Mwongozo Chadema baada ya uchaguzi mdogo

Kuna tatizo kubwa katika kuteau wagombeaji,ieleweke wazi kuna watu wazuri wenye uwezo wa kugombea na kushinda lakini hawajitokezi,sababu haijulikani bado,ni wazi vilevile watu wanachagua mtu na sio chama,ccm walijitahidi kuteua watu wanaokubalika,hilo ndio tatizo kubwa
 
CDM, operation zenu zimekuwa msaada mkubwa katika kuleta vuguvugu la mabadiliko na kujenga chama mijini na vijijini.

Pamoja na changamoto zote, kazi hiyo iendelee kwa nguvu na uzito
uleule.

Shirikisheni umma, mnapokwama.

Nakumbuka mliishia Iringa, toeni ratiba mkizingatia muda na majukumu mengine ya chama na viongozi.

Mikutano inayojumuisha timu ina impact kubwa kuliko ya mmoja mmoja!

Wananchi wanawasubiri, waliambiwa Hakuna Kulala!
 
Sitaki kuamini kama maneno haya yameandikwa na Candid scope.

Ni aibu kubwa sana kuandika vitu bila kufanya utafiti wa kina.

*Nitarudi kufafanua zaidi
 
Umeona eeh......Magamba yanajua nguvu yao ya dola kuzuia M4C imestukiwa na ulimwengu mzima wanataka sasa kuja na ushauri nasaha ili ku-derail hii silaha muhimu ya CDM.

Inaonekana milango mingi kuingilia CDM imefungwa sasa naona wanatafuta madirisha ili waweze kuingia kwakuweka chambo.....Pamoja na mengine yote haiingii akilini kuleta hoja ya Katibu kulipwa mshahara kumbuka huyu analipwa ujira wake kwa kazi ailiyoifanya kwa CDM..

Si kuwa hao wengine si muhimu bali hata wao bila wale wa mwanzo kujitoa kafara leo hii wasigetamani kuwa one among CDM.....Huu ujamaa usiozingatia malipo halali ni hatari sana.

Ndiyo hasa kilichafanya CCM ikageuka kuwa ya mafisadi....Na kila mtu kuanza kuishi kiujanja badala ya kufanya kazi na kulipwa inavyostahili.....
 
Mleta mada acha kuishi kwa hisia bali kwa uhalisia.

*Ni ujinga mkubwa kubeza mafanikio madogo ya CHADEMA kupitia matokeo ya chaguzi hizi za udiwani bila kuangalia kwanza mwenendo mzima wa uendeshaji wa uchaguzi ulivyokuwa.
 
*SAHIHISHO
Kuhusu Joshua Nassari kushinda Ubunge kule Arumeru Mashariki mwaka huu, ningependa nikufahamishe kuwa haikuwa bahati bali ni mkakati kwani mgombea alijiandaa na chama kilimwandaa vizuri kabla ya 2010.
 
Ni aibu kubwa sana kuandika vitu bila kufanya utafiti wa kina.

*Nitarudi kufafanua zaidi......[/QUOTE]

Hata mimi imenistua sana......Its like this, let me expose them maana shetani hapendi mwanga anapenda giza zaidi..M4C imeleta damage kubwa sana kwenye magamba na hawana ubavu wakuendelea kutumia nguvu kubwa iliyodhahiri kuisitisha..Na inawezekana kabisa hata haya matokeo ya udiwani si ya kweli...Kwanini?

Walikuwa wanajua what they are after kwamba kisiasa kuonyesha jamii na CDM wenyewe hiyo M4C haijawa na impact kubwa kama wanavyodhani..Na kwakua hakuna data base ya huhakika Tz kutokana na mfumo mbaya wa governance..(Hata local government nyingi hazina socio-economic profile zao kujua who is who and where are they na ili kutengeneza hili si kazi ya siku moja na inahitaji resources) so wakajua inahitaji akili sana na intelligence syatem kwa CDM kung'amua hili then wamepanga usanii wao waki system na nje wanakuja kama washauri kumbe ndiyo wale wale...

Kwanini nasema haya kwasababu haiingii akili kwa true member wa CDM kuja na vitu public vya kuibomoa zaidi kuliko kuijenga..Tena hizo advice zi reflect kabisa matukio halisi....Ingekuwa inafanywa na watu in-experienced ningeelewa lakini wale wenye akili zao timamu na wenye uwezo wa ziada..CDM kumbukeni maneno ya Wasira......M4C ndiyo dawa pekee ya kuwafikishia elimu ya uraia watu wengi hasa wale ambao siyo elite maana wengi wako emotional na siyo rational..Then on top sasa mjitahidi kutafuta jinsi ya kuwa-retain kwa incentive based mechanisms ambayo wala si garama sana kama tutajipanga vizuri..Ni coordination tu inayohitajika wala si financial facility kubwa just a seed money.
 
Kuandaa nguvu ya mikutano na maandamano tu si suluhisho na hapa nakubalina nawe hata sisi tuwe tayari kuchangia uimarishaji wa matawi vijijini na hata chama chenyewe kiwe na bajeti hiyo kwani ni eneo ambalo lina umuhimu wa kwanza kwa sasa.

Wakuu nashukuru mmeliona hilo, maana wenzenu si kuwalipa posho tu but wanagawa mpaka mbuzi kwa kupigiwa kura.
 
Hapa nitarudi asubuhi, tumeshauri mengi sana sasa kama hawayasomi mimi nitashangaa sana, muulize kila mtu anaijuwa BAVICHA lakini ni nani anaijuwa BAWACHA? hivi watu wanashindwa kujuwa chama kinahitaji sana wanawake majasiri wa kwenda kuwaamsha usingizini Wanawake wenzao?

Maana Wasichana wasomi na wasio wasomi wote wako BAVICHA huku BAWACHA inaonekana ni maujanja dot com tu. ifumuliwe yote we need New reform for BAWACHA.

mkuu matola nakuunga mkono.Nilipendekeza Ester wassira awe mwenyekiti wa BAWACHA! yule dada ni msomi pia ana anaweza kuwashawishi wanawake.Mtaji mkubwa wa CCM ni wanawake.
 
Kutofanya vizuri uchaguzi huu chadema sababu kusimamisha wagombea dhaifu
Maeneo mengi ambayo nguvu kubwa ya Chadema imetumika tumekuja kushuhudia kutoambulia hata kiti kimoja. Unaweza kujengeka utetezi wa aina mbalimbali, lakini kubwa zaidi ni Chama kuwaandaa wagombea wanaofaa ndio tatizo. Chama kisitegemee tu jina la Chadema limpatie mgombea kura, ila auzike na wapiga kura ndipo waridhie.​


Point hii ndiyo iliyosababisha kwa kiasi kikubwa madhara tuliyopata katika chaguzi hizi za madiwani. Uongozi uchukue hatua za makusudi kuhakikisha hali hii haijirudii katika chaguzi zijazo.​
 
hili la chombo cha habari nalo limesemwa sana ijapo bado hatuoni mrejesho ...on top,ushauri wako ufanyiwe kazi na chama.
 
Mimi sikubaliani na suala la kusitisha maandamano na mikutano. Tukumbuke kuwa CDM ya leo ni matokea ya operation sangara ambayo ni mkutano na maandamano, sasa unaposema wasiandamane una maana waache siasa. Siasa ni maandamano na mikutano. Viongozi wakifuata ushauri wa huyu bwana katika eneo hili wajue kuwa wanaitoa CDM kweye ramani ya siasa. PEOPLE'S POWER iko kwenye mikutano na maandamano.

Napendekeza kama kawa, mikakati yote iende pamoja. PEOPLE'S POWER (MAANDAMANO) NA USHAWISHI WA MTU MMOJA MMOJA NA NYUMBA KWA NYUMBA.
 
Akili ni nywele na kila mmoja ana zake. Lakini pia naheshimu sana mchango wako. Haya ni maoni yangu binafsi nikichukulia mifano ya waliofanikiwa kwa kutumia njia hiyo kwani umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Katu kidole kimoja hakivunji chawa.

Uhuru wa visiwa vya Zanzibar na Pemba vilivyafanikiwa baada ya vyama vya wazawa kuwa na umoja, na hivyo mapinduzi yalipangwa kwa pamoja, la sivyo mambo yasingewaendea kama ilivyokuwa.

Mwai Kibaki wa Kenya alifanikiwa kumng'a kisiki Daniel Arap Moi baada ya kutaabika mara kadhaa bila mafanikio, mwishoni aliamua kuteremka awakute wenzake kwenye kambi ya upinzani, alipounganisha nguvu ndipo dhoruba kali ya umoja wao ilimshinda nguvu Daniel Arap Moi.

Zambia tumeshuhudia mageuzi ya kisiasa yametokana na kuunganisha nguvu hizo pia.

Tanzania kabla ya uhuru kulikuwa na vyama vingi ambayo vingi vikiwa ni social clubs, lakini Nyerere akianzia na kile cha TAA alifanikiwa kuunganisha hata club za akina Kawawa huko makazini na kuwa na nguvu ya pamoja katika kudai uhuru na hivyo kuwa chimbuko la TANU.

Kama hali itaendeleea hivi hivi kwa kuwaweka kando wapinzani hapo CCM itakuwa imefanikiwa copy and paste ya mfumo wa mkoloni mwangereza ya divide and rule.

Baadhi ya ushauri mzuri sana, lakini mengi umekurupuka, hivi mkutano wa siku 1 ndani ya miezi sita kweli unakwamisha maendeleo ya wananchi, maana kwa viongozi wa mkoa wa CHADEMA au kitaifa wa kipita katika eneo moja inaweza kuchukua hadi mwaka mmoja kuja kufanya tene mkutano, hapo umechemsha, Eti watendaji wa matawi walipwe posho hoja nzuri lakini ni suala la kipaumbele, ruzuku wanayopata chadema sio kubwa kiasi hicho, ni suala la kuamua kutumia ruzuku hiyo kukijenga chama au kulipa posho, CHADEMA wameamua kutumia ruzuku hiyo kukijenga chama kwanza
 
Ili nisipoteze muda wangu leo kujadili kitu kinachofahamika, kwanza jiulizeni wakati Dr Slaa anagombea Urais watu wengi si walidhani jimbo la Karatu ndio linaondoka? wengi hatukujuwa kama Dr Alimuandaa mtu makini anayeaminika na anachagulika.

Anayetaka kuyaona mafanikio ya haraka siri kubwa ndio hiyo ni lazima wagombea waandaliwe na wawe wanaheshimika na kukubalika, uchaguzi hauwezi kuwa mgumu kamwe. huwezi kusimamisha mgombea from no where utegemee kushindana na CCM huku ni kujidanganya labda kwa baadhi ya cases kuwe na kura za chuki, ndipo mgombea dhaifu na asiyekubalika hushinda uchaguzi bila watu kuamini.
 
ntarudi nisome taratibu kuna ushauri wa tija humu lakini pia kuna ghiliba kama kumsema sema katibu mkuu hii inanitia wasiwasi cha msingi ni kwamba watu wanaogombea au wenye nia ya kugombea wajipime zaidi wasiwe wanategemea zaidi nguvu ya chama bila hata wao kujiandaa lakini yote tisa chadema imeendelea kuongeza madiwani zaid ni hatua
 
Ili nisipoteze muda wangu leo kujadili kitu kinachofahamika, kwanza jiulizeni wakati Dr Slaa anagombea Urais watu wengi si walidhani jimbo la Karatu ndio linaondoka? wengi hatukujuwa kama Dr Alimuandaa mtu makini anayeaminika na anachagulika.

Anayetaka kuyaona mafanikio ya haraka siri kubwa ndio hiyo ni lazima wagombea waandaliwe na wawe wanaheshimika na kukubalika, uchaguzi hauwezi kuwa mgumu kamwe. huwezi kusimamisha mgombea from no where utegemee kushindana na CCM huku ni kujidanganya labda kwa baadhi ya cases kuwe na kura za chuki, ndipo mgombea dhaifu na asiyekubalika hushinda uchaguzi bila watu kuamini.

Mkuu mawazo ni mazuri lakin yanachangamoto zake pia. Huoni kama ile demokrasia ya mtu kugombea na kuchagua ndan ya chama itakuwa inaminywa?

Mimi nadhani huu mfumo uliopendekezwa sasa wa vijana kuonyesha nia mapema ndani ya chama na kupatiwa mafunzo ya kiuongozi pamoja na mikakati ya ushindi halaf baadae wakauze sera zao kwa wanachama ili wapitishwe kupeperusha bendera ya chama ni mzuri zaidi kuliko kuandaa warithi
 
Ili nisipoteze muda wangu leo kujadili kitu kinachofahamika, kwanza jiulizeni wakati Dr Slaa anagombea Urais watu wengi si walidhani jimbo la Karatu ndio linaondoka? wengi hatukujuwa kama Dr Alimuandaa mtu makini anayeaminika na anachagulika.

Anayetaka kuyaona mafanikio ya haraka siri kubwa ndio hiyo ni lazima wagombea waandaliwe na wawe wanaheshimika na kukubalika, uchaguzi hauwezi kuwa mgumu kamwe. huwezi kusimamisha mgombea from no where utegemee kushindana na CCM huku ni kujidanganya labda kwa baadhi ya cases kuwe na kura za chuki, ndipo mgombea dhaifu na asiyekubalika hushinda uchaguzi bila watu kuamini.

That is true. Kuokoteza wagombea ndiko kunakoiangusha chadema licha ya kuwa na sera nzuri mgombea awe na sifa zinazomwuza na atanadika.
 
Back
Top Bottom