Ndio nafahamu hata ofisi yao niiliyo kuwa ya cuf wanachama wao siwafahamu
Nilishawahi kupita mitaa hiyo kipindi fulani ofisi yenyewe iko usawa wa makaburi ya Roma,kuna mafundi seremala.
Kulingana na Maelezo ya mleta uzi,mwenyekiti anae msema atakuwa ni yule aliyekuwa mwenyekiti wa CUF ni fundi wa kushona viatu na ni mchangamfu mzuri sana.
Siku moja katika mizunguko ya hapa na pale nilibahatika kuonana nae,nikamuuliza habari za chama chake cha CUF alinijibu kuwa siku hizi siko CUF niko ACT.
Nikamuuliza kuwa uliendaje ACT?akasema kuwa nilikuwa sina hili wala lile mara nikapigiwa simu na mtu mmoja aliye niuliza kuwa wewe si ndiyo mwenyekiti wa CUF wilaya ya Mbozi?akaitikia ndiyo mwenyewe,aliyepiga simu akajitambulisha kwake kuwa Mimi ni kiongozi wa ACT mkoa ninakuomba ufike mkoani ninamazungumzo na wewe.
Alipofika mkoani kesho yake alimkuta mwenyeji wake akiwa na wenzake waliotambulishwa kwake kuwa ni viongozi wa ACT Taifa.
Baada ya kutambulishana,aliambiwa kuwa tumepata habari zako za kiutendaji kwa hiyo tumekuita hapa ili utusaidie kukipeleka chama chetu Mbozi kama ni fedha zipo utapata za kutosha ambazo zitakuwa zinakusaidia kwenye shughuri za kichama na kimaisha.
Alisema kuwa nilipo sikia fedha hapohapo uzalendo wa CUF ulinitoka ni kahamia rasimi ACT na kupewa nafasi ya mwenyekiti wilaya.
Nikamrushia la kwangu na Mimi ninaomba unigawie hata kidogo basi,alijibu kuwa mbali na nauli niliopewa hawakuweza kunipa fedha zaidi ya hiyo,wamesema kuwa wakifika Dar watanitumia,Mimi siwezi nikakuficha wewe,mwisho wa mazungumzo.