Mwl. Nyerere aliwahi kutuasa

Mwl. Nyerere aliwahi kutuasa

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2008
Posts
10,942
Reaction score
437
Haya ni maneno ha mwl nyerere. Mwaka 1995.

"ni vizuri wakasikiliza wananchi wanasemaje.msidhani kwamba tutashinda bila kuwasikiliza wananchi. Hamteui katibu wa chama bali rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania kwa hiyo ni vizuri kusikiliza maoni ya wananchi. Chama kitakachopuuza maoni ya wananchi kitahangaika kufuta machozi na hakitopata wa kukisaidia kuyafuta kamwe.

Kama wote ni sawa ila wananchi wanampenda mmoja kuliko mwingine basi huyo wanayempenda ni anayefaa zaidi."
 
Mwalimu alisema tuwasikilize wananchi.lakini hakusema tuwape pesa halafu tujidanganye kwamba wanatupenda la hasha.wanapenda pesa lakini si mtu. Kwa hiyo Lowasa hapendwi inapendwa pesa yake.
 
Yeye lini alitowa fursa ya maoni ya wananchi?
 
Kwa bahati mbaya sana Lowasa hajawahi kuwa sawa na wagombea wengine. Lowasa ni fisadi mkubwa kuliko wengine. Kwa kigezo hicho tunamuondoa mapema then tuwalinganishe waliobaki
 
Kwa bahati mbaya sana Lowasa hajawahi kuwa sawa na wagombea wengine. Lowasa ni fisadi mkubwa kuliko wengine. Kwa kigezo hicho tunamuondoa mapema then tuwalinganishe waliobaki

Nyie watu mnanishangaza sana hakiyanani!!!

Wakati wengine tulipokuwa tunaeleza madudu ya hao watu, mlitetea kwa nguvu uovu wao.

Mkatuita sie wanywa viroba, tumechanganyikiwa.
Leo hii nyie wenyewe mmeamua kula matapishi yenu.

Ndani ya CCM hakuna msafi, hakuna muadilifu,hakuna mzalendo.
Wote ni mafisadi.
 
Hatuchagui umaarufu wa mtu ,tunamchagua mtu safi!!
 
suzan lema

Alichosema nyerere ni baada ya kuwa mshachuja na kuwatoa waliochafuka woote kama Lowasa ndio sasa mnaanza kuangalia miongoni mwa wasafi ni yupi anakubalika na wananchi. Lakini hakumaanisha mradi mtu anatumia pesa kulazimisha aonekane anakubalika basi ndo apitishwe tu kwa hadaaa , nyerere hakumaanisha hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Enl nje hata kama anapendwa na watz wooote ?????
 
Kwa bahati mbaya sana Lowasa hajawahi kuwa sawa na wagombea wengine. Lowasa ni fisadi mkubwa kuliko wengine. Kwa kigezo hicho tunamuondoa mapema then tuwalinganishe waliobaki
Halafu we bwana una Chuki Binafsi sana. Nakuona sana Kwenye comment zako. Yaani ile Chuki kabisa pasee..!
 
Kama yepi? hatutaki maneno matupu weka ushahidi

vip unakubaliana na maneno aliyoyasema madabida Kuwa lowasa ni sawa na mtume SAW?kama hapana una maoni gan juu ya ccm na lowasa
 
Back
Top Bottom