Joseph Matiko Matare
Member
- Oct 14, 2019
- 19
- 16
- Thread starter
- #21
NI MIMI.Punch kilikuwa ni kikundi kisichojulikana ambacho hakikuwa na jukwaa la kusemea na hakikujulikana tangu mwaka 1961 UDSM ilipoanza kilikuwapo kukosoa uongozi wa chuo na serikali bila kujulikana. Matiko Matare, Rudovick Bazigiza, James Mbatia, Mosene Nyambabe, Antony Komu ,Kangi Lugola, Harun kimaro, Ally Salehe na Dr.Kebwe walikuwa ni viongozi wa serikali ya DARUSO 1989 hadi 1992 na mashujaa wa wakati huo waliotetea hadhi ya chuo na kuikosoa serikali ya Rais Mwinyi Nkurumah Hall, hadharani na kwenye magazeti. Tume ya Jaji Koroso iliyopewa jukumu la kuchunguza mgogoro huo haikukuta mwanafunzi yeyote na hatia. Rais Mwinyi alitusamehe kama baba na sisi kama watoto tukamwomba msamaha yakaisha . Yale yote tuliyopigania yafanyike, ndiyo yanafanyika sasa chini ya serikali ya awamu ya tano. Sasa utapingaje mtu anayefanya yale unayotaka yafanyike? POLE SANA NDUGU YANGU KWA KUDANGANYWA!Wewe ni mtoto wa Matiku Matare? Yule aliyeleta matata na kumtukana Mzee Mwinyi kwa kujificha kwenye kichaka cha Mzee Punch pale Chuo Kikuu cha Manzese? Wakati huo akiwa na wenzake kina Bazigiza, Mbatia, Ally Salehe na wengine?