Kazi yetu ni kusema kama tulivyosema kabla ya uchaguzi mkatubeza, yakiharibika mtatafuta watu au makampuni ya kufanya Damage Control.
Baada ya tukio kubwa la 29/10, ambalo halijawahi kutokea nchini, kipindi hiki kilitakiwa kuwa kipindi cha kuliponya taifa, a healing period, kipindi cha kutibu majeraha, ilitakiwa siasa ziwekwe kando kwa muda.
Sio kipindi cha kutambiana kuwa tumeshinda kwa kishindo, wanatakiwa viongozi wenye busara watakao liunganisha taifa sio wanaochonganisha wananchi, viongozi watulivu, waungwana, wasio na ujivuni mfano wa mzee Pinda.
Kosa alilofanya Samia katika kipindi hiki ni kumteua Mwigulu kuwa PM, Kihongosi kuwa msemaji wa chama na kuendelea kumwamini Msigwa kuwa msemaji wa serikali.
Kuwatanguliza watu kama Mwigulu, Kihongosi, Makonda watu wenye makandokando wenye viburi wenye visasi ni kutia chumvi kwenye kidonda kibichi.
Hawa ni vijana bado wanaongozwa na mihemko zaidi kuliko busara, midomo yao itakuja kumponza Mkiti wao na kuliponza taifa zima, wanapotoa matamshi huwa hawaangalii consequences zake, mf. unaposema 'Mataifa ya nje yanahonga watu kutuchafua', bila kuwa na ushahidi wowote unategemea kupata response gani kutoka kwa mataifa unayoyatuhumu.
Baada ya tukio kubwa la 29/10, ambalo halijawahi kutokea nchini, kipindi hiki kilitakiwa kuwa kipindi cha kuliponya taifa, a healing period, kipindi cha kutibu majeraha, ilitakiwa siasa ziwekwe kando kwa muda.
Sio kipindi cha kutambiana kuwa tumeshinda kwa kishindo, wanatakiwa viongozi wenye busara watakao liunganisha taifa sio wanaochonganisha wananchi, viongozi watulivu, waungwana, wasio na ujivuni mfano wa mzee Pinda.
Kosa alilofanya Samia katika kipindi hiki ni kumteua Mwigulu kuwa PM, Kihongosi kuwa msemaji wa chama na kuendelea kumwamini Msigwa kuwa msemaji wa serikali.
Kuwatanguliza watu kama Mwigulu, Kihongosi, Makonda watu wenye makandokando wenye viburi wenye visasi ni kutia chumvi kwenye kidonda kibichi.
Hawa ni vijana bado wanaongozwa na mihemko zaidi kuliko busara, midomo yao itakuja kumponza Mkiti wao na kuliponza taifa zima, wanapotoa matamshi huwa hawaangalii consequences zake, mf. unaposema 'Mataifa ya nje yanahonga watu kutuchafua', bila kuwa na ushahidi wowote unategemea kupata response gani kutoka kwa mataifa unayoyatuhumu.