Hawana alternatives...
Usishangae mkuu,hawa ndo "vigoli chuchu saa sita" wa nyinyiemu na wengine ni "manung'ayembe"....kwi kwi kwi kwiiiiii.duh! CCM hawajifunzi tu kurudia kula matapishi?
Nchemba
Wassira
Lusinde
Umeona eeehWakiambiwa chama kinakufa wanapiga kelele, kama mtu aliyewagharimu mara mbili katika kipindi kifupi bado wanampa tena hiyo kazi... This is not a good sign at all. Kama vipi wampeleke mwenyekiti wao anaesema chama bado kiko hai sana.
Migomba ina rangi gani.. Kijaniii......
Majani yana rangi gani ,,kijaniii....
Bangi ina rangi gani,,,
Kipenga kimelia jimbo la Sumbawanga Mjini. Ni baada ya Mahakama ya Rufani Tanzania kutupilia mbali rufaa ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM,Hilary Aeshi. Kwa mujibu wa Sheria za Uchaguzi,ndani ya siku 90,uchaguzi mdogo utafanyika. Mahakama ya Rufani ndiyo Mahakama ya mwisho.Jana,jimbo la Sumbawanga Mjini limekuwa wazi rasmi.
Baada tu ya uamuzi huo wa Mahakama ya Rufani, wazito wa CCM waliitana Ofisi Ndogo za CCM-Dar es Salaam kwa kikao cha dharura. Kikao kilianza saa 2.00 usiku na kuisha saa 6.30 usiku. Kilikuwa na vigogo wa juu wa CCM wakiwemo baadhi ya Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM. Ajenda ilikuwa ni Uchaguzi wa Sumbawanga Mjini.
Katika kikao hicho ambacho nami shushushu huru nilikuwemo,timu ya Kampeni ilipangwa kabisa. Itaoongozwa na Mwigulu Lameck Nchemba,Mbunge wa Iramba Mashariki-CCM. Mwigulu atasaidiwa na timu inayoundwa na vijana wengi wa Sumbawanga Mjini waliobatizwa jina la 'Watoto wa Nyumbani'. Watia nguvu watakuwa akina Wassira,Firikunjombe na Lusinde. Fomu zitaanza kutolewa mwezi huu mwishoni.
Hatahivyo, UVCCM wametakiwa kukaa mbali na uchaguzi huo kwakuwa kwasasa hawana picha nzuri kwa jamii kutokana na kile kinachoendelea katika chaguzi zao. Ningweza kuandika mengi.Lakini nina 'hang-over' ya mkutano wa Lumumba.Kumekucha!