Mwigulu Chemba soma hapa baba!

Mwigulu Chemba soma hapa baba!

Kwa imani ya dini yangu kipimo ambacho mtu hutumia kuwapimia watu duniani naye atapimiwa kwa kipimo hichohicho kwa mungu hivyo nipamoja nawe kakika maombi ya kitaifa ya siku 7
 
Kwa imani ya dini yangu, nimefundishwa kwamba sitakiwi kulipa kisasi! Si vizuri kufunga ili umuombe Mungu amwadhibu binadamu mwingine. Hakuna mkamilifu chini ya jua, hivyo ni vizuri tukaombeana mema.

Tunatakiwa kufunga na kusali Mungu awape huruma wale walio kwenye mateso! Awape ujasiri na uwezo wa kupambana na magumu yanayowasibu.
Pia, tumuombe Mungu abadili moyo wa Bwana Mkubwa uliyemtaja kuhusika na mateso ya hao vijana. Awe na moyo wa ubinadamu na huruma. Chuki, kisasi na tamaa ya madaraka viondoke katika moyo wake.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums


Wewe,

Pharao alikuw na roho ngumu ya kutokuamini na kumtii Mungu, aliendelea kuwafuatilia Israel hadi alipopoteza jeshi lake lote. Waliangamia kwa ajli ya utii wako kwa farao aliyekuwa akinyanyasa Israel. Farao asiyemjua Yusuph, ccm isiyokuwa na uchungu wa taifa la Tanzania.

Nabii Elijah alipokuwa kwenye kilima, mfalme Ahabu alituma majeshi ili wamkamate, Elia aliagiza moto ukashuka na kuwateketeza wale majeshi ya Ahabu. Ahabu alitumikia miungu ya Baali.

Nabii Elisha alipokuwa amebaki baada ya kupaa kwa Elijah, wale wana wa manabii walimdhihaki wakisema "paa wewe mwenye upaa", Elisha aliagiza dubu wakawamaliza.

Yesu na yule mwenye pepo ziitwazo :legion" sijui kama nimeandika sahihi ama "jeshi" aliruhusu zile pepo ziingie kwa nguruwe na wale nguruwe na pepoe zao wakaishia majini.

MUNGU HANA KANUNI MOJA YA KUTETEA WATU WANAOTESWA. Kama mtu anaendelea kufuga roho chafu katika moyo wake, na anaendelea kumtumikia shetani huku akinyanyasa watu wa Mungu, Mungu halazimishwi kumtenganisha na hiyo roho. Wala hana kanuni moja.

IMANI YETU IMEJENGWA JUU YA MITUME NA MANABII. TUTAMWOMBA MUNGU NA NAMNA ATAKAVYOSHUGHULIKA NA AKINA NCHEMBA NA SYNDICATE YAKE YOTE, ANAJUA YEYE. SISI HATUWEZI KUMCHAGULIA. TUNACHOTAKA UDHALIMU HUU UKOME MARA MOJA NA MILELE.

SASA NI MUDA WA WACHAWI WOTE, WASHIRIKINA, WENYE VIBURI, FITINA, UWONGO NA HILA ZA KILA NAMNA, KUMTAMBUA NA KUKIRI KWAMBA, KWELI YUKO MUNGU ANAYEISHI NAYE NI MUNGU WAA MILELE WALA HAKUNA MWINGINE.

SAWA NA PHARAOH ALIVYO KIRI KWAMBA "GOD OF MOSES IS GOD"


THIS IS REAL, LET THE CHURCH SAY "ENOUGH IS ENOUGH, WE ARE NOW TAKING OUR POSITIONS IN THE SPIRITUAL REALM".

GOD BLESS TANZANIA.
 
Hivi ndugu yangu, umelogwa na CHADEMA? au ndio ulevi wa kupenda kitu. Yaani huwa mkikaa huwa hamna shughuli za kufanya mnawaza siasa tuuu na uzushi. na kama wewe ni kijana unapoteza muda mwingi sana wa faida ya uzee wako. Siwapendi sana watu wanaopenda kujiridhisha na hisia zao hata kama za uongo na kujitahidi kuwashawishi wengine waamini kuwa za kweli. Poleni vijana wenzangu wa Tanzania mnaofikiri kuwa kuna chama kitakachowakomboa mkaridhika. Nionavyo mimi, watu wengi hasa vijana wanamatumaini ya mkate tu wakifikiri ndio hitaji la maisha lakini kumbe maisha ni zaidi ya mkate. Nawaomba vijana wenzangu kama maisha yako unategemea siasa ikutoe kazania siasa lakini kama unategemea kazi ya mikono yako tufanye kazi tuache siasa na uzushi usiokuwa na manufaa kwetu.

Sidhani kuwa kuna mtu (awe ni kijana au vinginevyo) anaetegemea serikali impe kila kitu. Kinachotakiwa ni kuwepo mazingira bora (equal and fair playground if you like) ili kila mtu afanikiwe kulingana na juhudi zake. Utafanyaje kazi kama polisi wanaruhusiwa kukukamata na kukubambia kesi? Utafanyaje kazi kama unazuiwa kufanya kazi unayoiweza, kwa mfano kunyang'anywa ardhi na kupewa "wawekezaji"?

Are you that naive to see that this government hinders the prosperity of majority of people in this land for the benefit of kikwete and his gang of thieves?????
 
Kwa imani ya dini yangu kipimo ambacho mtu hutumia kuwapimia watu duniani naye atapimiwa kwa kipimo hichohicho kwa mungu hivyo nipamoja nawe kakika maombi ya kitaifa ya siku 7

Kwenye maombi hakuna mtu anaempangia Mungu kipimo kiwe cha kisasi au heri!
 
Zaburi 109 ni hatari jamani mtakimaliza kizazi chake kabisa wakati yeye binafsi ndio mwenye matatizo.
Mimi nafikiri anatakiwa aache kuvuta bangi kwanza na amrudie Mungu wake, vinginevyo atakwisha.

Huwezi kuamini asila nilizonazo dhidi ya Mwigulu!! Mungu aepushie mbali nisikutane naye eneo la kificho
 
Hivi ndugu yangu, umelogwa na CHADEMA? au ndio ulevi wa kupenda kitu. Yaani huwa mkikaa huwa hamna shughuli za kufanya mnawaza siasa tuuu na uzushi. na kama wewe ni kijana unapoteza muda mwingi sana wa faida ya uzee wako. Siwapendi sana watu wanaopenda kujiridhisha na hisia zao hata kama za uongo na kujitahidi kuwashawishi wengine waamini kuwa za kweli. Poleni vijana wenzangu wa Tanzania mnaofikiri kuwa kuna chama kitakachowakomboa mkaridhika. Nionavyo mimi, watu wengi hasa vijana wanamatumaini ya mkate tu wakifikiri ndio hitaji la maisha lakini kumbe maisha ni zaidi ya mkate. Nawaomba vijana wenzangu kama maisha yako unategemea siasa ikutoe kazania siasa lakini kama unategemea kazi ya mikono yako tufanye kazi tuache siasa na uzushi usiokuwa na manufaa kwetu.

Pole sana mheshimiwa! Umeongea point ila haijafika kwenye point of view!
Hata kama unaichukia siasa hujui kuwa unaishi kwenye siasa?

Kama wewe unajituma katika shughuli zako na umefanikiwa na sisi tunaonyanyaswa huku siku tukianzisha vita utabaki na mafanikio yako hayo? Wewe si utakimbia sana na utaenda kupumzikia mpaka wa Mawalawi tena mikononi mwa polisi?
Labda uko nje ya nchi ila kama uko ndani ya nchi tumia fikra pana kufikiri, siasa ndiyo habari ya mjini hakuna siasa hakuna maisha! Tafuta watu wakubwa na wenye heshima zao dunia wanasiasa watakuwa wengi.

Vipi wewe mbona unakuja na kujifanya mzalendo wakati kijana anayeteswa humuonei hata huruma? Fyoka tupu!!!

 
Zaburi 109 ni hatari jamani mtakimaliza kizazi chake kabisa wakati yeye binafsi ndio mwenye matatizo.
Mimi nafikiri anatakiwa aache kuvuta bangi kwanza na amrudie Mungu wake, vinginevyo atakwisha.

Basi angalau Zaburi 108 sasa ahahahahaha
 
Biblia ni zaidi ya Zaburi 109. Soma mafungu mbalimbali au biblia nzima ndipo unaweza kutambua uhalisia wa kila jambo!

Nyuma ya zaburi 109 kuna Zaburi 108 na vitabu vingine vingi. Nafikiri ametoa kinachohusiana na hoja
 
kwa wale wanaoogopa kulipa kisasi, sio tunafanya hivyo, bali nikumwomba Mungu anyooshe mambo maana hata yeye hayamfurahishi yakipinda hovyo!
 
Biblia ni zaidi ya Zaburi 109. Soma mafungu mbalimbali au biblia nzima ndipo unaweza kutambua uhalisia wa kila jambo!

Nyuma ya zaburi 109 kuna Zaburi 108 na vitabu vingine vingi. Nafikiri ametoa kinachohusiana na hoja
 
Imeniuma sana baada ya kupata maelezo ya mateso ya kijana kutoka Bukoba, nikajiaminisha kuwa Mwigulu Nchemba niye mhusika mkuu wa hili suala pale alipotamka anayo video ya viongozi wa CHADEMA wakipanga mauaji.

Mwigulu asikudanganye mtu, usiombe upate kisasi cha Mungu kwa haya unayoyafanya itakugharimu sana, wewe pia uliumbwa kwa pumzi ile ile ambayo hao uliowasababishia kesi wanateseka mahakamani.

Imeniuma sana, nadhani wewe unafurahia haya yanayotokea ila sikudanganyi UNAYOYAPANDA UTAYAVUNA HAPAHAPA DUNIANI.

Sasa ngoja tujipange turatibu kongamano la maombi ya kufunga na kuomba kitaifa ya siku 7 ya kumuomba Mungu akatilie mbali dhuluma na mateso ya waja wake, ikiwa ni pamoja na kuwaadhibu vikali wale wawatesao wana wa Mungu! Usidhani tutatangaza kama maandamano sisi ni kimya kimya yakianza kukupata mshukuru Mungu kwa kukujibu!

Nimelia machozi yangu leo, si bure. Hata kama unahitaji madaraka si bure wache watu waishi kwa amani!


Please Vote: Kama nawewe unaungana nami kuwa mwanasiasa aliyetengeneza mkanda wa Lwakatare alaaniwe ungana nami:-
tunaanza kwa maombi ya online fungua hii link kisha upige kura yako haya ni maombi maanisha.


Tiko Pamoja katika MAOMBI MKUU. MUNGU WETU SI MWENYE KUZIBA MASIKO YAKE HATA ASISIKIE MAOMBI YETU NA KILIO CHA HAWA WANAOONEWA MAHAKAMANI KWA SABABU YA MTU MMOJA KUTAKA MADARAKA.
 
ZABURI 109 8.....
8 Siku zake na ziwe chache, Usimamizi wake na atwae mtu mwingine.
9 Wanawe na wawe yatima, Na mkewe na awe mjane.
10 Kutanga na watange wanawe na kuomba, Watafute chakula mbali na mahame yao.
11 Mdai na anase vitu vyote alivyo navyo, Wageni na wateke mapato ya kazi yake.
12 Asiwe na mtu wa kumfanyia fadhili, Wala mtu wa kuwahurumia yatima wake.
13 Wazao wake waangamizwe, Jina lao likafutwe katika kizazi cha pili.
14 Uovu wa baba zake ukumbukwe mbele za Bwana, Na dhambi ya mamaye isifutwe.
15 Ziwe mbele za Bwana daima, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
16 Kwa kuwa hakukumbuka kutenda fadhili, Bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, Hata akamfisha mtu aliyevunjika moyo,
17 Naye alipenda kulaani, nako kukampata. Hakupendezwa na kubariki, kukawa mbali naye,
 
Hii zaburi ya 109 ni kiboko, hata zab. 17:14 nayo ni ya kumsalia huyu mtu!!!!!
 
Back
Top Bottom