Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,565
- 7,993
Salam ndugu wanaJF.
Miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia vijana wengi wakishawishika kujiunga katika shughuli za kisiasa hapa nchini. Mwamko huo wa vijana kujiunga katika shughuli za kisiasa umepelekea vyama vya kisiasa kutafuta namna bora ya kuwavutia na kuwashawishi vijana kujiunga na vyama vyao.
Kutokana na vuguvugu kubwa la vijana kujihusisha na masuala ya siasa, vyama vya siasa hapa nchini hasa vyenye ushindani mkubwa hapa nchini CHADEMA, CUF na CCM vimejikuta vikilazimika kuwateua vijana mahiri katika vyama vyao katika nafasi za juu za uongozi wa kitaifa.
Chadema walimteua Zitto Kabwe kuwa naibu katibu mkuu bara, CUF kwa upande wao wamemteua Julis Mtatiro kuwa naibu katibu mkuu bara huku CCM nao wakimteua Mwigulu Nchemba kuwa naibu katibu mkuu bara. Wote hawa ni vijana walioaminiwa na kuteuliwa na vyama vyao ili watumie ushawishi wao na umahiri wao katika kuwavuta vijana wengi zaidi kujiunga na vyama vyao. Kitu kimoja cha kufurahisha ni kwamba vijana hawa ambao wote ni mahiri sana katika vyama vyao, wote wameteuliwa kushika wadhifa unaofanana/unaolingana-Naibu katibu mkuu!!!
Vyama vyetu vya siasa vimekuwa vikipitia katika vipindi tofauti tofauti vya mlipuko na hamasa za kisiasa, na hasa vinapokuwa vikubwa na kujikusanyia wafuasi wa kila aina; vijana, wazee, akina mama, watu wa makamo, wataalamu waliobobea katika Nyanja mbalimbali na watu wengine wa kawaida. Katika kukua huku kwa vyama vya siasa changamoto mbalimbali zimekuwa zikijitokeza siku moja hadi nyingine. Wajibu wanaokuwa nao viongozi wa chama husika ni kuwa na uwezo wa kupambana, kuhimili na kukabiliana na changamoto zozote zinazojitokeza kwa kushirikiana (collective responsibility).
Ili kushadidia hoja yangu naomba nimtumie naibu katibu mkuu wa ccm ndugu Mwigulu Nchemba. Pamoja na kwamba sina mapenzi yoyote na ccm na sijawahi kuwaunga mkono kwakuwa sasa ni zaidi ya miaka 50 wanatuongoza tanguntupate uhuru lakini tunachoshuhudia ni wananchi kuendelea kuwa masikini lakini pia hali ya usalama wa wananchi na mali zao umeendelea kuwa shakani kwani tumeshuhudia mauaji ya hapa na pale kwa wananchi wasiokuwa na hatia.
Mauaji mengine yamekuwa yakifanywa na vyombo vya dola lakini pia mauaji mengine yamekuwa yakifanywa na majambazi kama ilivyotokea kwa Dr. Mvungi hivi karibuni pamoja na Prof. Mwaikusa na watanzania wengine wengi ambao wameuwawa kikatili kwasababu ya ulegelege wa serikali ya ccm kushindwa kuwahakikishia wananchi wake ulinzi wa maisha yao na mali zao.
Pamoja na kushuhudia ccm ikipita katika misukosuko mingi yenye migawanyiko mingi ndani ya chama lakini viongozi wake wameweza kumudu kuwa na mshikamano wa kushangaza, hata kama unaweza kuuita ni mshikamano wa kinafiki lakini umekuwa ukiwasaidia kukivusha chama chao katika changamoto mbalimbali.
Mara zote tunapokaribia uchaguzi mkuu wa nchi au uchaguzi ndani ya ccm tumekuwa tukishuhudia makundi mengi yakijitokeza kushindana na hata kufikia mahali pa kutishia uhai wa chama chao, hadi baadhi ya watu kudhani kwamba ccm inameguka kama si kupasuka. Pamoja na kuwepo na makundi ya uchaguzi kila mara lakini kama nilivyotaja awali ni kwamba makundi hayo yamekuwa yakiendesha siasa za hatari lakini bila kukiumiza chama chao.
Mathalani siku za hivi karibuni tumeshuhudia makundi mbalimbali yakijipanga kwa ajili ya uraisi wa JMT mwaka 2015. Tumeshuhudia kundi la Edward Lowasa wakiwa busy kumuuza mgombea wao, na hivi karibuni tunasubiri kuona watu wakienda kula nyama choma Monduli. Kwa upande mwingine kuna kundi la Bernard Membe, na upande mwingine tena kuna kundi la Samwel Sitta. Pia kumekuwa na miunganoya makundi mbalimbali ambayo nimekuwa nikiyasikia yakitajwa yakijipanga kuhakikisha kwamba wagombea wao ndio wanaopata fursa ya kupitishwa kupeperusha bendera ya ccm come 2015.
Pamoja na kuwepo minyukano ya mara kwa mara ndani ya ccm lakini hatujawahi kushuhudia viongozi wa juu wa ccm; Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Manaibu Makatibu Wakuu na Katibu Mwenezi , mmoja wao au wawili miongoni mwao wakifanya kazi za kiofisi za chama chao kupitia vyombo vya habari.
Kwa mfano Mwigulu Nchemba ambaye vijana wengi sana wa ccm wanamuamini na kumtumainia sana kwamba ndiye anayeweza kuwanusuru na kipigo cha upinzani katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015 amekuwa akitajwa kumuunga mkono Edward Lowasa. Na kwakuwa Mwigulu anamuunga mkono Lowasa basi ni dhahiri kuwa asingependa kuona mgombea wake akiendelea kusakamwa na kuchafuliwa na wanaccm wenzake wanaopingana nae ama kushindana nae.
Katika mazingira hayo ni dhahiri kuwa Mwigulu amekuwa akiwasiliana na bosi wake-Katibu mkuu Kinana katika kuwashauri au kutafuta maelezo au ufafanuzi wa mambo mbalimbali yanayokikumba chama chao. Katika kuwasiliana huko ni wazi kuwa amekuwa akiwasiliana kwa ukaribu zaidi na katibu mkuu wake Kinana na akimsaidia kwa ukaribu katika kutekeleza majukumu yake kwakuwa yeye (Mwigulu) ndiye msaidizi wa karibu zaidi kwa Kinana. Katika kuwasilaiana na Kinana bila shaka amekuwa akitumia njia mbalimbali za mawasiliano kama vile kuzungumza nae ana kwa ana, ama akizungumza nae kwa simu, ama anawasiliana nae kwa barua/barua pepe au fax na njia nyingine za mawasiliano zinazokubalika kiofisi.
Hata mara moja sijawahi kumsikia ama kumuona Mwigulu Nchemba akitoka hadharani kwenye vyombo vya habari na kuuambia umma wa watanzania aidha kupitia press release, au kupitia mitandao ya kijamii, au kupitia magazeti, au television na radaio kwamba amemuandikia rasmi katibu mkuu wake Kinana kumuomba ufafanuzi au maelekezo ya jambo Fulani linalomhusu kiongozi mmoja wa chama chao.
Pamoja na kushuhudia mashambulizi mengi dhidi ya Lowasa kutoka kwa wanaccm wenzake, tena wakati mwingine Lowasa ameshambuliwa hadharani na viongozi wakubwa wa ccm lakini sijawahi kumuona Mwigulu akitoka kwenye vyombo vya habari na kututangazia kwamba amemuandikia barua Katibu mkuu wake Kinana atoe taarifa ya kukanusha mashambulizi yaliyofanywa dhidi ya Lowasa ama akiri kwamba kiongozi huyo (aliyemshambulia Lowasa) ametoa matamshi hayo kwa niaba ya chama hivyo wanachama wa ccm na wananchi kwa ujumla watambue kuwa huo ndio msimamo wa ccm juu ya kada wake Lowasa.
Nionachoamini ni kwamba Mwigulu amekuwa akiwasiliana kwa karibu sana na katibu mkuu wake Kinana katika kumsaidia kutekeleza majukumu yake, ni dhahiri kuwa Mwigulu amekuwa akiitumia ofisi yake ya naibu katibu mkuu pale Lumumba na Dodoma katika kutekeleza majukumu yake ya unaibu katibu mkuu wa ccm. Ni dhahiri kuwa Mwigulu amekuwa akimuandikia barua rasmi za kiofisi kumhoji juu ya mambo Fulani yenye mwelekeo wa kukimuiza chama chao ama viongozi wao ama wanachama wao, lakini kama nilivyogusia tangu hapo awali sijawahi kumuona akivujisha barua zake hizo katika vyombo vya habari kwa sababu iwayo yoyote ile.
Kutokana na mazingira hayo na kutambua kwamba Mwigulu amekwisha kuchagua upande anaouunga mkono (Lowasa), lakini pia naye amekuwa akitajwa kwamba anafikiria kujitosa katika kinyanganyiro cha uraisi (huenda ni alternative choice incase bid ya Lowasa imekwama), bila shaka amekuwa akipambana ndani ya ccm kuhakikisha kuwa jina lake na la mgombea wake hayachafuliwi bila sababu za msingi.
Kwa mantiki hiyo basi nimekuwa nikitamani sana kumuona ama kumsikia ama kumsoma Mwigulu Nchemba akitoa press release, au akiandika katika mitandao ya kijamii kwamba amemuandikia rasmi barua katibu mkuu wake Kinana kutaka maelezo ama ufafanuzi wa hoja kwamba viongozi na wanachama wa ccm wanaomshambulia mgombea wake hadharani kwa kumhusisha na kashfa mbalimbali za ufisadi na zinazoonyesha dhahiri zinamchafua kiongozi huyo.
Kwakuwa Mwigulu anaungwa mkono na vijana wengi ndani ya ccm, na kwakuwa vijana wengi wa ccm wanamuunga mkono Lowasa katika mbio zake za kuwania uraisi, na kwakuwa kuna baadhi ya viongozi wa ccm tena wengine wa kitaifa wamekuwa wakiendelea kumchafua Lowasa, na kutokana na kuendelea kuongezeka kwa upinzani ndani ya ccm dhidi ya Lowasa ni dhahiri kuwa muda si mrefu tutamshuhudia Mwigulu Nchemba akitujuza ni kwa kiwango gani amepambana kuhakikisha kuwa jina la mgombea wake halichafuliwi na atatufahamisha ni barua ngapi amemuandikia Kinana akimtaka atoe tamko la kukubali ama kukanusha taarifa zote zinazoandikwa ama kuchapishwa zikimshambulia Lowasa. Ninausubiri wakati huo kwa hamu sana kwakuwa muda si mrefu tutayashuhudia maajabu hayo yakitokea.
Nawasilisha.
Miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia vijana wengi wakishawishika kujiunga katika shughuli za kisiasa hapa nchini. Mwamko huo wa vijana kujiunga katika shughuli za kisiasa umepelekea vyama vya kisiasa kutafuta namna bora ya kuwavutia na kuwashawishi vijana kujiunga na vyama vyao.
Kutokana na vuguvugu kubwa la vijana kujihusisha na masuala ya siasa, vyama vya siasa hapa nchini hasa vyenye ushindani mkubwa hapa nchini CHADEMA, CUF na CCM vimejikuta vikilazimika kuwateua vijana mahiri katika vyama vyao katika nafasi za juu za uongozi wa kitaifa.
Chadema walimteua Zitto Kabwe kuwa naibu katibu mkuu bara, CUF kwa upande wao wamemteua Julis Mtatiro kuwa naibu katibu mkuu bara huku CCM nao wakimteua Mwigulu Nchemba kuwa naibu katibu mkuu bara. Wote hawa ni vijana walioaminiwa na kuteuliwa na vyama vyao ili watumie ushawishi wao na umahiri wao katika kuwavuta vijana wengi zaidi kujiunga na vyama vyao. Kitu kimoja cha kufurahisha ni kwamba vijana hawa ambao wote ni mahiri sana katika vyama vyao, wote wameteuliwa kushika wadhifa unaofanana/unaolingana-Naibu katibu mkuu!!!
Vyama vyetu vya siasa vimekuwa vikipitia katika vipindi tofauti tofauti vya mlipuko na hamasa za kisiasa, na hasa vinapokuwa vikubwa na kujikusanyia wafuasi wa kila aina; vijana, wazee, akina mama, watu wa makamo, wataalamu waliobobea katika Nyanja mbalimbali na watu wengine wa kawaida. Katika kukua huku kwa vyama vya siasa changamoto mbalimbali zimekuwa zikijitokeza siku moja hadi nyingine. Wajibu wanaokuwa nao viongozi wa chama husika ni kuwa na uwezo wa kupambana, kuhimili na kukabiliana na changamoto zozote zinazojitokeza kwa kushirikiana (collective responsibility).
Ili kushadidia hoja yangu naomba nimtumie naibu katibu mkuu wa ccm ndugu Mwigulu Nchemba. Pamoja na kwamba sina mapenzi yoyote na ccm na sijawahi kuwaunga mkono kwakuwa sasa ni zaidi ya miaka 50 wanatuongoza tanguntupate uhuru lakini tunachoshuhudia ni wananchi kuendelea kuwa masikini lakini pia hali ya usalama wa wananchi na mali zao umeendelea kuwa shakani kwani tumeshuhudia mauaji ya hapa na pale kwa wananchi wasiokuwa na hatia.
Mauaji mengine yamekuwa yakifanywa na vyombo vya dola lakini pia mauaji mengine yamekuwa yakifanywa na majambazi kama ilivyotokea kwa Dr. Mvungi hivi karibuni pamoja na Prof. Mwaikusa na watanzania wengine wengi ambao wameuwawa kikatili kwasababu ya ulegelege wa serikali ya ccm kushindwa kuwahakikishia wananchi wake ulinzi wa maisha yao na mali zao.
Pamoja na kushuhudia ccm ikipita katika misukosuko mingi yenye migawanyiko mingi ndani ya chama lakini viongozi wake wameweza kumudu kuwa na mshikamano wa kushangaza, hata kama unaweza kuuita ni mshikamano wa kinafiki lakini umekuwa ukiwasaidia kukivusha chama chao katika changamoto mbalimbali.
Mara zote tunapokaribia uchaguzi mkuu wa nchi au uchaguzi ndani ya ccm tumekuwa tukishuhudia makundi mengi yakijitokeza kushindana na hata kufikia mahali pa kutishia uhai wa chama chao, hadi baadhi ya watu kudhani kwamba ccm inameguka kama si kupasuka. Pamoja na kuwepo na makundi ya uchaguzi kila mara lakini kama nilivyotaja awali ni kwamba makundi hayo yamekuwa yakiendesha siasa za hatari lakini bila kukiumiza chama chao.
Mathalani siku za hivi karibuni tumeshuhudia makundi mbalimbali yakijipanga kwa ajili ya uraisi wa JMT mwaka 2015. Tumeshuhudia kundi la Edward Lowasa wakiwa busy kumuuza mgombea wao, na hivi karibuni tunasubiri kuona watu wakienda kula nyama choma Monduli. Kwa upande mwingine kuna kundi la Bernard Membe, na upande mwingine tena kuna kundi la Samwel Sitta. Pia kumekuwa na miunganoya makundi mbalimbali ambayo nimekuwa nikiyasikia yakitajwa yakijipanga kuhakikisha kwamba wagombea wao ndio wanaopata fursa ya kupitishwa kupeperusha bendera ya ccm come 2015.
Pamoja na kuwepo minyukano ya mara kwa mara ndani ya ccm lakini hatujawahi kushuhudia viongozi wa juu wa ccm; Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Manaibu Makatibu Wakuu na Katibu Mwenezi , mmoja wao au wawili miongoni mwao wakifanya kazi za kiofisi za chama chao kupitia vyombo vya habari.
Kwa mfano Mwigulu Nchemba ambaye vijana wengi sana wa ccm wanamuamini na kumtumainia sana kwamba ndiye anayeweza kuwanusuru na kipigo cha upinzani katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015 amekuwa akitajwa kumuunga mkono Edward Lowasa. Na kwakuwa Mwigulu anamuunga mkono Lowasa basi ni dhahiri kuwa asingependa kuona mgombea wake akiendelea kusakamwa na kuchafuliwa na wanaccm wenzake wanaopingana nae ama kushindana nae.
Katika mazingira hayo ni dhahiri kuwa Mwigulu amekuwa akiwasiliana na bosi wake-Katibu mkuu Kinana katika kuwashauri au kutafuta maelezo au ufafanuzi wa mambo mbalimbali yanayokikumba chama chao. Katika kuwasiliana huko ni wazi kuwa amekuwa akiwasiliana kwa ukaribu zaidi na katibu mkuu wake Kinana na akimsaidia kwa ukaribu katika kutekeleza majukumu yake kwakuwa yeye (Mwigulu) ndiye msaidizi wa karibu zaidi kwa Kinana. Katika kuwasilaiana na Kinana bila shaka amekuwa akitumia njia mbalimbali za mawasiliano kama vile kuzungumza nae ana kwa ana, ama akizungumza nae kwa simu, ama anawasiliana nae kwa barua/barua pepe au fax na njia nyingine za mawasiliano zinazokubalika kiofisi.
Hata mara moja sijawahi kumsikia ama kumuona Mwigulu Nchemba akitoka hadharani kwenye vyombo vya habari na kuuambia umma wa watanzania aidha kupitia press release, au kupitia mitandao ya kijamii, au kupitia magazeti, au television na radaio kwamba amemuandikia rasmi katibu mkuu wake Kinana kumuomba ufafanuzi au maelekezo ya jambo Fulani linalomhusu kiongozi mmoja wa chama chao.
Pamoja na kushuhudia mashambulizi mengi dhidi ya Lowasa kutoka kwa wanaccm wenzake, tena wakati mwingine Lowasa ameshambuliwa hadharani na viongozi wakubwa wa ccm lakini sijawahi kumuona Mwigulu akitoka kwenye vyombo vya habari na kututangazia kwamba amemuandikia barua Katibu mkuu wake Kinana atoe taarifa ya kukanusha mashambulizi yaliyofanywa dhidi ya Lowasa ama akiri kwamba kiongozi huyo (aliyemshambulia Lowasa) ametoa matamshi hayo kwa niaba ya chama hivyo wanachama wa ccm na wananchi kwa ujumla watambue kuwa huo ndio msimamo wa ccm juu ya kada wake Lowasa.
Nionachoamini ni kwamba Mwigulu amekuwa akiwasiliana kwa karibu sana na katibu mkuu wake Kinana katika kumsaidia kutekeleza majukumu yake, ni dhahiri kuwa Mwigulu amekuwa akiitumia ofisi yake ya naibu katibu mkuu pale Lumumba na Dodoma katika kutekeleza majukumu yake ya unaibu katibu mkuu wa ccm. Ni dhahiri kuwa Mwigulu amekuwa akimuandikia barua rasmi za kiofisi kumhoji juu ya mambo Fulani yenye mwelekeo wa kukimuiza chama chao ama viongozi wao ama wanachama wao, lakini kama nilivyogusia tangu hapo awali sijawahi kumuona akivujisha barua zake hizo katika vyombo vya habari kwa sababu iwayo yoyote ile.
Kutokana na mazingira hayo na kutambua kwamba Mwigulu amekwisha kuchagua upande anaouunga mkono (Lowasa), lakini pia naye amekuwa akitajwa kwamba anafikiria kujitosa katika kinyanganyiro cha uraisi (huenda ni alternative choice incase bid ya Lowasa imekwama), bila shaka amekuwa akipambana ndani ya ccm kuhakikisha kuwa jina lake na la mgombea wake hayachafuliwi bila sababu za msingi.
Kwa mantiki hiyo basi nimekuwa nikitamani sana kumuona ama kumsikia ama kumsoma Mwigulu Nchemba akitoa press release, au akiandika katika mitandao ya kijamii kwamba amemuandikia rasmi barua katibu mkuu wake Kinana kutaka maelezo ama ufafanuzi wa hoja kwamba viongozi na wanachama wa ccm wanaomshambulia mgombea wake hadharani kwa kumhusisha na kashfa mbalimbali za ufisadi na zinazoonyesha dhahiri zinamchafua kiongozi huyo.
Kwakuwa Mwigulu anaungwa mkono na vijana wengi ndani ya ccm, na kwakuwa vijana wengi wa ccm wanamuunga mkono Lowasa katika mbio zake za kuwania uraisi, na kwakuwa kuna baadhi ya viongozi wa ccm tena wengine wa kitaifa wamekuwa wakiendelea kumchafua Lowasa, na kutokana na kuendelea kuongezeka kwa upinzani ndani ya ccm dhidi ya Lowasa ni dhahiri kuwa muda si mrefu tutamshuhudia Mwigulu Nchemba akitujuza ni kwa kiwango gani amepambana kuhakikisha kuwa jina la mgombea wake halichafuliwi na atatufahamisha ni barua ngapi amemuandikia Kinana akimtaka atoe tamko la kukubali ama kukanusha taarifa zote zinazoandikwa ama kuchapishwa zikimshambulia Lowasa. Ninausubiri wakati huo kwa hamu sana kwakuwa muda si mrefu tutayashuhudia maajabu hayo yakitokea.
Nawasilisha.