Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,615
MAALIM Seif Sharrif Hamad alihamia ACT-Wazalendo Machi 18, 2019. Hii ni baada ya ‘kusalimu amri’ kwenye mpambano wake na Prof. Ibrahim Lipumba kwenye CUF ya zamani. Maalim Seif aliingia kwenye mgogoro mkubwa na mwenyekiti wake Prof. Lipumba baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Maalim Seif alidai Lipumba alishajiuzulu uenyekiti wa CUF toka Agosti 2015 akipinga chama chake kumuunga mkono Edward Lowassa kama mgombea urais wa ushirikiano wa UKAWA. Maalim alidai kwamba Mkutano Mkuu wa CUF ulikutana na kukubali ombi la Lipumba la kujiuzulu.
Lakini Prof. Lipumba anadai kwamba kabla mkutano mkuu haujakutana kujadili ombi lake la kujiuzulu, alikutana na Maalim Seif wakazungumza na kuona umuhimu wa yeye kurudi kwenye uenyekiti na hivyo akaandika barua ya kufuta barua yake ya kujiuzulu. Kwa lugha nyingine Lipumba anasema kwamba wakati mkutano mkuu maalum unajadili kujiuzulu kwa Lipumba, ulikuwa unajadili barua hewa ambayo haikuwepo ilikuwa imeshafutwa!
Baada ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kukubaliana na hoja za Lipumba na kuamua kumtambua kama Mwenyekiti halali wa CUF, Maalim Seif na kundi lake waliamua kukimbilia mahakamani. Kesi iliunguruma na hatimaye mahakama nayo kwenye hukumu yake ikakubaliana na upande wa Lipumba na kumtambua kama mwenyekiti halali wa CUF. Siku hiyo hiyo Mahakama ilipotoa hukumu yake ndiyo Maalim Seif na kundi lake walihamia ACT-Wazalendo.
Miezi mitatu baadaye yaani Juni 18, 2019 niliandika makala yenye kichwa cha habari: “Zitto ajiandae kupambana na Maalim Seif, hana hadhi ya kupambana na JPM. Nitakumbusha kidogo kwa nini nilisema wawili hawa lazima watapambana mbele ya safari. Moja nilisema huyu kijana ni mnafiki, kigeugeu na asiyeaminika! Akisema hasemi ukweli, akiaminiwa haaminiki na akiweka ahadi hatekelezi!
Zitto anaweza kuongea kama mpambanaji mkubwa dhidi ya ufisadi na wizi nchini kumbe ndiye fisadi wa kutupwa! Anaweza kuongea kama mzalendo namba moja wa nchi yake, kumbe msaliti na kibaraka namba moja wa mabeberu. Zitto ukiongea naye jambo usiku saa 3, usitegemee kwamba kukicha saa 12 asubuhi bado atakuwa nawe katika kile mlichoongea. Unaweza kukuta alishakugeuka ndani ya masaa 9 tu ya usiku.
Nilisema wazi kwamba nimekaa na kufanya kazi na wanasiasa wengi tokea niingie rasmi kwenye siasa. Katika wanasiasa wote niliofanya nao kazi mpaka leo, sijawahi kuona mwanasiasa mnafiki kama Zitto Zuberi Kabwe! Katika wanasiasa waliopata kuwa marafiki zangu sana kwenye siasa za nchi hii ni Freeman Mbowe, Zitto Kabwe, Anthony Komu, Kitila Mkumbo na Peter Mwambuja! Kati yao hakuna mnafiki, kigeugeu na asiyeaminika kama Zitto!
Hakuna mwanasiasa aliyewahi kumwamini Zitto Kabwe akaaminika. Kuanzia Freeman Mbowe aliyemwingiza kwenye siasa za kitaifa mpaka Kitila Mkumbo ambaye Zitto kwa kinywa chake aliwahi kututamkia kwamba Kitila ndiye alikuwa injini yake. Kwa kifupi Zitto aliaminiwa na Freeman Mbowe, Willibrod Slaa, Marehemu Chacha Wangwe, Anthony Komu na wakurugenzi wenzake wa makao makuu ya CHADEMA, Marehemu Bob Makani, Marehemu Philemon Ndesamburo, Marehemu Amani Kabourou, hakuaminika!
Aliaminiwa na vijana wake waliokuwa tayari kumsaidia kwa lolote dhidi ya Mbowe: akina Ben Saanane, Habibu Mchange, Juliana Shonza na Mtera Mwampamba lakini hakuaminika! Maswahiba wake wa kufa na kuzikana akina Msafiri Mtemelwa na David Kafulila nao wakamwamini lakini hakuaminika!
Kitila naye alimwamini Zitto lakini aliishia kuwa mhanga wa huyu mwanasiasa mdogo lakini aliyeumiza wengi! Zitto aliyedai kwamba kumwachanisha na Kitila ni sawa na kumwondoa kwenye siasa, ndiye Zitto aliyefanya mkutano na wanaandishi wa habari na kudai chama kimebariki uteuzi wa Kitila Mkumbo kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji. Lakini nataka nikuhakikishie kwamba ni Zitto huyo huyo aliyeanzisha mchakato wa siri wa kumvua Kitila uanachama wa ACT-Wazalendo baada ya kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara kwenye serikali ya CCM.
Huyo ndiye Zitto Kabwe aliyekuwa upande wa Lipumba wakati mgogoro wa ndani ya CUF umeanza. Alimsaidia Lipumba kwa kumpa vijana wa kufanya fitna. Lakini pia alimpa Lipumba wanasheria wa kumtetea kwenye kesi aliyofunguliwa na upande wa Maalim Seif. Kabla kesi haijaisha akahamia upande wa Maalim Seif na leo Maalim Seif ni mwanachama namba moja wa ACT na Mwenyekiti Taifa wa chama hicho.
Huyu ndiye Zitto Kabwe ambaye kwenye makala ile nilisema wazi kwamba, “Nguvu anazotumia kupambana na ‘jabali’ JPM anazipoteza bure na atazijutia. Magufuli anazidi kuchanja mbuga. Treni yake ya kuelekea uchumi wa kati imeshika kasi na kama Zitto anadhani anaweza kuizuia kwa tamaa yake ya madaraka, asimame relini kujaribu kuizuia ‘treni’ hii aone itakavyompasua vipande vipande! Nguvu anazotumia kupambana na Magufuli, azitunze aje azitumie kupambana na Maalim Seif.” Samson Mwigamba, Kalamu ya Mwigamba, Juni 18, 2019.
Kama utabiri huu alidhani ni ndoto za mchana, akumbuke matukio ya hivi karibuni tu wala asiende mbali. Akumbuke alivyoumbuka siku alipojaribu kumsingizia Rais Magufuli kwamba amemfukuza kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Prof. Mohamed Janabi. Aangalie alivyokurupuka na jinsi watanzania walivyomshambulia mpaka kwa aibu akaja kukanusha habari yake yeye mwenyewe!
Kama hiyo haitoshi atazame juhudi zote alizofanya kuzuia mkopo wa Benki ya Dunia kwa Tanzania kwa ajili ya Mradi Kabambe wa Kuboresha Elimu ya Sekondari nchini. Amefanya jitihada kubwa za kuandika barua kwa kutumia nembo ya bunge, ameenda mwenyewe Marekani kuwashawishi wasitoe huo mkopo. Wakati akifanya hayo yote Rais Magufuli alikuwa hapa nchini anaendelea na shughuli zake wala hakuwahi kumtuma hata Afisaelimu wa Mkoa kwenda kuzungumza na Benki ya Dunia!
Lakini Zitto ‘ameangukia pua’ baada ya Benki ya Dunia kutangaza kwamba itatoa mkopo huo kwa serikali. Maelezo yaliyotolewa na Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Dunia, maelezo ya Mkurugenzi wa Benki hiyo hapa nchini, ‘yamemvua nguo’ Zitto akabaki uchi wa kisiasa! Kwa aibu akaandika andiko la kuipongeza benki hiyo na wanaharakani wenzake kana kwamba mkopo huo umetokana na juhudi zake na wanaharakati wenzake. Kweli kuongozwa na huyu jamaa kama kiongozi wako wa chama ni shida!
Kwenye makala yangu ile nilisema Maalim Seif kwa upande mwingine ni Sultani. Kwenye kila chama anachokuwemo Maalim Seif, kila mpemba aliyemo kwenye chama hicho anakuwa kiongozi na thamani zaidi ya kiongozi yeyote wa bara. Mpemba anaweza kuelekeza jambo lolote ndani ya chama alichomo Maalim Seif.
Msimamo na malengo ya chama ni lazima yajikite Zanzibar kibajeti na kimikakati. Lazima kutakuwa na kikao cha wazanzibari walioko kwenye uongozi wa chama hicho nje ya vikao vya chama vya kikatiba kabla na baada ya vikao hivyo. Kila mtanganyika ni adui wa Zanzibar hata kama ni mwanachama wa chama alichomo Maalim Seif.
Maalim Seif ni Sultani wa pili wa Zanzibar baada ya yule wa kwanza kuondolewa kwa mapanga kwenye mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964. Sultani wa pili anawekwa mbali na ikulu kwa sanduku la kura! Sultani huyu ana wapambe wake akina Ismail Jussa Ladhu, Salim Bimani, Nassor Mazrui na Issah Kheri. Kwenye chama chochote alichomo Maalim Seif, yeye na hawa wapambe wake ndio watakuwa na maamuzi.
Naweza kutamka bayana sasa kwamba kwenye mpambano kati ya Zitto na Maalim Seif, tayari Maalim ana ‘point’ moja! Amejipanga tayari ndani ya ACT tena akiwa makini asirudie makosa aliyoyafanya kwenye CUF mpaka kuja kutimuliwa. Zitto alipomtaka Maalim kwenye ACT alipewa masharti ambayo Maalim alijua kabisa kwamba yatamlinda atakapoanza usultani wake. Alipelekwa mpaka kwa wazee wa Pemba wakamwapisha na kumpa masharti akakubaliana nayo!
Akihojiwa na Shirika la Habari la BBC kabla ya uchaguzi wa ndani ya ACT, Maalim aliulizwa kwamba tayari alishapewa nafasi ya kuwa Mshauri Mkuuwa chama hicho kwa nini amechukua fomu ya kugombea uenyekiti? Akajibu kwamba, “Ukiwa mshauri unashauri na ushauri wako unaweza kukubaliwa au kukataliwa. Mimi nataka niwe Mwenyekiti ili niweze kufanya maamuzi siyo kushauri!” Sultani huyo!
Mwaka jana nilisema, “Hivi tunavyozungumza karibu wote hawa na wengine wengi wa upande wa Maalim Seif wameshaingizwa kwenye kamati kuu. Baada ya uchaguzi wa ndani ya chama, watazidi kuingia wengine.” Fuatilia leo ‘composition’ ya Kamati Kuu ya ACT uone. Theluthi mbili ni watu wa Maalim Seif.
Nilisema, “Tayari mikakati ya ‘kuwapiga chini’ baadhi ya viongozi wa zamani ndani ya ACT imeshaanza. Hata uchaguzi uliosimamiwa na viongozi wa zamani kwenye majimbo na mikoa nusura ufutwe na kamati kuu ili uanze upya.” Leo ninapoandika makala hii kuna barua za viongozi wa ACT-Wazalendo mikoa mitatu ya Ruvuma, Singida na Manyara ziko kwa Msajili wa Vyama. Viongozi wote hawa wanalalamikia kuenguliwa kwenye mkutano mkuu wa chama uliofanyika Machi 14 mwaka huu uliowachagua akina Zitto Kabwe na Maalim Seif.
Kutoka upande wa bara ni majimbo 68 tu yaliyoruhusiwa kupeleka wajumbe kwenye mkutano huo wakati Zanzibar majimbo yote yaliruhusiwa. Nia ilikuwa ni kuhakikisha wajumbe wa bara ambao ndio wangewanya kura zao kati ya Maalim Seif na Yeremiah Maganja, wanakuwa wachache sana. Lengo lilikuwa wajumbe wote wa Zanzibar wakimpa kura Maalim Seif na wachache wa bara wakagawanyisha kura zao, ni rahisi Maalim kushinda. Ndivyo ilivyokuwa wakiongeza na mbinu nyinginezo, Maalim akashinda kwa asilimia 93.
Mabadiliko ya Katiba ya ACT nayo ni kwa ajili ya kumsaidia Maalim Seif. Tutayajadili wakati utakapowadia. Tusubiri kwanza wayapitishe mabadiliko hayo!
Sent using Jamii Forums mobile app
Maalim Seif alidai Lipumba alishajiuzulu uenyekiti wa CUF toka Agosti 2015 akipinga chama chake kumuunga mkono Edward Lowassa kama mgombea urais wa ushirikiano wa UKAWA. Maalim alidai kwamba Mkutano Mkuu wa CUF ulikutana na kukubali ombi la Lipumba la kujiuzulu.
Lakini Prof. Lipumba anadai kwamba kabla mkutano mkuu haujakutana kujadili ombi lake la kujiuzulu, alikutana na Maalim Seif wakazungumza na kuona umuhimu wa yeye kurudi kwenye uenyekiti na hivyo akaandika barua ya kufuta barua yake ya kujiuzulu. Kwa lugha nyingine Lipumba anasema kwamba wakati mkutano mkuu maalum unajadili kujiuzulu kwa Lipumba, ulikuwa unajadili barua hewa ambayo haikuwepo ilikuwa imeshafutwa!
Baada ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kukubaliana na hoja za Lipumba na kuamua kumtambua kama Mwenyekiti halali wa CUF, Maalim Seif na kundi lake waliamua kukimbilia mahakamani. Kesi iliunguruma na hatimaye mahakama nayo kwenye hukumu yake ikakubaliana na upande wa Lipumba na kumtambua kama mwenyekiti halali wa CUF. Siku hiyo hiyo Mahakama ilipotoa hukumu yake ndiyo Maalim Seif na kundi lake walihamia ACT-Wazalendo.
Miezi mitatu baadaye yaani Juni 18, 2019 niliandika makala yenye kichwa cha habari: “Zitto ajiandae kupambana na Maalim Seif, hana hadhi ya kupambana na JPM. Nitakumbusha kidogo kwa nini nilisema wawili hawa lazima watapambana mbele ya safari. Moja nilisema huyu kijana ni mnafiki, kigeugeu na asiyeaminika! Akisema hasemi ukweli, akiaminiwa haaminiki na akiweka ahadi hatekelezi!
Zitto anaweza kuongea kama mpambanaji mkubwa dhidi ya ufisadi na wizi nchini kumbe ndiye fisadi wa kutupwa! Anaweza kuongea kama mzalendo namba moja wa nchi yake, kumbe msaliti na kibaraka namba moja wa mabeberu. Zitto ukiongea naye jambo usiku saa 3, usitegemee kwamba kukicha saa 12 asubuhi bado atakuwa nawe katika kile mlichoongea. Unaweza kukuta alishakugeuka ndani ya masaa 9 tu ya usiku.
Nilisema wazi kwamba nimekaa na kufanya kazi na wanasiasa wengi tokea niingie rasmi kwenye siasa. Katika wanasiasa wote niliofanya nao kazi mpaka leo, sijawahi kuona mwanasiasa mnafiki kama Zitto Zuberi Kabwe! Katika wanasiasa waliopata kuwa marafiki zangu sana kwenye siasa za nchi hii ni Freeman Mbowe, Zitto Kabwe, Anthony Komu, Kitila Mkumbo na Peter Mwambuja! Kati yao hakuna mnafiki, kigeugeu na asiyeaminika kama Zitto!
Hakuna mwanasiasa aliyewahi kumwamini Zitto Kabwe akaaminika. Kuanzia Freeman Mbowe aliyemwingiza kwenye siasa za kitaifa mpaka Kitila Mkumbo ambaye Zitto kwa kinywa chake aliwahi kututamkia kwamba Kitila ndiye alikuwa injini yake. Kwa kifupi Zitto aliaminiwa na Freeman Mbowe, Willibrod Slaa, Marehemu Chacha Wangwe, Anthony Komu na wakurugenzi wenzake wa makao makuu ya CHADEMA, Marehemu Bob Makani, Marehemu Philemon Ndesamburo, Marehemu Amani Kabourou, hakuaminika!
Aliaminiwa na vijana wake waliokuwa tayari kumsaidia kwa lolote dhidi ya Mbowe: akina Ben Saanane, Habibu Mchange, Juliana Shonza na Mtera Mwampamba lakini hakuaminika! Maswahiba wake wa kufa na kuzikana akina Msafiri Mtemelwa na David Kafulila nao wakamwamini lakini hakuaminika!
Kitila naye alimwamini Zitto lakini aliishia kuwa mhanga wa huyu mwanasiasa mdogo lakini aliyeumiza wengi! Zitto aliyedai kwamba kumwachanisha na Kitila ni sawa na kumwondoa kwenye siasa, ndiye Zitto aliyefanya mkutano na wanaandishi wa habari na kudai chama kimebariki uteuzi wa Kitila Mkumbo kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji. Lakini nataka nikuhakikishie kwamba ni Zitto huyo huyo aliyeanzisha mchakato wa siri wa kumvua Kitila uanachama wa ACT-Wazalendo baada ya kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara kwenye serikali ya CCM.
Huyo ndiye Zitto Kabwe aliyekuwa upande wa Lipumba wakati mgogoro wa ndani ya CUF umeanza. Alimsaidia Lipumba kwa kumpa vijana wa kufanya fitna. Lakini pia alimpa Lipumba wanasheria wa kumtetea kwenye kesi aliyofunguliwa na upande wa Maalim Seif. Kabla kesi haijaisha akahamia upande wa Maalim Seif na leo Maalim Seif ni mwanachama namba moja wa ACT na Mwenyekiti Taifa wa chama hicho.
Huyu ndiye Zitto Kabwe ambaye kwenye makala ile nilisema wazi kwamba, “Nguvu anazotumia kupambana na ‘jabali’ JPM anazipoteza bure na atazijutia. Magufuli anazidi kuchanja mbuga. Treni yake ya kuelekea uchumi wa kati imeshika kasi na kama Zitto anadhani anaweza kuizuia kwa tamaa yake ya madaraka, asimame relini kujaribu kuizuia ‘treni’ hii aone itakavyompasua vipande vipande! Nguvu anazotumia kupambana na Magufuli, azitunze aje azitumie kupambana na Maalim Seif.” Samson Mwigamba, Kalamu ya Mwigamba, Juni 18, 2019.
Kama utabiri huu alidhani ni ndoto za mchana, akumbuke matukio ya hivi karibuni tu wala asiende mbali. Akumbuke alivyoumbuka siku alipojaribu kumsingizia Rais Magufuli kwamba amemfukuza kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Prof. Mohamed Janabi. Aangalie alivyokurupuka na jinsi watanzania walivyomshambulia mpaka kwa aibu akaja kukanusha habari yake yeye mwenyewe!
Kama hiyo haitoshi atazame juhudi zote alizofanya kuzuia mkopo wa Benki ya Dunia kwa Tanzania kwa ajili ya Mradi Kabambe wa Kuboresha Elimu ya Sekondari nchini. Amefanya jitihada kubwa za kuandika barua kwa kutumia nembo ya bunge, ameenda mwenyewe Marekani kuwashawishi wasitoe huo mkopo. Wakati akifanya hayo yote Rais Magufuli alikuwa hapa nchini anaendelea na shughuli zake wala hakuwahi kumtuma hata Afisaelimu wa Mkoa kwenda kuzungumza na Benki ya Dunia!
Lakini Zitto ‘ameangukia pua’ baada ya Benki ya Dunia kutangaza kwamba itatoa mkopo huo kwa serikali. Maelezo yaliyotolewa na Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Dunia, maelezo ya Mkurugenzi wa Benki hiyo hapa nchini, ‘yamemvua nguo’ Zitto akabaki uchi wa kisiasa! Kwa aibu akaandika andiko la kuipongeza benki hiyo na wanaharakani wenzake kana kwamba mkopo huo umetokana na juhudi zake na wanaharakati wenzake. Kweli kuongozwa na huyu jamaa kama kiongozi wako wa chama ni shida!
Kwenye makala yangu ile nilisema Maalim Seif kwa upande mwingine ni Sultani. Kwenye kila chama anachokuwemo Maalim Seif, kila mpemba aliyemo kwenye chama hicho anakuwa kiongozi na thamani zaidi ya kiongozi yeyote wa bara. Mpemba anaweza kuelekeza jambo lolote ndani ya chama alichomo Maalim Seif.
Msimamo na malengo ya chama ni lazima yajikite Zanzibar kibajeti na kimikakati. Lazima kutakuwa na kikao cha wazanzibari walioko kwenye uongozi wa chama hicho nje ya vikao vya chama vya kikatiba kabla na baada ya vikao hivyo. Kila mtanganyika ni adui wa Zanzibar hata kama ni mwanachama wa chama alichomo Maalim Seif.
Maalim Seif ni Sultani wa pili wa Zanzibar baada ya yule wa kwanza kuondolewa kwa mapanga kwenye mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964. Sultani wa pili anawekwa mbali na ikulu kwa sanduku la kura! Sultani huyu ana wapambe wake akina Ismail Jussa Ladhu, Salim Bimani, Nassor Mazrui na Issah Kheri. Kwenye chama chochote alichomo Maalim Seif, yeye na hawa wapambe wake ndio watakuwa na maamuzi.
Naweza kutamka bayana sasa kwamba kwenye mpambano kati ya Zitto na Maalim Seif, tayari Maalim ana ‘point’ moja! Amejipanga tayari ndani ya ACT tena akiwa makini asirudie makosa aliyoyafanya kwenye CUF mpaka kuja kutimuliwa. Zitto alipomtaka Maalim kwenye ACT alipewa masharti ambayo Maalim alijua kabisa kwamba yatamlinda atakapoanza usultani wake. Alipelekwa mpaka kwa wazee wa Pemba wakamwapisha na kumpa masharti akakubaliana nayo!
Akihojiwa na Shirika la Habari la BBC kabla ya uchaguzi wa ndani ya ACT, Maalim aliulizwa kwamba tayari alishapewa nafasi ya kuwa Mshauri Mkuuwa chama hicho kwa nini amechukua fomu ya kugombea uenyekiti? Akajibu kwamba, “Ukiwa mshauri unashauri na ushauri wako unaweza kukubaliwa au kukataliwa. Mimi nataka niwe Mwenyekiti ili niweze kufanya maamuzi siyo kushauri!” Sultani huyo!
Mwaka jana nilisema, “Hivi tunavyozungumza karibu wote hawa na wengine wengi wa upande wa Maalim Seif wameshaingizwa kwenye kamati kuu. Baada ya uchaguzi wa ndani ya chama, watazidi kuingia wengine.” Fuatilia leo ‘composition’ ya Kamati Kuu ya ACT uone. Theluthi mbili ni watu wa Maalim Seif.
Nilisema, “Tayari mikakati ya ‘kuwapiga chini’ baadhi ya viongozi wa zamani ndani ya ACT imeshaanza. Hata uchaguzi uliosimamiwa na viongozi wa zamani kwenye majimbo na mikoa nusura ufutwe na kamati kuu ili uanze upya.” Leo ninapoandika makala hii kuna barua za viongozi wa ACT-Wazalendo mikoa mitatu ya Ruvuma, Singida na Manyara ziko kwa Msajili wa Vyama. Viongozi wote hawa wanalalamikia kuenguliwa kwenye mkutano mkuu wa chama uliofanyika Machi 14 mwaka huu uliowachagua akina Zitto Kabwe na Maalim Seif.
Kutoka upande wa bara ni majimbo 68 tu yaliyoruhusiwa kupeleka wajumbe kwenye mkutano huo wakati Zanzibar majimbo yote yaliruhusiwa. Nia ilikuwa ni kuhakikisha wajumbe wa bara ambao ndio wangewanya kura zao kati ya Maalim Seif na Yeremiah Maganja, wanakuwa wachache sana. Lengo lilikuwa wajumbe wote wa Zanzibar wakimpa kura Maalim Seif na wachache wa bara wakagawanyisha kura zao, ni rahisi Maalim kushinda. Ndivyo ilivyokuwa wakiongeza na mbinu nyinginezo, Maalim akashinda kwa asilimia 93.
Mabadiliko ya Katiba ya ACT nayo ni kwa ajili ya kumsaidia Maalim Seif. Tutayajadili wakati utakapowadia. Tusubiri kwanza wayapitishe mabadiliko hayo!
Sent using Jamii Forums mobile app