VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Kipenga kimelia jimbo la Sumbawanga Mjini. Ni baada ya Mahakama ya Rufani Tanzania kutupilia mbali rufaa ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM,Hilary Aeshi. Kwa mujibu wa Sheria za Uchaguzi,ndani ya siku 90,uchaguzi mdogo utafanyika. Mahakama ya Rufani ndiyo Mahakama ya mwisho.Jana,jimbo la Sumbawanga Mjini limekuwa wazi rasmi.
Baada tu ya uamuzi huo wa Mahakama ya Rufani, wazito wa CCM waliitana Ofisi Ndogo za CCM-Dar es Salaam kwa kikao cha dharura. Kikao kilianza saa 2.00 usiku na kuisha saa 6.30 usiku. Kilikuwa na vigogo wa juu wa CCM wakiwemo baadhi ya Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM. Ajenda ilikuwa ni Uchaguzi wa Sumbawanga Mjini.
Katika kikao hicho ambacho nami shushushu huru nilikuwemo,timu ya Kampeni ilipangwa kabisa. Itaoongozwa na Mwigulu Lameck Nchemba,Mbunge wa Iramba Mashariki-CCM. Mwigulu atasaidiwa na timu inayoundwa na vijana wengi wa Sumbawanga Mjini waliobatizwa jina la 'Watoto wa Nyumbani'. Watia nguvu watakuwa akina Wassira,Firikunjombe na Lusinde. Fomu zitaanza kutolewa mwezi huu mwishoni.
Hatahivyo, UVCCM wametakiwa kukaa mbali na uchaguzi huo kwakuwa kwasasa hawana picha nzuri kwa jamii kutokana na kile kinachoendelea katika chaguzi zao. Ningweza kuandika mengi.Lakini nina 'hang-over' ya mkutano wa Lumumba.Kumekucha!
Baada tu ya uamuzi huo wa Mahakama ya Rufani, wazito wa CCM waliitana Ofisi Ndogo za CCM-Dar es Salaam kwa kikao cha dharura. Kikao kilianza saa 2.00 usiku na kuisha saa 6.30 usiku. Kilikuwa na vigogo wa juu wa CCM wakiwemo baadhi ya Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM. Ajenda ilikuwa ni Uchaguzi wa Sumbawanga Mjini.
Katika kikao hicho ambacho nami shushushu huru nilikuwemo,timu ya Kampeni ilipangwa kabisa. Itaoongozwa na Mwigulu Lameck Nchemba,Mbunge wa Iramba Mashariki-CCM. Mwigulu atasaidiwa na timu inayoundwa na vijana wengi wa Sumbawanga Mjini waliobatizwa jina la 'Watoto wa Nyumbani'. Watia nguvu watakuwa akina Wassira,Firikunjombe na Lusinde. Fomu zitaanza kutolewa mwezi huu mwishoni.
Hatahivyo, UVCCM wametakiwa kukaa mbali na uchaguzi huo kwakuwa kwasasa hawana picha nzuri kwa jamii kutokana na kile kinachoendelea katika chaguzi zao. Ningweza kuandika mengi.Lakini nina 'hang-over' ya mkutano wa Lumumba.Kumekucha!