Mwigulu na TRC, kuhusu mkandarasi CCECC, tuzungumze kizalendo kidogo!

Apr 24, 2011
29
542
Mwigulu, katika hotuba ya Bajeti kuu ya serikali, ukurasa wa 44, ulisema serikali imeanza mchakato wa kutafuta mkandarasi wa kujenga kipande cha SGR (Tabora-Kigoma) 514km kwa US$2.1 bilioni (Sh4.89 trillioni). Tulifahamu uliwapa kandarasi CCECC.

20/12/2022 serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa SGR Tabora-Kigoma kilometa 506km. $2.7bn (Sh6.34 trilioni) na ujenzi huu unatarajiwa kuchukua miezi 48. Kwa kusaini kipande hiki, Serikali itakuwa imewekeza $10.04bn (Sh23.3 trilioni) kwa awamu ya Dar-Mwanza na Tabora-Kigoma.

Hapa ipo tofauti. Hotuba yako ya bajeti ulisema ni 514km, lakini Shirika la Reli Tanzania (TRC) wamesaini mkataba wa kujenga 506km. Kuna pungufu ya 8km. Ulisema ujenzi utagharimu Sh4.89 trilioni lakini mkataba umesainiwa Sh6.34 trilioni. Ongezeko la Sh1.45 trilioni. Maelezo?

Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa amesema Mikataba haitakuwa na mabadiliko ya bei, ikijumuisha vitu vya ujenzi, hivyo ongezeko la $1.304bn (30.3%, kwa maana ya thamani ya fedha) HALIPO. Ongezeko la Sh1.45 trilioni kwenye bajeti kuu ya serikali na mkataba imetoka wapi?

Katika mfumo wa TANePS (Tanzanian National e-Procurement System), Mkandarasi CCECC alipewa zabuni ya ujenzi wa SGR Tabora-Kigoma kwa Sh6.69 trilioni. Tofauti ya bajeti ya Mwigulu na TANePS ni Sh1.85 trilioni. Tofauti ya bajeti ya Mwigulu na mkataba uliosainiwa ni Sh1.45 trilioni. Lipo TATIZO.

Mwigulu Nchemba wakati akisoma bajeti kuu ya serikali 2022/2023 alisema “serikali imeanza mchakato” wakati ukweli ni kwamba Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation alikuwa tayari amepewa zabuni tangu 04.04.2022 kwa utaratibu wa ‘single source’.

Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation (CCECC) alipewa hii zabuni kwa utaratibu wa bila ushindani (single source) ambayo ilidumu TANePS kwa dakika 30, yenye BID ID 421346 ambayo ipo secured. Opening na Closing date yake ni 10:00 hadi 10:30, 04/04/2022

Title;PA/154/HQ/2021-22/W/02LOT1
Status; (Evaluation)
Closing Date; 4/4/2022 10:00
Opening Date; 4/4/2022 10:30
Envelope; Single
Suplier Name; CCECC,
BID ID; 421346
Financial Value; 6,698,935,255,040
BID security provided; TRUE
BID security Value; 103932450000
FDR; 0.00

Hii ndiyo zabuni ambayo mkandarasi (CCECC) alishinda kama ilivyoonekana katika mfumo wa TANePS. Mwigulu, hotuba ya Bajeti kuu ya serikali ilisema ni $2.1 bilioni (Sh4.90 trillioni) kwa 516km. Mkataba wa ujenzi uliosainiwa kati ya TRC na CCECC ni $2.7bn (Sh6.34 trilioni) kwa 506km.

Bunge limeshindwa kuhoji tofauti hizo mbili. Tuseme bunge halina watu wenye akili timamu. Baraza la mawaziri lilijadili na kuridhia? Hata Ikulu imekubali kumchukua Rais Samia Suluhu Hassan na kumruhusu kuketi mbele ya TRC na CCECC kushuhudia utiaji saini huo ambao una mazonge.

Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation (CCECC) aliyepewa zabuni hiyo bila kushindana (single source) ana zaidi ya 38% ya kiasi ambacho Mwigulu (waziri wa fedha) amekitaja katika hotuba yake ya bajeti. Gharama za ujenzi ni US$4.8M (Sh11.19bn) kwa kila 1km.

Hii tofauti ambayo ni ziada ya Sh1.45 trilioni, ni mara 30 ya pesa waliotumia USA kushambulia miji ya Homs na Damascus nchini Syria 14.4.2018. USA walitumia Nyambizi inayotumia umeme wa nyuklia, ndege ya kijeshi B-1 bomber na meli vita bajeti ikiwa US$26M (Sh60.7 bilioni)

Sh1.45 trilioni ni karibu nusu ya utajiri wa Bilionea Mohammed Dewji. Ni zaidi ya fedha zilizotumika kwenye uwekezaji wa kiwanda cha saruji cha Dangote (Sh1.3 trilion). Ni robo ya Utajiri wa Rais wa zamani wa USA, Bilionea Donald Trump (Sh6.99 trilioni). Kimsingi ni fedha nyingi.

Ikiwa noti moja ya elfu 10 ina uzito wa gram 1. Sh1.4 trilioni (noti za 10,000 zikiwa milioni 140) zina uzito wa gram milioni 140 (140,000,000gm) au kilogram 140,000 sawa na uzito wa tani 140. Reli ya SGR inayojengwa inaweza kuhimili mzigo wa uzito wa Tani 35. Hii NI KUFURU.

Yaani hiyo ziada (Sh1.45 trilioni) ambayo haieleweki katika hiyo biashara ya TRC na CCECC ni zaidi ya bajeti za wizara tatu katika mwaka wa fedha 2022/2023. Ni zaidi ya fedha zote ambazo zilipigwa katika ufisadi wa ESCROW (Sh306 bilioni) na EPA (Sh133 bilioni) kwa pamoja.

Pia hata ukijumlisha ufisadi wa MEREMETA (Sh205.9 bilioni), RADA (Sh73 bilioni), KAGODA (Sh40 bilioni), MABILIONI YA JK (Sh50 bilioni) bado haufiki hiyo tofauti ya kiasi cha ziada (Sh1.45 trilioni). Bunge lenye utimamu lingeomba ‘review’ ya ‘procurement and tendering’.

Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation alipewa ujenzi wa lot Na. 5, Isaka–Mwanza (249km). Miezi 16 alijenga 4.4% pekee na HAKUNA hata kipande kimoja cha reli aliweka katika miezi 17. Mwigulu akaenda bungeni kusema haukuwepo ufadhili wa kifedha. Ni MZAHA.

RICHMOND; kampuni ilipewa zabuni ya kuzalisha umeme ikiwa haina fedha, wataalam wala ofisi. Ndiyo iliondoka na Edward Lowassa. Sasa China Civil Engineering construction corporation (CCECC) nao wamepewa zabuni katika mazingira kama hayo. Mwigulu anakiri kweli hawakuwa na fedha

Utaratibu wa zabuni za ‘single source’ ni LAZIMA mkandarasi akidhi vigezo na uwezo. Huyu mkandarasi wa Mwigulu hana sifa hizo. Miezi 17 alishindwa kupeleka hata ambulance, hakuna usalama kwa wafanyakazi, amefanya kazi kwa 4.4%. Mkandarasi huyu hajakidhi vigezo vya single source.

China Civil Engineering construction corporation (CCECC) kapewa ujenzi wa lot Na.6 kutoka Tabora-Kigoma (506km). Hivyo kwa 506km mkandarasi atatumia $2.7 bilioni (Sh6.34 trillioni). Kapewa zabuni bila ushindani. Zingatia; TANePS inaonyesha ni Sh6.69 trilioni

Phase 1 Dar es Salaam – Morogoro (300km) kandarasi ni Yapi Merkezi na Mota Engil Africa. Phase 2 Morogoro - Makutupora (422km) kandarasi ni Yapi Merkezi. Phase 3 Makutupora–Tabora (294km) kandarasi ni Yapi Merkezi. Kumbuka, phase 3 imegharimu US$1.9 billion (Sh4.43 trillioni)

Mwigulu na TRC, Mkandarasi wenu, China Civil Engineering construction corporation (CCECC), amekidhi wapi vigezo vya kupewa kandarasi yenye thamani ya $2.7 bilioni (Sh6.34 trillioni) wakati kwa miezi 17 alifanikiwa kujenga lot Na.5 kwa 4.4% pekee?

Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation (CCECC) kipande cha Tabora-Kigoma (514km) anachukua Sh6.34 trilioni. Nusu ya fedha zote ambazo zimetengwa kwa ujenzi wa DSM-Mwanza ambao ujenzi wake jumla ni Sh14.9 trillion (US$6.4 billion). Hapa kuna mashaka makubwa.

Utaratibu wa ununuzi katika kazi za ujenzi, ununuzi wa huduma na bidhaa kwa njia ya zabuni zisizoshindanishwa (single source) unasimamiwa na Kanuni ya 159, 160 na 161 ya Kanuni za Ununuzi wa Umma, 2013 kama zilivyofanyiwa marekebisho na Tangazo la Serikali Na. 333. la 2016.

Kwa utaratibu wa ununuzi wa zabuni za (single source), PPRA inatakiwa kuhakikisha wanapata wazabuni wenye sifa, uzoefu na uwezo wa kutekeleza mikataba hiyo kwa haraka na ndani ya muda wa mkataba na kuhakikisha Serikali inapata thamani ya fedha kwa manunuzi yote yatakayofanyika.

Athari za kutumia mzabuni mmoja kwa utaratibu wa manunuzi wa zabuni zisizoshindanishwa (single source) ni kiini cha rushwa, uzembe, upendeleo, pamoja na uwezo mdogo wa mzabuni. Tunaona yanayotokea kati ya Mwigulu, TRC na China Civil Engineering construction corporation (CCECC).

Mfumo wa ushindani wa wazabuni wengi, ambayo kwa mujibu wa sheria za nchi, huchukua takriban miezi mitatu au zaidi hadi kutangazwa mshindi. kutoa zabuni bila ushindani kunaleta upendeleo kwa baadhi ya wazabuni kwa gharama za watu wengine. Rushwa inaweza kutamalaki.

Kuna uwezekano mkubwa wa kutekeleza miradi chini ya kiwango. Gharama za mradi zinaweza zisiwe halisi. Kwamba zinaweza kuwa gharama kubwa zaidi, maana makubaliano ndio yanasimamia gharama za mradi. Tuwaonee huruma watu wetu. UMASKINI ni mkubwa.

MMM, Martin Maranja Masese
Mtikila!
 
Mwigulu, katika hotuba ya Bajeti kuu ya serikali, ukurasa wa 44, ulisema serikali imeanza mchakato wa kutafuta mkandarasi wa kujenga kipande cha SGR (Tabora-Kigoma) 514km kwa US$2.1 bilioni (Sh4.89 trillioni). Tulifahamu uliwapa kandarasi CCECC.

20/12/2022 serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa SGR Tabora-Kigoma kilometa 506km. $2.7bn (Sh6.34 trilioni) na ujenzi huu unatarajiwa kuchukua miezi 48. Kwa kusaini kipande hiki, Serikali itakuwa imewekeza $10.04bn (Sh23.3 trilioni) kwa awamu ya Dar-Mwanza na Tabora-Kigoma.
Aisee ndimi mbili hizi Mwigulu mmoja.
 
Kuna mambo mengi ya kiufundi umepotosha, mf. Mpango WA bajeti ni mwaka mmoja wakati kipande cha reli itajengwa kwa miaka minne Ina maana budget itatengwa miaka hiyo minne ili kumlipa mkandarasi.
Hotuba inaongelea matarajio na planning. Huwezi kusema una plani ya miaka 6 then ufanye bajeti ya miezi mitatu. Lazima uwe na estimated costs
 
[mention]Martin Maranja Masese [/mention] umesema madini sana ndio maana nasema hii nchi,kijana mmoja wa BAVICHA ni sawa na Vijana 5000 wa UVCCM…..imagine watu kama hawa Twaha mwaipaya,John Pambalu,GJ Malissa pamoja na bwana Martin uwape ukuu wa mikoa na wilaya?? Hii nchi ingepiga hatua sana
 
Mwigulu na TRC, Mkandarasi wenu, China Civil Engineering construction corporation (CCECC), amekidhi wapi kupewa kandarasi yenye thamani ya $2.1 bilioni (Sh4.89 trillioni) wakati kwa miezi 17 alifanikiwa kujenga lot Na.5 kwa 4.4% pekee?
Duuh kazi ipo. Hii SGR inaweza isiishe for 20yrs.🤣🤣
 
Kadiri unavyozidi kujua vitu vingi in details kuhusu bongo yetu ndivyo kichwa kinavyozidi kuuma, wale wasiojua kabisa hawana habari wala hawajali kwa hiyo hawana stress..
Na ndio wenye maisha magumu hatari ila hawana habari na yanayoendelea.
Mtz anayefatilia mambo ya Nchi unakuta nimtu anayeweza kujikwamua na kutokana na changamoto anazokutana nazo anaamua kufatilia kwa ukaribu. Wenzangu na mimi holaaaa
 
Mwigulu, katika hotuba ya Bajeti kuu ya serikali, ukurasa wa 44, ulisema serikali imeanza mchakato wa kutafuta mkandarasi wa kujenga kipande cha SGR (Tabora-Kigoma) 514km kwa US$2.1 bilioni (Sh4.89 trillioni). Tulifahamu uliwapa kandarasi CCECC.

20/12/2022 serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa SGR Tabora-Kigoma kilometa 506km. $2.7bn (Sh6.34 trilioni) na ujenzi huu unatarajiwa kuchukua miezi 48. Kwa kusaini kipande hiki, Serikali itakuwa imewekeza $10.04bn (Sh23.3 trilioni) kwa awamu ya Dar-Mwanza na Tabora-Kigoma.

Hapa ipo tofauti. Hotuba yako ya bajeti ulisema ni 514km, lakini Shirika la Reli Tanzania (TRC) wamesaini mkataba wa kujenga 506km. Kuna pungufu ya 8km. Ulisema ujenzi utagharimu Sh4.89 trilioni lakini mkataba umesainiwa Sh6.34 trilioni. Ongezeko la Sh1.45 trilioni. Maelezo?

Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa amesema Mikataba haitakuwa na mabadiliko ya bei, ikijumuisha vitu vya ujenzi, hivyo ongezeko la $1.304bn (30.3%, kwa maana ya thamani ya fedha) HALIPO. Ongezeko la Sh1.45 trilioni kwenye bajeti kuu ya serikali na mkataba imetoka wapi?

Katika mfumo wa TANePS (Tanzanian National e-Procurement System), Mkandarasi CCECC alipewa zabuni ya ujenzi wa SGR Tabora-Kigoma kwa Sh6.69 trilioni. Tofauti ya bajeti ya Mwigulu na TANePS ni Sh1.85 trilioni. Tofauti ya bajeti ya Mwigulu na TANePS ni Sh1.45 trilioni. Lipo TATIZO.

Mwigulu Nchemba wakati akisoma bajeti kuu ya serikali 2022/2023 alisema “serikali imeanza mchakato” wakati ukweli ni kwamba Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation alikuwa tayari amepewa zabuni tangu 04.04.2022 kwa utaratibu wa ‘single source’.

Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation (CCECC) alipewa hii zabuni kwa utaratibu wa bila ushindani (single source) ambayo ilidumu TANePS kwa dakika 30, yenye BID ID 421346 ambayo ipo secured. Opening na Closing date yake ni 10:00 hadi 10:30, 04/04/2022

Title;PA/154/HQ/2021-22/W/02LOT1
Status; (Evaluation)
Closing Date; 4/4/2022 10:00
Opening Date; 4/4/2022 10:30
Envelope; Single
Suplier Name; CCECC,
BID ID; 421346
Financial Value; 6,698,935,255,040
BID security provided; TRUE
BID security Value; 103932450000
FDR; 0.00

Hii ndiyo zabuni ambayo mkandarasi (CCECC) alishinda kama ilivyoonekana katika mfumo wa TANePS. Mwigulu, hotuba ya Bajeti kuu ya serikali ilisema ni $2.1 bilioni (Sh4.90 trillioni) kwa 516km. Mkataba wa ujenzi uliosainiwa kati ya TRC na CCECC ni $2.7bn (Sh6.34 trilioni) kwa 506km.

Bunge limeshindwa kuhoji tofauti hizo mbili. Tuseme bunge halina watu wenye akili timamu. Baraza la mawaziri lilijadili na kuridhia? Hata Ikulu imekubali kumchukua Rais Samia Suluhu Hassan na kumruhusu kuketi mbele ya TRC na CCECC kushuhudia utiaji saini huo ambao una mazonge.

Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation (CCECC) aliyepewa zabuni hiyo bila kushindana (single source) ana zaidi ya 38% ya kiasi ambacho Mwigulu (waziri wa fedha) amekitaja katika hotuba yake ya bajeti. Gharama za ujenzi ni US$4.8M (Sh11.19bn) kwa kila 1km.

Hii tofauti ambayo ni ziada ya Sh1.45 trilioni, ni mara 30 ya pesa waliotumia USA kushambulia miji ya Homs na Damascus nchini Syria 14.4.2018. USA walitumia Nyambizi inayotumia umeme wa nyuklia, ndege ya kijeshi B-1 bomber na meli vita bajeti ikiwa US$26M (Sh60.7 bilioni)

Sh1.45 trilioni ni karibu nusu ya utajiri wa Bilionea Mohammed Dewji. Ni zaidi ya fedha zilizotumika kwenye uwekezaji wa kiwanda cha saruji cha Dangote (Sh1.3 trilion). Ni robo ya Utajiri wa Rais wa zamani wa USA, Bilionea Donald Trump (Sh6.99 trilioni). Kimsingi ni fedha nyingi.

Ikiwa noti moja ya elfu 10 ina uzito wa gram 1, maana yake kwenye Sh1.4 trilioni (noti milioni 140) zina uzito wa gram milioni 140 (140,000,000gm) au kilogram 140,000 sawa na uzito wa tani 140. Reli ya SGR inayojengwa inaweza kuhimili mzigo wa uzito wa Tani 35. Hii NI KUFURU.

Yaani hiyo ziada (Sh1.45 trilioni) ambayo haieleweki katika hiyo biashara ya TRC na CCECC ni zaidi ya bajeti za wizara tatu katika mwaka wa fedha 2022/2023. Ni zaidi ya fedha zote ambazo zilipigwa katika ufisadi wa ESCROW (Sh306 bilioni) na EPA (Sh133 bilioni) kwa pamoja.

Pia hata ukijumlisha ufisadi wa MEREMETA (Sh205.9 bilioni), RADA (Sh73 bilioni), KAGODA (Sh40 bilioni), MABILIONI YA JK (Sh50 bilioni) bado haufiki hiyo tofauti ya kiasi cha ziada (Sh1.45 trilioni). Bunge lenye utimamu lingeomba ‘review’ ya ‘procurement and tendering’.

Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation alipewa ujenzi wa lot Na. 5, Isaka–Mwanza (249km). Miezi 16 alijenga 4.4% pekee na HAKUNA hata kipande kimoja cha reli aliweka katika miezi 17. Mwigulu akaenda bungeni kusema haukuwepo ufadhili wa kifedha. Ni MZAHA.

RICHMOND; kampuni ilipewa zabuni ya kuzalisha umeme ikiwa haina fedha, wataalam wala ofisi. Ndiyo iliondoka na Edward Lowassa. Sasa China Civil Engineering construction corporation (CCECC) nao wamepewa zabuni katika mazingira kama hayo. Mwigulu anakiri kweli hawakuwa na fedha

Utaratibu wa zabuni za ‘single source’ ni LAZIMA mkandarasi akidhi vigezo na uwezo. Huyu mkandarasi wa Mwigulu hana sifa hizo. Miezi 17 alishindwa kupeleka hata ambulance, hakuna usalama kwa wafanyakazi, amefanya kazi kwa 4.4%. Mkandarasi huyu hajakidhi vigezo vya single source.

China Civil Engineering construction corporation (CCECC) kapewa ujenzi wa lot Na.6 kutoka Tabora-Kigoma (506km). Hivyo kwa 506km mkandarasi atatumia $2.7 bilioni (Sh6.34 trillioni). Kapewa zabuni bila ushindani. Zingatia; TANePS inaonyesha ni Sh6.69 trilioni

Phase 1 Dar es Salaam – Morogoro (300km) kandarasi ni Yapi Merkezi na Mota Engil Africa. Phase 2 Morogoro - Makutupora (422km) kandarasi ni Yapi Merkezi. Phase 3 Makutupora–Tabora (294km) kandarasi ni Yapi Merkezi. Kumbuka, phase 3 imegharimu US$1.9 billion (Sh4.43 trillioni)

Mwigulu na TRC, Mkandarasi wenu, China Civil Engineering construction corporation (CCECC), amekidhi wapi vigezo vya kupewa kandarasi yenye thamani ya $2.7 bilioni (Sh6.34 trillioni) wakati kwa miezi 17 alifanikiwa kujenga lot Na.5 kwa 4.4% pekee?

Mkandarasi China Civil Engineering construction corporation (CCECC) kipande cha Tabora-Kigoma (514km) anachukua Sh6.34 trilioni. Nusu ya fedha zote ambazo zimetengwa kwa ujenzi wa DSM-Mwanza ambao ujenzi wake jumla ni Sh14.9 trillion (US$6.4 billion). Hapa kuna mashaka makubwa.

Utaratibu wa ununuzi katika kazi za ujenzi, ununuzi wa huduma na bidhaa kwa njia ya zabuni zisizoshindanishwa (single source) unasimamiwa na Kanuni ya 159, 160 na 161 ya Kanuni za Ununuzi wa Umma, 2013 kama zilivyofanyiwa marekebisho na Tangazo la Serikali Na. 333. la 2016.

Kwa utaratibu wa ununuzi wa zabuni za (single source), PPRA inatakiwa kuhakikisha wanapata wazabuni wenye sifa, uzoefu na uwezo wa kutekeleza mikataba hiyo kwa haraka na ndani ya muda wa mkataba na kuhakikisha Serikali inapata thamani ya fedha kwa manunuzi yote yatakayofanyika.

Athari za kutumia mzabuni mmoja kwa utaratibu wa manunuzi wa zabuni zisizoshindanishwa (single source) ni kiini cha rushwa, uzembe, upendeleo, pamoja na uwezo mdogo wa mzabuni. Tunaona yanayotokea kati ya Mwigulu, TRC na China Civil Engineering construction corporation (CCECC).

Mfumo wa ushindani wa wazabuni wengi, ambayo kwa mujibu wa sheria za nchi, huchukua takriban miezi mitatu au zaidi hadi kutangazwa mshindi. kutoa zabuni bila ushindani kunaleta upendeleo kwa baadhi ya wazabuni kwa gharama za watu wengine. Rushwa inaweza kutamalaki.

Kuna uwezekano mkubwa wa kutekeleza miradi chini ya kiwango. Gharama za mradi zinaweza zisiwe halisi. Kwamba zinaweza kuwa gharama kubwa zaidi, maana makubaliano ndio yanasimamia gharama za mradi. Tuwaonee huruma watu wetu. UMASKINI ni mkubwa.

MMM, Martin Maranja Masese
Mtikila!
Uko vizuri sana Mwamba bonge la mzalendo kudos Mura!!
 
Back
Top Bottom