Mwl. Nyerere hakuwa Mungu

Mwl. Nyerere hakuwa Mungu

Lakini Jamani huyu anafaa kuitwa mtakatifu kwa wenzetu Sawa kwani hatamitume kila mwenyemazingaombwe huitwa mtume baadae wanaishia kupeperushwa mapicha nabinti naomba utakatifu utumike kwa baadhi yaimani tusilazimishwe imani zote tumtamke hivyo mimi sintotumia jina hilo hatakama namuona jaji pale waangalie mpaka kufikia vizazi vyawatoto wetu watajikuta wanamwita mungu watajijua walioanzisha nawalio ona wakaliacha lipevuke mbeleni wasaga meno nakilio kikuu tumeamrishwa tukatazane mbaya ambayo humchukiza muumba tukumbushane yanaompendeza muumba
Hiyo bangi ni ya wapi, Arusha au Tarime!
Nenda taratibu nayo, la sivyo ubongo utanyauka haraka ungali kijana. Bado unayo maisha marefu sana hapo ulipo, kunyaukiwa na ubongo wakati huu.
 
Hiyo bangi ni ya wapi, Arusha au Tarime!
Nenda taratibu nayo, la sivyo ubongo utanyauka haraka ungali kijana. Bado unayo maisha marefu sana hapo ulipo, kunyaukiwa na ubongo wakati huu.
Hakika nakwambia yule ambae anaona dunia nimakazi yake milele yupo kwenye hasara kubwa tumeamrishwa tukumbushane mema tukatazane mabaya pia mwenyezi mungu alisha sema cheo chake hatompa mungine kifupi ametakasika mwenyezi mungu tafakari ndugu yangu kunamaisha baada yadunia hii na ufahamu asiosema Uongo ni mungu tu kumwita mwanasiasa mtakatifu nikujiweka upofu kwakuwa wanasiasa husema sana uongo kama vile m50 kila kijiji democrasia silazima mtu aamini unacho kiamini Nashukuru kwa ushauri wako kweli mimi nikijana mdogo ninayofahamu nihayo
 
pia mwenyezi mungu alisha sema cheo chake hatompa mungine kifupi ametakasika mwenyezi mungu tafakari ndugu yangu kunamaisha baada yadunia hii na ufahamu asiosema
Umewasiliana naye kwa mara ya mwisho lini rafiki yako mungu akakueleza hayo unayoyaeleza hapa..
Ukiwasiliana naye tena, mwambie watu wapo bize na misheni zao, na kwamba hawana mida ya kusikiliza wavuta bangi.
Usisahau kufikisha salaam nyingi toka kwa kalamu1.
 
Lengo ni Jiwe kuwekewa malengo ya kutawala zaidi ya mihura miwili, mleta uzi umekwama, ulikolala ndio tulipoamkia.
 
NI MIMI.Punch kilikuwa ni kikundi kisichojulikana ambacho hakikuwa na jukwaa la kusemea na hakikujulikana tangu mwaka 1961 UDSM ilipoanza kilikuwapo kukosoa uongozi wa chuo na serikali bila kujulikana. Matiko Matare, Rudovick Bazigiza, James Mbatia, Mosene Nyambabe, Antony Komu ,Kangi Lugola, Harun kimaro, Ally Salehe na Dr.Kebwe walikuwa ni viongozi wa serikali ya DARUSO 1989 hadi 1992 na mashujaa wa wakati huo waliotetea hadhi ya chuo na kuikosoa serikali ya Rais Mwinyi Nkurumah Hall, hadharani na kwenye magazeti. Tume ya Jaji Koroso iliyopewa jukumu la kuchunguza mgogoro huo haikukuta mwanafunzi yeyote na hatia. Rais Mwinyi alitusamehe kama baba na sisi kama watoto tukamwomba msamaha yakaisha . Yale yote tuliyopigania yafanyike, ndiyo yanafanyika sasa chini ya serikali ya awamu ya tano. Sasa utapingaje mtu anayefanya yale unayotaka yafanyike? POLE SANA NDUGU YANGU KWA KUDANGANYWA!
Kuna walio nje ya nchi,usalama wao uko hatarini wanaomba regime iwahakikishie na wao haki ya kuishi iliyotaka kuporwa ili warudi,regime haitaki kuiga aliyoyafanya MZEE mwinyi enzi hizo( kutoa msamaha kama baba vs Mwana mpotevu). Shida inaanzia hapo.
 
Kusema madhaifu yake(mwalimu) siyo kumchukia,ni kubainisha ubinadamu wake. Kila binadamu hukosea/si mkamilifu.
Ukikutana na Binadamu / Mtu anamchukia kabisa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere basi jua ya kwamba huyo si tu kwamba atakuwa ni ' Mpumbavu / Popoma ' lakini pia ni lazima tu atakuwa na Matatizo makubwa mno ya Akili ( Fikra ) na huenda hadi muda huu alipaswa / alitakiwa awe ameshawahishwa Hospitali ya Wagonjwa wa Akili pale Mirembe Mji Mkuu Mkoani Dodoma. R.I.P Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Burito Nyerere.
 
Hakuna aliesema Nyerere alikuwa Mungu ,wewe ndo umeweka kwenyr heading hivyo

Japo kuna wanaotaka kumtangaza mtakatifu, wana sababu zao, na utaratbu wao na maana yao ya utakatifu ambayo inawezekana mimi siielewi au sikubalian nayo ila siwez ingilia maamuzi yao


Ila ni kweli kuwa Nyerere alikuwa wakipekee, kama tu ambavyo hata mimi na wewe tu wakipekee

Kila binadamu ana element za upekee, tunachozidianaga ni wengine wanaishi maisha yao yote bila kuactivate eneo hilo la upekee, ni kwa sababu ya kuishi kwa mkumbo na kufuata watu wanavyosema

Sasa Nyerere alifanikiwa kuactivate maeneo yake ya upekee, yanayomtofautisha na watu wengine

Jpm aliefanikiwa pia nae kwa muda mfupi, ameonesha dunia waziwazi eneo lake la upekee

Na kwa bahat mbaya au nzuri, katika eneo la upekee la Mwalimu na Eneo la upekee la JPM kuna visimilarity

Na ndo maana wengi wanaona JPM anafananishwa na Mwalimu

Ila katika conclusions ni kuwa Mwalimu alikuwa mtu pekee kama ambavyo JPM ni mtu pekee ila wanashahibiana
 
Umewasiliana naye kwa mara ya mwisho lini rafiki yako mungu akakueleza hayo unayoyaeleza hapa..
Ukiwasiliana naye tena, mwambie watu wapo bize na misheni zao, na kwamba hawana mida ya kusikiliza wavuta bangi.
Usisahau kufikisha salaam nyingi toka kwa kalamu1.
Naamini katika vitabu takatifu hakuna alie mbora kumzidi mungu kamahuamini basi jaribu wewe tuone kama hutotoka katika dunia hii
 
kwa nini unajichanganya mwenyewe? yaelekea huelewi unachochangia mwenyewe. unataka tuelewe unachoelezea wakati wewe mwenyewe huelewi unatueleza nini! unaonekana typical mtz. jambo dogo kulifanya kubwa na jambo gumu kuwa rahisi. utamsikia mtz akimalizia kwa ' si unajua?' najua nn? nilifikiri kwa kiingereza chako kizuri una kainfluence ka Kenya. nilikosea huna!
tukisema fulani ni baba/babu/mjomba wake mtupu, unaelewa? wengine wanatukatalia na kutoa sababu. wakati mwingine tunajiona tumekosea baada ya maelezo yao. tunakubali kushindwa. hatuwaambii kwamorphous fanya hao wazazi miungu-watu! hayo mambo ya sura,tabia, nk watoto kufanana au kutofanana na wazazi wao kama binadamu. rahisi sana tena sana. no complication.
kufanana au kutofanana kwa Magufuli na Nyerere sio kwa sura, akili, nk. hata hilo walitofautiana. mmoja alikufa akiwa bado handsome na uzee alokuwa amefikia. huyu mwingine ni amorphous ( natumia that terminology rahisi kwa chemist kuelewa). pengine kueleweka zaidi kwa vile wote wawili uhusishwa na nchi jirani yenye wahutu na watutsi, walitoka makabila tofauti. tunazungumzia statesmanship yao. yatosha tu kukwambia rejea hotuba zao kuhusu kuhamia Dodoma. there's no comparison but only contrast between them. unazunguka tu. mahaba yako kwa wa sasa yanakufanya umfananishe na yule. hutaweza. UTA's hinder tu. malengo yao ya dhati na approaches in tofauti sana
Utahangaika bure na huyo Matiko Matare. He's not mentally fit!
 
Naamini katika vitabu takatifu hakuna alie mbora kumzidi mungu kamahuamini basi jaribu wewe tuone kama hutotoka katika dunia hii
Mbona ni rahisi sana kuelewa nilichoandika katika ujumbe uliopita, ni kipi kigumu hapo hadi ushindwe kukielewa na kuendelea kumng'ang'ania 'mungu' kama mali yako?
Ni lini alikutuma ukawatishie watu wengine wewe unaoona hawafai 'mungu' wako awasikilize?

Kama 'mungu' sio mali yako, je, kakutuma wewe uje kuwatishia watu hapa, kama hivi "...kama huamini basi jaribu wewe tuone kama hutotoka katika dunia hii."
Nikikwambia kwamba Mungu ninayemuamini na kumwabudu mimi ni rafiki yangu mkubwa, wewe utabisha?
 
MWL. NYERERE HAKUWA MUNGU
Kudai kwamba Nyerere hawezi kufananishwa na mtu yeyote ni ajali kubwa sana kuliko ajali ya M.V Bukoba ziwa Viktoria na Treni kule Dodoma zilizosababisha maafa makubwa katika nchi yetu.Ni ajali kwa sababu kauli hii inaweza kuua kifikira vijana wengi ambao hawaijui historia ya nchi yetu.Hii ni kwa sababu;
  • Binadamu yeyote anafanana na mwingine kwamba wote wanazaliwa, wananyonya, wanakufa na pia wanaweza kufanana kwa mawazo au matendo ndiyo maana watu wanakuwa katika imani moja ya dini na itikadi mbalimbali ambazo zimeundwa na watu wanaofanana katika imani na itikadi hizo.Kauli hii inaukana ubinadamu wa Nyerere na kumweka katika daraja la malaika au Mungu. Nyerere alikataa jambo hil na hata hakutaka kuitwa mtukufu kwani alijua utukufu ni wa Mungu tu. Alipenda aitwe ‘’Ndugu Rais au Mwalimu’’
  • Kusema Nyerere hafanani na mtu yeyote ni kufuru kwa Nyerere mwenyewe na aibu kubwa kwa msemaji.Nyerere katika kitabu chake cha UJAMAA anasema “Hakuna binadamu asiyekosea (No man is infallible)”. Mwaka 1971 aliandika kitabu kidogo kinaitwa TUJISAHIHISHE na wakati anang’atuka urais alisema yeye si malaika na hata malaika mkuu Gabriel angepewa Tanzania kuongoza asingemaliza matatizo yake yote.Hii ina maana alikiri alikuwa na mapungufu kama binadamu yeyote. Hivyo, kusema hawez kufananishwa na mtu mwingine ni dhambi kubwa.
  • Baada ya uhuru mwaka 1961, serikali ya Nyerere mwaka 1965 ilifuta vyama vingi na kuunda katiba ya chama kimoja (mono-party system) na chama cha TANU kikashika hatamu (party- supremacy). Mwalimu Nyerere aliendelea kugombea chaguzi za urais kwa kutumia picha yake na kivuli. Mpiga kura alitakiwa kuweka tiki kwenye picha ya Nyerere au kwenye kivuli. Ndiyo demokrasia mnayotaka Mh. Magufuli afanye ili afanane na Nyerere? Mko tayari mh. Magufuli akifanana na Nyerere katika hilo?
  • Nyerere hakuleta vyama vingi. Vyama vingi vilianza zamani sana katika mataifa ya Ulaya magharibi lakini katika mataifa ya ulaya mashariki vilianza baada kuanguka kwa ukomunisti wa Urusi chini ya utawala wa Mikael Gorvachev na sera zake za ‘’Perestroika na Glassnots. Wimbi hili la kuvunjika kwa ukominist na kutaka mfumo wa vyama vingi lilikuwa kubwa sana kiasi cha kuathiri nchi nyingine. Nyerere alisoma majira akaona asipokubali hapa atalazimishwa na nguvu za nje ikawa ni aibu. Hivyo, akatangulia kusema kuzungumzia vyama vingi si dhambi tena. Nchi nyingine za Afrika ambazo hazikuwa zimeanza kama Kenya na Uganda zililazimishwa na mataifa makubwa kuingia mfumo wa vyama vingi na ilikuwa ni aibu kwao.Katika kupiga kura tuwe na vyama vingi au kimoja katika Tanzania, asilimia themanini (80%) ya watanzania walichagua chama kimoja lakini Nyerere kwa kuona hali halisi wakati huo alishawishi serikali ya Mwinyi ikubali kuwa na vyama vingi na kwa kuwa yeye ndiye alikuwa mwenyekiti wa chama, serikali ilikubali.Tusipotoshe vijana wetu, tuwafundishe ukweli kuhusu nchi yao.
  • Nyerere alitaka vyama vingi visimpotezee muda wa kujenga taifa akavifuta, Magufuli anataka vyama visiwapotezee muda wananchi ili watumie muda huo kujenga uchumi wetu na amevipa muda wa kufanya siasa na namna ya kufanya siasa hizo.Hapo ni nani afadhali?
  • Matumizi ya vyombo vya dola yapo dunia nzima na kusudi la vyombo vya dola (State apparati) kuzaliwa duniani ni kulinda tabaka tawala (The dominant class) na tabaka tawala ndilo linaamua vifanye nini, wapi, lini na kwa namna gani kulingana na mazingira yaliyopo.Hii hutofautiana kutoka nchi moja hadi nyingine. Karl Marx na Lenin walitabiri kuwa dola zingetoweka duniani(withering away of states) lakini halikutokea. Nyerere alikwisha kusema dola ni chombo cha mabavu ni sheria,polisi,mahakama ,magereza na majeshi. Hivyo usitarajie kubembelezwa na dola unapotishia usalama wake.
Kwan ww unataka kumfananisha na nani? Au kisa unalala, kula na kunya bila shda ndo maana unaongea utumbo. Nenda kambi za wakimbizi kisha fuatilia historia ya mwalimu.
 
Kwani yeye alijiita Mungu au watu ndio wanamuita

Katika philosophy kuna Dini ya ABRAHAMIC RELIGIOUS na Non ABRAHAMIC RELIGIOUS

ABRAHAMIC RELIGIOUS are descendant of Abraham it includes Islamic, Christians, na Judaism, Hawa Wako kundi la MONOTHEISM Wanaamini kama Mungu mmoja

NON ABRAHAMIC RELIGIOUS ni watu wanaoamini Katika Miungu wengi, Hawa huitwa POLYTHEISM

Sasa watu wakimuabudu NYERERE kama Mungu wao Wako sahihi Hawajakosea

Usiwalazimishi wote waamini Katika Mungu wa Ibrahim
 
Mbona ni rahisi sana kuelewa nilichoandika katika ujumbe uliopita, ni kipi kigumu hapo hadi ushindwe kukielewa na kuendelea kumng'ang'ania 'mungu' kama mali yako?
Ni lini alikutuma ukawatishie watu wengine wewe unaoona hawafai 'mungu' wako awasikilize?

Kama 'mungu' sio mali yako, je, kakutuma wewe uje kuwatishia watu hapa, kama hivi "...kama huamini basi jaribu wewe tuone kama hutotoka katika dunia hii."
Nikikwambia kwamba Mungu ninayemuamini na kumwabudu mimi ni rafiki yangu mkubwa, wewe utabisha?
Kazi kwako wewe narafiki yako niache mimi na muabudiwa sio rafiki yangu mimi namuita muabudiwa
 
Unamwabudu huku ukimwogopa? Ukimtumia kuwatisha watu wengine?
Sijui watu wengine wanawaza nini aukwakutumia nini chanzo kilikuwa ni mwalimu kumuita mtakatifu mimi nikasema mtakatifu nimungu pekee sintomwita mungine jina hilo isipokuwa mungu tu sasa hapo namtisha nani kifupi ndugu ukipenda uamini au ukufuru
 
Mwalimu Nyerere alikataa kuitwa Mheshimiwa Rais badala yake aitwe NDUGU na kila mtanzania awe addresed ndugu sio bibi na mabwana
 
Back
Top Bottom