Freyzem
JF-Expert Member
- Jun 29, 2013
- 10,052
- 24,442
Wapo watakaosema tunamuonea wivu, n.k!
Lakini huo ndio ukweli! Mwigulu Nchemba kupewa Wizara ya Fedha kwake ni kama kumvisha mtoto wa chekechea kiatu namba 45 cha mtu mzima.
Huyu Mwigulu aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha na pengine wengine wanaweza kumtetea kwa kigezo hicho kwamba tayari ana uzoefu na hiyo wizara na zaidi ni kwamba ni msomi mwenye taaluma ya juu ya masuala ya uchumi! Lakini kiuhalisia japo ana sifa hizo lakini kwa mwenendo wake alionaylo hakupaswa kupewa hii nafasi nyeti!
Hakuna cha maana sana atakachofanya kwenye hii wizara, zaidi anaweza kuwa miongoni mwa mawaziri wabovu zaidi katika hiyo wizara.
Alipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani yapo mambo ya hovyo sana alikuwa akiyayafanya hali iliyopelekea akatumbuliwa akiwa njiani na kunyang'anywa hata gari bila kutarajia.
Hali iliyopelekea kuanza kumlamba viatu mwendazake na kupewa Wizara ya Katiba na Sheria lakini nayo wizara hii ilimshinda ni vile tu haiangaliwi sana.
Sasa amepewa wizara nyeti ya fedha, kwa anayoyafanya hata huko bungeni yanaakisi kabisa ubovu wake katika kuiongoza.
Kinachotakiwa ni hatua za haraka zifanyike na ninaamini Mama yetu macho yake yanaona vyema kama alivyosema, pengine hakushauriwa vyema hivyo naamini tayari mezani mwake wapo washauri mahiri ambao tayari wamekwishaona na wamekwisha mshauri vyema la kufanya.
Hivyo naamini mapema tu matokeo yataonekana.
Lakini huo ndio ukweli! Mwigulu Nchemba kupewa Wizara ya Fedha kwake ni kama kumvisha mtoto wa chekechea kiatu namba 45 cha mtu mzima.
Huyu Mwigulu aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha na pengine wengine wanaweza kumtetea kwa kigezo hicho kwamba tayari ana uzoefu na hiyo wizara na zaidi ni kwamba ni msomi mwenye taaluma ya juu ya masuala ya uchumi! Lakini kiuhalisia japo ana sifa hizo lakini kwa mwenendo wake alionaylo hakupaswa kupewa hii nafasi nyeti!
Hakuna cha maana sana atakachofanya kwenye hii wizara, zaidi anaweza kuwa miongoni mwa mawaziri wabovu zaidi katika hiyo wizara.
Alipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani yapo mambo ya hovyo sana alikuwa akiyayafanya hali iliyopelekea akatumbuliwa akiwa njiani na kunyang'anywa hata gari bila kutarajia.
Hali iliyopelekea kuanza kumlamba viatu mwendazake na kupewa Wizara ya Katiba na Sheria lakini nayo wizara hii ilimshinda ni vile tu haiangaliwi sana.
Sasa amepewa wizara nyeti ya fedha, kwa anayoyafanya hata huko bungeni yanaakisi kabisa ubovu wake katika kuiongoza.
Kinachotakiwa ni hatua za haraka zifanyike na ninaamini Mama yetu macho yake yanaona vyema kama alivyosema, pengine hakushauriwa vyema hivyo naamini tayari mezani mwake wapo washauri mahiri ambao tayari wamekwishaona na wamekwisha mshauri vyema la kufanya.
Hivyo naamini mapema tu matokeo yataonekana.