PreGE2025 Mwl. Steven Jacob aliyedaiwa kutekwa na watu wasiyojulikana apatikana Kilimanjaro akiwa amepigwa

PreGE2025 Mwl. Steven Jacob aliyedaiwa kutekwa na watu wasiyojulikana apatikana Kilimanjaro akiwa amepigwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
huenda ni waamini wake tu wameamua kumrekebisha tabia kwa style hiyo ili ijulikane moja ikiwa mtumishi huyo anafanya siasa au anahubiri neno la Mungu kwenye jengo ambalo waamini walijenga kwaajili ya kuhubiri neno la Mungu 🐒
Wewe mama una akili?.
 
Wakuu,

Sasa hivi ni mwendo wa kutekana tu, hali inazidi kutisha, ni muda wa wananchi kuungana kuliko wakati wowote ule kupinga udhalimu huu.

===


Mtumishi wa Mungu anayejulikana kama Mwl. Steven Jacob aliripotiwa kutekwa asubuhi ya jana Mei 16, 2025 nyumbani wake na watu wasiyojulikana ambao walifika nyumbani kwake na cruiser nyeupe na kutokomea naye pasipojulikana.

Usiku huu imeripotiwa na wananchi kuwa amepatikana sehemu inatwa Forest mkoa wa Kilimanjaro baada ya kutupwa huko akiwa amepigwa sana, ambapo wasamaria hao wamempeleka kituo cha afya kupatiwa huduma ya kwanza na matibabu zaidi mpaka ndugu zake watakapofika.

Pia soma Pre GE2025 - Mchungaji Mwl Steven Jacob atekwa na watu wasiojulikana

Mtumishi huyu amekuwa akipost video kuikosoa serikali ambazo ndio zinasema kama chanzo cha utekaji huu kufanyika.

Kuna video alipost akisema Samia hafai kuwa Rais na akilazimisha atasababisha damu kumwagika sana nchini, na nyingine alipost akiwaambia polisi na serikali wajitafakari baada ya kuuliwa na radi kwani huo ni ujumbe wa Mungu kama kuwaonya.
Alipohusisha Samia na Askari ndipo alipoyakanyaga.
 
Hongera kwa jamii wapenda haki na Jeshi la polisi
Huyo nae kwa nini anaikosoa serekali, hajui kuwa serikali inatakiwa kusifiwa tu bila kukosolewa?!

Mjinga sana huyo anajiita mwalimu sijui mchungaji sijui nani.
 
We zombie CCM ndio baba lao, hao vibaraka wako hawatapata uongozi asilani. Mke wa Lissu ni raia wa Ubelgiji ameshapewa makazi, hujamwona juzi? Mtamalizwa moja moja.
Kwa hiyo hamuwezi tena kushindana nao kwa hoja bali sasa ni kuwamaliza moja moja eti?
 
huenda ni waamini wake tu wameamua kumrekebisha tabia kwa style hiyo ili ijulikane moja ikiwa mtumishi huyo anafanya siasa au anahubiri neno la Mungu kwenye jengo ambalo waamini walijenga kwaajili ya kuhubiri neno la Mungu 🐒
Sijawahi kumuona mwanamke mtekaji kama huyu anaependa kuona damu za watu zinamwagika
 
CHADEMA,
mkusanye ushahidi kwa haya maovu yanayofanyika
polisi wajiande kisaikolojib chadema ikiwa chama tawala

Ni uonevu na dhambi kumteka mtu kwaajiri ya madaraka na kumpiga au kumuua

Mungu ni mwema kama wamemuachia akiwa hai
Umesema polisi?
 
Sijawahi kumuona mwanamke mtekaji kama huyu anaependa kuona damu za watu zinamwagika
sijawahi kuona mtu lofa kama yule anaefumaniwa na mke wa mtu na kutembezewa kichapo halafu anasingizia kutekwa.

hiyo ni nonsense 🐒
 
sijawahi kuona mtu lofa kama yule anaefumaniwa na mke wa mtu na kutembezewa kichapo halafu anasingizia kutekwa.

hiyo ni nonsense 🐒
Mwanamke anayeogopa hata mende chooni,kila anachoambiwa ni kuogopa tu,kana kwamba kitamdhuru
 
Back
Top Bottom