Ninalaani kitendo cha kumuua mtu wakati mmemkamata na hana uwezo wowote wa kuwadhuru.
Hivi ni mahakama gani imemhukumu kuwa ni mwizi?
Na hao waliomuua, wanauhakika gani kwamba kukutwa kwake hata kama yuko na wezi naye ni mwiiz?
Mara ngapi watu wanakodishwa na watu kuwasaidia usafiri ukizingatia hali ngumu ya maisha?
Mara ngapi watu wanapewa lift halafu mtoa lift anasema, anapitia sehemu anashguhuli kabla ya kuendelea na safari?
Acheni kabisa kumwaga damu za watu hivyo. Mnatengeneza laana kwa mikono yenu.
Ninyi mnadani kwa nini wenziye walikimbia yeye akabaki?
Mtasema nini juu ya damu yake huyu mtu, ikiwa alibaki kwa kuwa hakuwa akifahamu mpango wa hao wengine?
Damu za watu wasioa na hatia zitalia juu ya ardhi ya Tanzania na nchi italaaniwa.
Ninawambea watoto wenu ninyi mliomuua mtu bila kuhukumiwa wala kupewa nafasi ya kusikilizwa, kwamba gadhabu ya Mungu isije kuwaka juu yao.
Nanyi watanzania mnaofurahia mauaji ya watu bila trials, naomba muungame nia hizo ovu mbele za Mungu. La sivyo, msije mkashangaa mabalaa yatakayowaandama kuanzia sasa. Amani itakuwa mbali nanyi.
Mungu hapendi umwagaji damu za watu kwa kuwa damu ni uhai na uhai unatoka kwa Mungu pekee.
Acheni kabisa dhambi na ukatili huo.
Naomba Mungu kwa ajili ya mimi na uzao wangu, pamoja na watu wote wanaochukia uovu huu, na wanaotubu na kuacha Mungu awarehemu, ili atakapoipiga nchi kwa gadhabu yake,, sisi aturehemu. Tusiwe na sehemu katika mapigo hayo.