kutoa tafsiri kadhaa zenye kuleta matumaini kwa wenye moyo mkuu au kufifisha kwa wenye moyo mchache.

Kauli ya Freeman Mbowe yazaa tunda la kwanza
Mwenyekiti wa Chadema miezi michache iliyopita alitoa kauli ya kuwaasa vijana wasomi na wengine kujitokeza na kuchagua maeneo ya kugombea nafasi mbalimbali zikiwemo za uwakilishi ili waandaliwe. Wengi tulipongeza kwa utashi huo, kwa bahati nzuri katika uchaguzi huu mdogo wa Madiwani uliomalizika, kuna kijana mmoja msomi ambaye ameamua si kusubiria nafasi ya kugombea ubunge, bali ameamua kuanzia nafasi ya udiwani naye si mwingine bali ni diwani mchaguliwa wa kata ya Mlangali katika wilaya ya Ludewa ndani ya Mkoa mpya wa Njombe. Tunampongeza kwa kujituma, kutetena azima yake na kushinda. Kwa wengi haikuwa katika picha kwamba Chadema yaweza kupata kiti cha udiwani huko kuliko ngome ya CCM miaka nenda rudi kwa akina hayari Horace Kolimba, ni dalili kwamba mipango ikifanyika kwa umahiri na kumsimamisha mwenye sifa yawezekana, na imewezekana. Ni dhahiri Chadema imeshafunguliwa mlango Ludewa.

Diwani mchaguliwa ametoa mwanga kwa vijana wengi ambao pengine kwa kutokuwa na ujasiri wa kuthubutu wanahofia kitu wasichokuwa na hakika nacho kama watashinda au la, lakini kwa uchaguzi huu tumapata jibu kuwa wananchi wengi wanatuhitaji vijana katika kuleta mabadiliko katika jamii na maendeleo ya taifa letu. Chadema zoezi hilo limefana sana, wana mfano wa kuwafunda vijana wasomi wengi wajitokeze.​

Kutofanya vizuri uchaguzi huu chadema sababu kusimamisha wagombea dhaifu
Maeneo mengi ambayo nguvu kubwa ya Chadema imetumika tumekuja kushuhudia kutoambulia hata kiti kimoja. Unaweza kujengeka utetezi wa aina mbalimbali, lakini kubwa zaidi ni Chama kuwaandaa wagombea wanaofaa ndio tatizo. Chama kisitegemee tu jina la Chadema limpatie mgombea kura, ila auzike na wapiga kura ndipo waridhie. Tatizo kubwa ambalo naona wagombea wengi wa Chadema kula mwanguko wa mende ni kukosa sifa kulinganisha na wagombea wa CCM. Eneo hilo linatakiwa kufanyiwa kazi na Chama.​

Mbinu za Chadema kujitanua zibadilishwe kuendana na upepo unavyovuma.
Yale maandamano na mikutano ya hadhara inaonekana kutokuwa na nafasi kubwa kwa watanzania leo, kwani kama kuwasikia Chadema tumewasikia sana tu na jina la Chadema linalia masikioni mwa wengi kama mwangwi wa mlima Kilimanjaro. Tabia ya kinyonga kujibadilibadili rangi kuakisi mazingira yanayomzunguka ndiyo inayohitajika kwa Chadema sasa hivi.

Pendekezo kwa Chadema ni:


  • [*=1]Kuachana na maandamano kwani yanachelewesha watu kuwajibika katika kujenga uchumi wa nchi
    [*=1]Kupunguza mlolongo wa mikutano kwani inapoteza nguvu na rasilimali za chama wakati chama sera zimeshafahamika.
    [*=1]Kuanza mkakati wa kupeleka wajumbe vijijini na mitaani kwa kusaka wafuasi watakao kuwa wanachama hai nyumba kwa nyumba na mtaa kwa mtaa hapo uchaguzi ujapo Chadema itakuwa na uhai wa kura kuanza kuhesabu wanachama hai walio nao kama CCM ifanyavyo, la sivyo watabaki kuvimbisha mishipa usoni majwakwani na kuambulia patupu kura zipigwapo.
    [*=1]Zoezi la kuwapata wanachama mijijini liwe endelevu na kuimarisha kuwa na wajumbe wa nyumba kumi wenye kuhakiki wanachama kwa kulinda na kuhamasisha uhai wao chamani.
    [*=1]Chama kuweka msingi vijijini na kuwa na wanachama ni mtaji mkubwa kwani ndiko kwenye wapiga kura wengi na majimbo mengi ya uchaguzi.
    [*=1]Chambo cha mawasiliano kitaifa iwe ni radio au TV ili harakati na sera za chama ziweze kuwafikia wengi badala ya kutumia tu blog kwa njia ya online ambayo mwenye kufikiwa ni Candid Scope badala ya walengwa wapiga kura walio wengi wa vijijini.

Posho za watumishi wa matawini
Kufanya kazi kwa ridhaa kuna madhara yake. Mfano, unaposikia Katibu Mkuu wa Chadema analipwa Tsh. 7,000,000 huku watumishi wa matawini, katani, mikoa na wengineo wakifanya kazi kwa ridhaa huathiri utendaji na ukuaji wa chama. Chama kiwe na mkakati maalumu kuwapa posho walao kidogo kinachowezekana hawa watumishi.

Ruzuku inayopewa isielekezwe kwenye mikutano na maandamano tu, bali watumishi wa mawawini, katani, mkoani na wengineo wafikiriwe ili wafanya kazi kwa moyo wa matumaini zaidi. Pengine ongezeko la wadiwani sasa hivi litapandisha dau la ruzuku, hivyo ongezeko hilo bora lingeelekezwa kuwapa posho watumishi hao kila mwezi kila inapowezekana ili kupunguza manung'uniko ya hapa na pale na hivyo kuathiri utendaji na uwajibikaji wao. Kumbuka CCM inatumia mwanya wa ukata wa vyama vya upinzani kuwarubuni wapiga kura.​

Kuandaa wagombea nafasi mbalimbali wenye sifa
Jitihada kubwa zinatakiwa kuwekwa katika kuandaa nguvu ya kutosha katika kuwaandaa wagombea katika chaguzi mbalimbali zijazo kwa kipindi kirefu kutosha. Isitumike ila ya zima moto. Kama alifanikiwa Nasari wa Arumeru mashariki kwa mtindo wa zima moto tusitazamie mtindo huo huo utatumika kufanikisha chaguzi nyingine, kwani wagombea wanatakiwa umma uwafahamu kwa kipindi cha kutosha na hivyo wanatakiwa kuwa karibu na maeneo yao wanakotegemea kugombea mara kwa mara.​

Kuunganisha nguvu za upinzani
Mwenyekiti wa Chadema ambaye ni mbunge na mkuu wa kambi ya upinzani bungeni, mara baada ya uchaguzi mkuu uliopita alisema kuungana kambi ya upinzani wapate muda kwanza kwa sababu ya majeraha ya uchaguzi. Hilo lilieleweka. Sasa majeraha ni karibu yamepona labda kama yapo ambayo yamegeuka kuwa donda ndugu.

Viongozi wa Chadema kitaifa wanatakiwa wataremke kutoka pale walipo ili wawafikie wenzao na kupika na kula meza moja chakula kinakuwa kitamu zaidi. Unyenyekevu ni siri moja kubwa katika kujiwekea malengo ya mafanikio. Ushupavu umewaweka wengi katika hali ya kubakizwa isolated. Ukiwa na mtoto jifanye kama watoto wafanyavyo, kwa wachezaji utajifanya mwanamichezo, wasomi utaongea mambo ya kisomi nk. Ndilo linalotakiwa Chadema wawaone wenzao vyama vya upinzani ni hazina katika kubuni, kupanga na kufanikisha mikakati ya kuikomboa nchi. Kura nyingi katika uchaguzi mdogo uliomalizika utakuta kama wangeunganisha nguvu CCM ingetelekeza viti vingi zaidi, sasa bora lipi? Kuthoofisha nguvu za CCM kwa kunyang'anya himaya yao kuwa chini ya umoja wa upinzani au kubaki na unyonge wa mwenye kiti kimoja abaki kivyake na wenye viti vingi wajisikie kujitutumua huku kuchukua dola ikibaki ndoto za kufikirika?​

Viongozi kitaifa watambue kasoro zisemazo wajitahidi kujirekebisha
Viongozi wa kitaifa Chadema yanayolalamikiwa na baadhi ambao wamewahi kufanya kazi nao na kisha kuamua kujitoa hayawezi kubezwa, kwani lisemwalo lipo kama halipo laja, na tujue hawa ni binadamu kama tulivyo wengi tulivyo na kasoro nyingi tu za kimaumbili, kimaadili, kifikra, kujikuza, kujiona baora, na kiutambuzi. Siyo kubeza tu, wanatakiwa kujitathmini, maana kuendekeza sana tabia binafsi na nafsi ya mtu katika uongozi ni hatarishi katika nyanja za siasa. Yalisemwa, yanasemwa, lakini kuyaacha yapite tu kama tunataka mageuzi ya kweli hatutakuwa wa kweli na kuwatakia mema.
Hulka ya kiaongozi katika jamii:​


  • [*=1]ushirikiano na ushirikishi,
    [*=1]unyenyekevu na ukakamavu,
    [*=1]uvumilivu na ustahimilivu,
    [*=1]hekima na busara
ni mambo ambayo yanamjengea heshima na mafakio katika utumishi. Maamuzi ya papo kwa papo ni hatari, majuto ni mjukuu kwani maji yakishamwagika hayazoleki.

Viongozi wanatakiwa kuondokana na kulewa sifa, kulewa umati wa wahudhuriaji mikutano. Wanaohudhuria mikutano ya Chadema walio wengi ni mashabiki ambao si wapiga kura tofauti na mikutano ya CCM ambayo wahudhuriaji ni wapiga kura. Mkutano wa CCM wahudhuriaji 75% ni wapiga kura wake wakati wahudhuria wa Chadema kiwango hicho hicho wahudhuria ni mashabiki tu kama inapotokea tukio fulani watu wanafurika isivyotegemewa ndivyo Chadema wanavyotakiwa kusoma mwelekeo huu unavyowalaza chali katika chaguzi. CCM inapobeba watu kwa malori ni wanachama wake si mashabiki wakati mikutano ya Chadema wanaofurika ni mashabiki wasio wapiga kura. Hii ndiyo hali halisi ya tathmini yangu.​

Diwani wa Mlangali, Ludewa ni changamoto na hasa kwa vijana wasomi
Vijana wasomi na wahitimu wengi vyuo vikuu tumekuwa na kasumba ya kuhangaika huku na kule huku tukilazimika kumaliza kandambili zetu kwa ajili ya kutembeza RESUME wakati tuna nafasi tele kama za huyu msomi mwenzetu kuelekeza nguvu huko matawini, vijijini, katani na wilayani kujenga msingi wa maisha. Ametufunza mengi, ametufunza mengi, wenye upeo wa masafa marefu wamempata, wenzangu mimi wenye kufikiria leo na kesho tu tutabaki kuchakaza kandambili kutembeza resume huku na kule.​


Binafsi nimevutiwa na mwono huo, huenda wengine wakaona isovyo kwa sababu tunapendelea kusifiwa tu na kuonyesha na madhafu tunaona kero fulani kwa watu wa uchambuzi wa aina hiyo.
 
Back
Top Bottom